Aingie Kagame wapi wakati naye alishiriki mauaji, mpaka sasa anawauawa wanaompinga, vipi vita vya Congo nasikia ni Waislam.
Scenario zako haziendani lakini tujadli tu, ishu ya kongo ni ya kimfumo, hatuwezi kataa udikteta wa kagame pia, kwa hili la Kagame nilichotaka kuonyesha hapa ni ile hali ya wengi kukubali kitu halafu wachache wakatii, kwani siku zote mkuu hata kwenye familia yako si wote wanaokukubali ila watakuheshim kama wengi wanakukubali na hiyo ni asili(Nature), "wengi wape wachache wasikilizwe" kwa misri sivyo, wachache wanamwaga mboga kisa wamekosa ugali.
Kongo pia ni madaraka kama tu ya misri, na mimi kwa mawazo yangu tatizo la nchi zetu za Afrika ni kukosa viongozi.
Si kila mtu anayepata nafasi ya kutawala ni kiongozi, na kwa sababu uongozi ni mzuri so unapiganiwa na watu wote wema na waovu, kongo muda mwingi ilishikwa na mabutu seseseko, hakufanya lolote la maana zaidi ya kujitajirisha, hata baranara hakujenga kwa kuogopa kupinduliwa akawa anaruka kwa ndege tuu.
Nachelea kusema kabiala aendelee kuwepo madarakani angalau kwq kipindi flani ajaribu kuweka angalau hata taswira ya ki nchi lakini brother ulimwengu huu wa demokrasia ya vyamq vingi nashindwa kuliunga mkono wazo hilo ingawa sina uhakika hata hao wapinzqni kama watakuwa kweli na moyo wa kuwatumikia wakongo mani.
Kuna waasi mashariki mwa kongo ambao walimkimbia kagame kipindi kile anaingia madarakani(Interahamwe), ni vigumu kongo kuwaondoa kulingana na changamoto za kimfumo walizonazo kama, hawakuwa na jeshi isipokuwa wanamgambo tu, pia hamna njia yaani nchi haijqunganishwa ki miundombinu ya usafiri, hakuna muundo wa jueleweka wa ki usalama kama wa ki mtaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa mpaka taifa kulingana na hali yenyewe ya ki uongozi ilivyo.
Pia kongo madini kama yale ya katanga yalipelekea machafuko ya muda mrefu sana mpaka sasa m23 nao walienda kusini kujaribu bahati yao.
Yaani ishu ya kongo no terrible huwezi amini na kinachosumbua kongo si dini wala kabila ila nguvu kutoka nje ya kongo,
nadhani nitakuwa nimejibu swalilako kwani unaamini kuwa hata machafuko ya misri ni nguvu ya kutoka mataifa makubwa, sawa ni kweli ina haya bilq kupewa nafasi huwa hayawezi kuingilia na ndiyo maana huwa yana weka timing ya muda na muitikio wa umma.
Pia kongo wanao ua watu si wakongomani kwa wakongomani, ni makundi ya waasi ambayo yalimsaidia kabila senior kuingia ikulu, haya ni yale ya kitusi na kiganda.
So bado naona scenario ya kongo na misri pia hazishabiiani.