Ushauri: Kwenda kusoma Iran

Ushauri: Kwenda kusoma Iran

Kusoma ni jambo moja

Mazingira ya kusomea ni jambo la pili la muhimu zaidi

Binafsi Iran na Iraq nisingeenda kwa sababu hiyo ya pili
Iran ni nchi salama haina shida kama iraq ndugu
 
Habari zenu wakuu!

Mimi ni mtanzania niliefadhiliwa kwenda kusoma Iran, program DOCTOR OF MEDICINE.

Kwa nyie mnavyoijua Iran,mungenishauri niende au niikache mana sina aidia yoyote kuhusu Iran.
Sio unaenda kusomea ugaidi kweli?
 
Ingekuwa mimi ningeenda bila kusita kabsa...na ni kwasbb..moja....tv hiz huwa zinatuaminisha sana vitu ambavyo viko kinyume na hali halisi...ni kweli iran ina mzozo na mataifa makubwa ikiwamo israel lakin maisha ya kawaida ya kijamiii yanaendelea kama kawaida tu. Kikubwa ukienda roma...ishi kama waroma...usiwapelekee mbwembwe...jamaa wako siriaz na taratibu zao...!
Ni kweli tv zinatuaminisha vitu ambavyo havipo.iran kiusalama imetulia nenda kasome nina ndugu zangu wawili wapo huko ni fresh tu.
 
Habari zenu wakuu!

Mimi ni mtanzania niliefadhiliwa kwenda kusoma Iran, program DOCTOR OF MEDICINE.

Kwa nyie mnavyoijua Iran,mungenishauri niende au niikache mana sina aidia yoyote kuhusu Iran.
Nenda kasome iran taaluma yao iko juu sana huwezi kulinganisha na sisi hapa .pia suala la usalama usiogope maisha ndani ya iran ni amani kabisa na.yakawaida .na kwasasa wameondolewa vikwazo mataifa mengi yatapelekwa watu huo kubadilishana taaluma
 
Ni kweli tv zinatuaminisha vitu ambavyo havipo.iran kiusalama imetulia nenda kasome nina ndugu zangu wawili wapo huko ni fresh tu.
nashukuru lolowapi,samahani lakin kama aitaleta shida unaweza kuniunganisha na mmoja wapo kama anaweza akanipa detailz zaid
 
Nenda kasome iran taaluma yao iko juu sana huwezi kulinganisha na sisi hapa .pia suala la usalama usiogope maisha ndani ya iran ni amani kabisa na.yakawaida .na kwasasa wameondolewa vikwazo mataifa mengi yatapelekwa watu huo kubadilishana taaluma
nashukuru kwailo koyola mana nilikuwa cjui hilI wala lile about iran
 
nenda wakakung'oe kende, ukimaliza uende na somalia kupiga masters na phd umalizie syria.
 
Nenda usichelewe maana hata kama ni kifo kinaweza kukukuta hata hapa nyumbani. Usiogope Mungu atakulinda na utarejea tena hapa nyumbani.
 
Nenda usichelewe maana hata kama ni kifo kinaweza kukukuta hata hapa nyumbani. Usiogope Mungu atakulinda na utarejea tena hapa nyumbani.
nashukuru sana sungurajv for inspiration na kuntia moyo pia
 
Habari yako kk!
Kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kwenda kusoma Iran.
BINAFSI mm ni mwanafunzi nasoma Biomedical engineering huku Russia.Mara ya kwanza nilipopata chua watu wakaanza kunishauri vitu vingi ambavyo vilikuwa negative kama mambo ya ubaguzi,usalama na baridi.nikisikiliza ushauri wao na baada ya muda nikaamua kwenda kusoma russia mji mmoja unaitwa Tambov.nikisoma lugha huko tambov na baada ya mwaka nikamaliza.nikiwa tambov sikuwai kupata tatizo lolote la ubaguzi,usalama au hata michongo ya baridi.nilipo maliza lugha Tambov nikaamua kuama mji kwenda kusoma mji mwingine unaitwa Vladivostok.mjii huu wa Vladivostok ni mji ulipo mbali sana KUTOKA mji mkuu wa urusi moscow na mji ambao nilikuwa nasoma mwanzo.watu wakaanza kunishauri mambo kibao kuhusu kuama kwangu kwani mji huu wa Vladivostok haukua na mwafrika hata mmoja na mi ndo nikikuwa wakwaza kwanza.lakini nikaamua kwenda na nilipofika huko nikakutana na mambo ambayo sikutegemea maana nilikuta watu wa huko ni wakarim sana na maisha ya huko yalikuwa mazuri kuliko sehemu yoyote ile niliopata kushi ndani ya urusi japo mwafrika nilikuwa peke yangu.
Hoja yangu ni kuwa ni vizuri kuomba ushauri but unapofanya maamuzi jalibu kuangalia ni kipi moyo wako unataka mana wao wanaokupa ushauri wanasema ivyo labda kwa kusikia sikia tu au kwa jinsi walivyo jionea japo kila mtu anastail tofauti za kuishi so haimaanishi jinsi alivyoishi au yaliyomtokea fulani na ww yatakutokea.
Ushauri wangu nenda kasome mana KUTOKA tu nje ni faida sana hasa kama unajitambua mana licha ya masomo utajifunza mengi sana
 
Back
Top Bottom