Ushauri kwa waislamu Tanzania, hasa walio mtandaoni

Ushauri kwa waislamu Tanzania, hasa walio mtandaoni

bank ya vatican ndo imewafundisha mkombozi bank jinsi ya ku laundry pesa,juu wao wana uzoefu tangu kipindi cha adolf hitler

Mkuu umekula data za kutosha kuhusu kanisa, ni kweli Cathoric Church ilianza kipindi cha dark period by Constantine the great, kwa kipindi kile kanisa ndiyo lilikuwa likiongoza nchi na kiongozi wa nchi ni lazima alikuwa wa dini husika, anglican cathoric or vyovtote.

Kanisa likawa tajiri sana na kupelekea lenyewe kuongoza uchumi wa dunia kipindi hicho(300 Baada ya Yesu kupaa mbinfuni).Kanisa lili jikita katika kutengeza rasilimali watu wenye elimu ya juu sana, yaani Masters tangu kipindi hicho.

Watendaji wake wote(mapadre) walitakiwa kuwa watu wenye ujuzi wa kufahamu mambo mengi sana ikiwemo hata uwekezaji na ndiyo maana walipoamua kueneza dini yao waliyazingatia mambo hayo muhimu kuwa

i. Walihakikish wanajua mipango miji yaani mji unaelekea wapi na wao hawakuhangaika kupigana wa wenyeji bali walienda maporini na jujichukulia maeneo ya kutosha ila wakijua kuwa baada ya muda hatakama itachukua miaoa 20 lazima mji utafika mahala pale,

ii.Walijenga shule kuhakikisha kuwa wanapata waumini wenye uelewa na wanaoweza kuwasaidia kirahisi(Cracks).

iii.Walijenga hospitali,kwa ajili yao na jamii inayowazunguka kwani kuwezi kufanya kazi mahala ambapo watu hawana uhakika na afya zao.

Baada ya hapo kadri miaka inavyokwenda waliingia mpaka kwenye uwekezaji wa mabenki kama ulivyo sema na kwa taarifa yako hii biashra ndiyo ilichangia kufa kwa papa John Paul 1.Father Lucian Alban, mwitariano wa kweli, siku thelatjin na tatu tu tangu asimikwe kuwa Papa.soma David Yalop..,

Sitaki kukataa kwamba kanisa katoliki si kanisa la kimkakati kwa maana halifanyi vitu kwa bahati mbaya na ni kwa sababu watendaji wake wote wamesona vizuri.

Ila hii haifanyi nikaunga mkono eti kwamba mpaka sasa linafanya hivyo, hapana kwa sasa kanisa si kiongozi wa serikali tena na si lazima lilipo mtu wake ndiye awe kiongozi wa nahala pale hivyo kwa sasa kuna mabadiliko makubwa na kamwe Roma haiwezi kutoa maelekezo yoyote kwa matawi huku.

Yaani huwezi amini zamani hela zilitoka roma kuja Tanzania kwenye miradi ya kanisa ila akwa sasa mnajenga wenyewe na nyingine mnapeleka roma, we tembelea tu jumuia ndogondogo utaona watu wanavyokamuliwa na michango.

Hao walio pitisha pesa za wizi ni wao wenyewa hakuna benki wala mtu aliye watuma.
 
Kwani chuo kikuu cha kiislamu morogoro wanafunzi wanasoma bure??? Pamoja na kwamba wote ni waislamu.
Sasa sijui kama chuo cha morogoro waislamu wote,wala si mbaya,mi shuleni mwislamu nilikua mimi tu katika watu karibu 500,kwahiyo siyo ishu.
point yangu ni kuwa shule za kidini ambazo si seminary zinapokea mwanafunzi wa imani yeyote provided analipa ada.
hospitali za misheni wanatafuta pesa kwahiyo hawachagui mteja.
 
Mkuu Uko Sahihi! Lakini Kuna Kitu Ambacho Wanadai Kimeua Taasisi Nyingi Za Kiislam Toka Kianzishwe! Nacho Ni BAKWATA Ambayo Wengi Wao Hudai Ni Chombo Kinachosimamiwa Na Sirikali. Dhehebu La AnsarSuna Ambalo Mara Nyingi Hupingana Na BAKWATA Ndilo Sehemu Pekee Ya Uislam Ambayao Ndio Yenye Kuangaza Maendeleo Ya Uislam Tz, Ndio Walioanzisha Chuo Kiku Cha Kislam Morogoro, Ndio Wenye Vyombo Vya Habari Mfano Tv Iman, Radio Iman, Saut Ya Quran,magazeti Ya Alhuda, Anuur Nk. Lakini Bakwata Sijajua Wanamiliki Nini. Hawa Hawa Ansarsuna Ndio Hawaitaki Kabisa Mahakama Ya Kadhi Ila BAKWATA Ndio Wanaoipigania Mahakama Ya Kadhi. Hata Mimi Nashawishika Kuamini Kua BAKWATA Ndio Wanatakiwa Kubebeshwa Lawama Zote.
Kulikuwepo na east africa muslim welfare society kama sikosei,na ilikuwa imewekeza katika elimu na mashule etc.
sijui mashehe walimkosea nini julius kambarage,aliifuta hiyo jumuia na kuanzisha bakwata
, ambayo ilipewa kazi ya kutangaza mwandamo wa mwezi tu.
mambo ya shule wakaambiwa zipo za serikali,hospitali hivyohivyo.
bakwata wakamsikia baba wa taifa na kukaa.
ni mpaka wakati wa mzee ruxa ndo pakaanza kuwepo taasisi za kiislamu tofauti na bakwata na ndo walioanza tena harakati za kujenga mashule
 
Na mimi kama Muislam nakushauri huu ushauri wako upeleke Kanisani.

Kawaambie hivi toka toka uhuru mpaka sasa wasomi wa Kikirsto wamejazana serikali kila idara wamelisaidiaje taifa letu kutoka kwenye nchi masikini duniani, unajua kuwa Tanzani ipo kwenye nchi 20 masikini wa kutupwa duniani huko serikalini kazi yenu kufanya ufisadi tu.

Halafu nyie Wakirsto ndiyo mnabebwa unajua kama kila mwaka Kanisa linapewa bilioni 61.9.

Ahsante.
haa haa suala la ufisadi halina dini mkuu, unawakumbuka kina daudi balali? Kina rostam aziz, jakaya kikwete walivyohusika kwenye Epa? Mkuu sio vizuri matendo ya mtu kuyaingiza moja kwa moja kwenye imani au dini yake. Kwa mfano ikiwa muislamu mmoja amezini, huwezi sema uislamu unapenda uzinifu kamwe! Pia suala la kanisa kupewa fedha na serikali tuwekee uthibitisho hapa!
 
Hakuna jambo linalodhalilisha uislamu kama hili linaloendelea kwa sasa kwa taifa letu, yaani kudai serikali ibebe mzigo wa kuendesha sehemu ya mambo yao ya ibada kupitia mahakama ya kadhi, huu ni ushahidi mkubwa kwamba uislamu umeshindwa kusimama wenyewe ili kujiendesha mpaka utegemee serikali ambayo inayo watu wanaoamini uislamu na wasioamini uislamu, hili ni kosa la mwaka. Pia serikali hiyo inayoombwa igharimie mzigo wa mahakama ya kadhi inapata mapato yake kutoka kwenye vyanzo haramu vingi kwa mfano, mabeki yanayotoza riba, kodi kutoka kwenye sigara, vilevi na hata kodi ya kwenye mabucha kama vitimoto. Je uislamu uko tayari kugharimiwa toka vyanzo hivyo vya mapato haramu? Je waislamu wao wenyewe wameshindwa kuchangisha pesa halali na kuiendesha mahakama hii? Kwa kweli kinachotaka kutendeka ni haramu juu ya haramu.
 
WanaJF,
Nimefikiria muda mrefu kuhusu sakata hili la kufa na kupona la mahakama ya kadhi. Ni wazi kuwa mahakama ni muhimu katika jamii. Lakini pamoja na umuhimu wake, nadhani tukikaa chini na kutafakari, kuna mengi ya umuhimu zaidi. Jambo la kwanza kwa Nchi kama Tanzania ambayo kwaajili ya uongozi mbovu wa waliokuwa madarakani kwa nyakati tofauti lingepaswa kupewa kipaumbele ni Elimu. Ona jinsi Elimu inavyochezeshwa gwaride, hadi tumefikia hatua ya kuweka div. 5, ili kuficha waliofeli.

Nirudi kwenye mada,
Nasema ushauri kwa waislamu kuwa waongeze nguvu kwenye elimu dunia. Waongeze shule zinazoendeshwa na taasisi za kiislamu, zenye ubora. Waongeze vyuo vikuu vinavyoendeshwa na taasisi za kiislamu, wakitaka wawapokee waislamu tu haidhuru, lakini ni bora wakawapokea wote kama zifanyazo taasisi za kikristu. Elimu bora Tanzania inahitajika. Na Elimu bora Tanzania haiwezi kutolewa na Serikali tu. Ona madhehebu ya kikristo walivyoweka kipaumbele katika elimu. Hesabu tu vyuo vikuu vinavyoendeshwa na madhehebu ya kikristo. Hesabu shule za sekondari zenye ubora wa hali ya juu zinazoendeshwa na taasisi za kikristo. Sijui taasisi za kiislam zinaendesha vyuo vikuu vingapi, lakini nafahamu walau moja ile ya Morogoro, iliyokuwa chuo cha Tanesco, ambayo walipewa na serikali ili kuwatuliza.

Tazama kwenye afya, ona ni vituo vingapi vya afya, hospitali, hadi hospitali za rufaa zinazoendeshwa na taasisi za dini? Nafahamu walau hospitali ya rufaa ya KCMC na Bugando zinaendeshwa na taasisi za kikristo. Hospitali za kawaida ni nyingi. Zinazoendeshwa na taasisi za kiislamu sizifahamu, zinaweza kuwa nyingi kuliko hizo, au la. Kwenye suala la afya ndipo pa kutumia nguvu nyingi. Huko ndipo pa kuwa na hitaji la kuweka kambi Bungeni kama kutakuwa na haja.

Nadhani sio vizuri kusubiri siku zote kubebwa na serikali. Kila madhehebu wana sheria zao, sheria zao ambazo hazipaswi kwenda kinyume na sheria za Nchi. Sioni sababu ya kutumia nguvu kubwa kudai mahakama badala ya kuwekeza kwenye mambo ya maandeleo kama elimu, afya, nk. Kwanini tunadhani maisha yetu lazima kupelekana mahakamani?

Ndiyo maana nasema natoa ushauri kwa waislamu hasa waJF maana ndo watakaosoma ushauri huu, Waislamu wawekeze nguvu nyingi kwenye mambo ya maendeleo zaidi kuliko mahakama. Wawekeze kwenye elimu na afya. Achaneni mambo ya mahakama. Mahakama ya nchi inaweza kumaliza yote, ikiwa kutakuwa na haja. Lakini kwa mtu optimistic hawezi kutumia nguvu nyingi kwenye hilo.

Sio haki kwa wabunge: wawakilishi wa wananchi kupoteza muda kujadili kuwa waislamu wawe na mahakama ya kadhi au la. Ni wazi watajadili, hasa wakati huu tunapokaribia uchaguzi. Ili kila mchangiaji aonekane anawajali waislamu, ataunga mkono mahakama ya kadhi, watafanya funika kombe mwanaharamu apite. Ili tu waislamu wa jimbo lake wasimtose, ili tu waislamu wasikikatae chama chake. Lakini nasema tena sio haki wabunge wapoteze muda katika jambo hili ambalo sio kipaumbele cha taifa. Sio haki lakini litajadiliwa kwaajili wa woga wa kupoteza kura.

Mniwie radhi, kama kuna moja hatapendezwa na ushauri wangu. Ukweli utabaki kuwa kuwekeza kwenye elimu, hasa elimu dunia na afya ni bora kuliko kuwekeza kwenye mahakama.
mkuu hongera sana kwa ushauri mzuri hawa kama hawataki kusikia yatakuja kuwatokea puani
 
Hawa watu wanatakiwa kusoma hata kama ni kwa lazima kwa sabbu kwa kweli, kukosa kwao elimu ndiko kunakopelekea wawe wanaongea wanayoyasema. Jamaa hawanaga uwezo wa kujenga hoja, jamaa hawana uwezo wa kuelewa hata simple phrases, halafu hawajui kama hawaelewi, jamaa hawana uwezo wa kujadili kwa point wala kujibu swali kama linavyoulizwa; jamaa hawa kwa kujua hawana hoja wamejikita zaidi kwenye ubishi wa kila kitu kwa makelele, matusi, fujo na vitisho.

Terror approaches!. Utasikia wanasema "msipotupa hiki mtaona", msipofanya hivi, tutaonyeshana adabu", mara utasikika, "...mkikataa hiki, tutafanya kama boko haramu",.."mahakama ya kadhi ni lazima hata kwa jihadi". Hivi kinachowafanya wawe na approach za kigaidi ni mafundisho ya dini yao au ni ujinga na kukosa uwezo wa kujenga wala kuelewa hoja?

Ninakwenda kazini lakini usishangae watakapokuja hapa,yote niliyoyasema pale utayaona. matusi, vitisho, nguvu, fujo, vurugu za kijinga tu.

Ni afadhali serikali ilazimish waislam wote waende shule hata kama ikibidi ziwepo za watu wazima ili angalau halmashauri zikae kwenye order badala ya mahakama ya kadhi. Mahakama ya kadhi hawana uwezo wa kuiendesha na itazidisha migogoro miongoni mwao. Hainatija kwa taifa na hata kwa waislam walio wengi. Sana sana itanufaisha wale wanaotafuta kuajiriwa kule, na wanaoume wanaoamini katika ubabe dhidi ya wanawake na watoto wa kike. Hakuna la ziada.

Mahakama za kadhi ziko na zinafanya kazi, kwa nini leo zijadiliwe na bunge? Hizi ni za kidini, kwa nini ziingizwe kwenye katiba hata kama serikali haizihudumii? Wawaachie masuala yao ya kidini wayafanye wenyewe misikitini. Si jukumu la serikali kuweka kwenye katiba masuala ya dini.

Wakitumia neno la kuudhi dhidi yangu, wala sio tatizo, hata wakindiitukana. Ila ukweli utabaki huu, na ukweli huu utawasuta siku za usoni.
 
MIMI huwa NASHANGAA SAANA HAWA NDUGU ZANGU KALUBANDIKA WENZANGU WANAPOKUA MBELE YETU KUTAMBA KWAMBA WAO NI WASOMI NCHI HII

HIVI NDUGU ZANGU MMESOMA KITU GANI HASA??

MMESOMA MUAJIRIWE AU MMESOMA ILI KULISAIDIA TAIFA??

KAMA KIPIMO CHA MAENDELEO YA WATU NI ELIMU,NA TUJAAALIE WASOMI WENGI NI NYINYI

OKEY,,HIVI MMELISAIDIA NIN TAIFA HILI TOKEA LIMEPATA UHURU NA HUU USOMI WENU??

MNACHOFANYA NI KUIBA PESA NA KUPELEKA MAKANISANI TUH

TEH TEH TEH

MNA MSAADA GANI KWA TAIFA HILI??


TEH TEH TEH

HIZO HOSPITALS NA SHULE MMEJENGA WENYEWE??THUBUTU UWEZO HUO MUUTOE WAPI MASKIN WA KUTUPWA,,MISAADA KUTOKA KWA EX SLAVE MASTERS WENU THEN MJIONE MNA CHA KUTAMBA??


HA HA HA

MAHAKAMA YA KADHI KWETU NI MUHIMU ZAID YA UDHANIAVYO,,WEWE HAIKUHUSU NA HATUHITAJI USHAUR WAKO

:lol: :lol: :lol:
 
Ha ha ha ha

lol ndiyo wasomi wetu hawa

eti naenda kazini,,teh teh teh

kazin waende kufanya nin wewe,,kuiba???kila siku mnaamkia makazini,,mnafanya nin huko vya maana mbona nchi stil bado maskini tuh??
Hivi hii slogans za kwamba waislam hawana shule bado zipo tuh??

Maana naona teuzi zikifanyika na wakishika nyadhifa waislam wenye weledi wao mnaanza tena kulalama kwamba kuna upendeleo wa udini kwenye hizo teuzi yaani nyinyi jamaa sijui nani kawaroga aisee,,teh teh teh


halafu hii ya mahakama ya kadhi kwann inawachoma sana??

Haiwahusu,haiwagusi,na mmeambiwa haitumii pesa yenu,,its totally non of your bzness,,sasa shida nin??
hawa watu wanatakiwa kusoma hata kama ni kwa lazima kwa sabbu kwa kweli, kukosa kwao elimu ndiko kunakopelekea wawe wanaongea wanayoyasema. Jamaa hawanaga uwezo wa kujenga hoja, jamaa hawana uwezo wa kuelewa hata simple phrases, halafu hawajui kama hawaelewi, jamaa hawana uwezo wa kujadili kwa point wala kujibu swali kama linavyoulizwa; jamaa hawa kwa kujua hawana hoja wamejikita zaidi kwenye ubishi wa kila kitu kwa makelele, matusi, fujo na vitisho.

Terror approaches!. Utasikia wanasema "msipotupa hiki mtaona", msipofanya hivi, tutaonyeshana adabu", mara utasikika, "...mkikataa hiki, tutafanya kama boko haramu",.."mahakama ya kadhi ni lazima hata kwa jihadi". Hivi kinachowafanya wawe na approach za kigaidi ni mafundisho ya dini yao au ni ujinga na kukosa uwezo wa kujenga wala kuelewa hoja?

Ninakwenda kazini lakini usishangae watakapokuja hapa,yote niliyoyasema pale utayaona. Matusi, vitisho, nguvu, fujo, vurugu za kijinga tu.

Ni afadhali serikali ilazimish waislam wote waende shule hata kama ikibidi ziwepo za watu wazima ili angalau halmashauri zikae kwenye order badala ya mahakama ya kadhi. Mahakama ya kadhi hawana uwezo wa kuiendesha na itazidisha migogoro miongoni mwao. Hainatija kwa taifa na hata kwa waislam walio wengi. Sana sana itanufaisha wale wanaotafuta kuajiriwa kule, na wanaoume wanaoamini katika ubabe dhidi ya wanawake na watoto wa kike. Hakuna la ziada.

Mahakama za kadhi ziko na zinafanya kazi, kwa nini leo zijadiliwe na bunge? Hizi ni za kidini, kwa nini ziingizwe kwenye katiba hata kama serikali haizihudumii? Wawaachie masuala yao ya kidini wayafanye wenyewe misikitini. Si jukumu la serikali kuweka kwenye katiba masuala ya dini.
 
haa haa suala la ufisadi halina dini mkuu, unawakumbuka kina daudi balali? Kina rostam aziz, jakaya kikwete walivyohusika kwenye epa? Mkuu sio vizuri matendo ya mtu kuyaingiza moja kwa moja kwenye imani au dini yake. Kwa mfano ikiwa muislamu mmoja amezini, huwezi sema uislamu unapenda uzinifu kamwe! Pia suala la kanisa kupewa fedha na serikali tuwekee uthibitisho hapa!

sasa utalitofautisha vipi kanisa na escrow??

Ha ha ha ha

pale kila mwenye macho haambiwi tazama

hadi maaskofu ndani???

Hadi bank za kanisa ndani???

Teh teh teh

wakiulizwa eti wanasema zile ni fedha za matoleoo,,duuuh,,allahu akbar...!
 
Aceni ujinga wenu kwani nyie wacristo ndio mliotusomesha ss wailamu
Mmebebwa na serkali nyerere na kupewa ma bilioni ya sh
Hapo mtakosaje kuwa na mashule kama uyoga?

Nikupe taarifa tu watoto wetu kuwapa elimu ya dini tutaendelea hadi siku ya mwisho
 
...Sijui taasisi za kiislam zinaendesha vyuo vikuu vingapi, lakini nafahamu walau moja ile ya Morogoro, iliyokuwa chuo cha Tanesco, ambayo walipewa na serikali ili kuwatuliza ...
Sasa kwa taarifa yako chanzo cha madai ya mahakama ya kadhi ni kuwepo kwa hicho chuo cha kiisilamu kilichopewa majengo ya Tanesco. Jamaa walipopewa wakaanzisha shahada nyingi za elimu ya kiisilamu kama vile Bachelor of Laws with Shariah na Bachelor of Islamic Studies with Education. Kinachowaumiza kichwa ni kwamba wahitimu wawapeleke wapi? Ndipo madai ya kuanzisha mahakama za kadhi zinazogharamiwa na serikali yalipoanza kushika kasi.

Ninachotaka kusema ni kwamba hapa sio suala la kutoa elimu tu kwa waisilamu, bali elimu yenye ushindani katika soko la ajira ili tusilazimike kuanza kuforce ajira zitengenezwe na serikali!
 
Mkuu Dopas umenena kile ambacho huwa nawaza kila mara! Hawa watu badala ya kuwaza kuendeleza huduma za kijamii wanatoa povu kwa jambo la ibada! tena eti ligharamiwe na serikali! Maana yake wapate mishahara, posho nk kutoka serikalini kwa jambo la ibada! Nonsense kabisa.
 
imeandikwa "hamtakuwa rafiki zao hadi pale mtakapofuata yale wayatakayo". Hakuna neno zuri kama Quran, na ushauri mzuri zaidi ya sunnah ya Mtume Mohammad S.A.W

Tunashukuru, kwa vile ni ushauri basi sio lazima kuusikiliza. Mahakama ya kadhi must exist.
 
Back
Top Bottom