Mathayo Christopher
JF-Expert Member
- Dec 15, 2013
- 429
- 328
Si kweli wengi tumelelewa na baba au mama wa kambo hata wewe ukilea si mbaya MAISHA HAYANA KANUNI KAMA ZA HISABATI
Vipi kwa we kidume uliyezalisha na hujaoa, mwanao sio kikwazo ujapooa..... Au hii ndo maana ya mfumo dume....?
Sikubaliani na hoja zako kabisa hapo,wanawake wasumbufu sana kwenye ndoa ni hao hao watoto ambao hawajazaa hata mtoto mmoja,migogoro ya ndoa haijalishi umemuowa nani, kuna mengi sana ambayo yanasababisha hizo vurugu kwenye wala sio sababu wanawake waliokwishazaa,
jaribu kufanya research kidogo tazama ndoa za wanawake waliokwisha olewa na wale ambao ndio kwanza wameolewa ndoa za kwanza utakuja na majibu tofauti na uzi wako hapa,
wanawake walikwishazaa wakaolewa mara ya 2 ni watulivu kwenye ndoa na wanaheshima kuzidi hao wapya
Buy 1 get 3 for free.
Nalog off
Je, ukimuoa kwa sharti la mwanae kwenda kwa baba yake baada akifika umri wa miaka saba halafu mkabaki wewe na mkeo itakuwaje?..
je kama huyo aliyezaa naye alishafariki bado hizi factors zako zitakuwa valid?lakini usikariri mambo,usemi wako ni sawa na mtu anayesema kama mwanamke hana bikra hafai kuoa,je uliyemuoa wewe ni bikra ?
Walezi kwa walezi huwa hawaachani wanapumzishana tu kwa hiyo cha msingi ni kujitunza tu kma dada alivyo toa huo ushahuri hapo juu
sio kweli labda wale wenye umalaya wao tu, mtu ambaye mliachana wa kazi gani? basi inabidi mtu aoe bikra maana kama kufanya nikufanya tu
Dah! Nimesikitika sana, mi na kaka yangu, tumelelewa na baba wa kambo na katulea vizuri kwa mapenzi yote.
Kaka yangu alioa mke akiwa na watoto mapacha, wana miaka 15 kwenye ndoa sasa na wako happy,
Niliolewa nikiwa na mtoto tayari, Ila Nina 10 kwenye ndoa na wala mwanangu hajawahi kuwa tatizo,
Mara nyingi matatizo yanakuja iwapo baba wa kambo hatompokea mtoto yule kama mwanae.
Pia umaskini unachangia, mwanaume anaona kama kaongezewa majukumu,
Hivyo hoja hii sitoikubali kamwe