ISLETS
JF-Expert Member
- Dec 29, 2012
- 8,121
- 5,332
Wamajamvi salaam kwenu wakuu.
Mwezi wa saba wanafunzi wengi wataanza masomo ya Advance. hata kama sio wewe yawezekana akawa ni rafiki yako, ndugu yako au hata mtoto wako anataka kaja kuwa DAKTARI au MFAMASIA basi ni vyema kujua hali ya kitaaluma ya shule utakayopangiwa.
ninamaanisha kuwa kuna watu wengi waliofaulu vizuri form 4 lakini wakafeli vibaya form6 au kuwa ufaulu finyu.
wanafunzi wengi wa science A level wanategemea tuition na wanafaulu kupitia huko. Shule nyingi walimu hawafundishi vizuri na pia unakuta hata vitabu husika maktaba havipo.
sasa mzazi anaingia gharama kumnunulia mwanaye vitabu na ada za tuition ambazo ni ghali si kama vya O Level.
ni mazingira ambayo nimeyaona mwenyewe pindi nikiwa shuleni lakini na kusikia malalamiko kwa watu wengine ambapo licha ya jitihada nyingi wengi wameishia kufeli.
Science sio mchezo hasa PCB japo tumetofautiana uwezo kiakili.
ukiona tangu umeingia Form 5 umesoma miezi 7 (mpaka mwakani mwezi wa tatu) lakini ufaulu wako unasua sua achana na hiyo shule. .maana huko unakoenda ndio kugumu zaidi. SURELY
MTU HUYO NINAMSHAURI AKASOME DIPLOMA YA COURSE ANAYOIPENDA MFANO CLINICAL MEDICINE ukutoka huko unapata kazi na pia unaweza kwenda kusomea degree ya MD- UDAKTARI/ MEDICAL DOCTOR.
wengi wanaosoma PCB au CBG wanapenda kuwa madaktari lakini sio siri shule huwa zinazima ndoto za wengi.Mtu anasoma kwa bidii lakini bado anafeli. Sasa kuliko kupoteza muda wa miaka miwili na pesa ni vyema kujaribu Diploma.
Sijui ugumu wa diploma lakini wengi wanasoma wanasema kuna unafuu.
jamani ni ushauri tu maana nimeona wengi wa dizaini hiyo walivyopata shida.
Kusoma diploma haimaanishi umefeli ni njia mojawapo tu ya kuelimika na kufaidi matunda ya elimu yako.
Tafakari mara mbili kisha kuchua hatua.
Nawasilisha.
Mwezi wa saba wanafunzi wengi wataanza masomo ya Advance. hata kama sio wewe yawezekana akawa ni rafiki yako, ndugu yako au hata mtoto wako anataka kaja kuwa DAKTARI au MFAMASIA basi ni vyema kujua hali ya kitaaluma ya shule utakayopangiwa.
ninamaanisha kuwa kuna watu wengi waliofaulu vizuri form 4 lakini wakafeli vibaya form6 au kuwa ufaulu finyu.
wanafunzi wengi wa science A level wanategemea tuition na wanafaulu kupitia huko. Shule nyingi walimu hawafundishi vizuri na pia unakuta hata vitabu husika maktaba havipo.
sasa mzazi anaingia gharama kumnunulia mwanaye vitabu na ada za tuition ambazo ni ghali si kama vya O Level.
ni mazingira ambayo nimeyaona mwenyewe pindi nikiwa shuleni lakini na kusikia malalamiko kwa watu wengine ambapo licha ya jitihada nyingi wengi wameishia kufeli.
Science sio mchezo hasa PCB japo tumetofautiana uwezo kiakili.
ukiona tangu umeingia Form 5 umesoma miezi 7 (mpaka mwakani mwezi wa tatu) lakini ufaulu wako unasua sua achana na hiyo shule. .maana huko unakoenda ndio kugumu zaidi. SURELY
MTU HUYO NINAMSHAURI AKASOME DIPLOMA YA COURSE ANAYOIPENDA MFANO CLINICAL MEDICINE ukutoka huko unapata kazi na pia unaweza kwenda kusomea degree ya MD- UDAKTARI/ MEDICAL DOCTOR.
wengi wanaosoma PCB au CBG wanapenda kuwa madaktari lakini sio siri shule huwa zinazima ndoto za wengi.Mtu anasoma kwa bidii lakini bado anafeli. Sasa kuliko kupoteza muda wa miaka miwili na pesa ni vyema kujaribu Diploma.
Sijui ugumu wa diploma lakini wengi wanasoma wanasema kuna unafuu.
jamani ni ushauri tu maana nimeona wengi wa dizaini hiyo walivyopata shida.
Kusoma diploma haimaanishi umefeli ni njia mojawapo tu ya kuelimika na kufaidi matunda ya elimu yako.
Tafakari mara mbili kisha kuchua hatua.
Nawasilisha.