Habari za Leo
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 35 nimeoa na kubahatika kupata watoto wawili.
Nimeoa takribani miaka 6 iliyopita na mke wangu nilimtoa kijijini kutokana na hali yangu ya uchumi haikua sawa.
Changamoto iliyofanya kuandika huu uzi ni kwamba mke wangu habadiliki kabisa, ule ushamba wa kijijini bado anao. Nimejitahidi sana kumjali, kumpa pesa lakini habadiliki kabisa kuanzia uvaaji na hata kupendeza kitu ambacho hupelekea mimi kupata aibu kwa sababu inaonekana kama natesa familia.
Nimejitahidi kumpatia sehemu biashara zangu ili apate pesa na kununua baadhi ya mahitaji ya kujipendezesha lakini hakuna kitu.
Binafsi nampenda sana mke wangu, ni mpole na siyo msaliti ila nataka apendeze zaidi. Naombeni ushauri kama kuna njia naweza tumia ili mke wangu awe mzuri, bora na hadhi na apendeze. Inafika mpaka anazidiwa na wafanyakazi wangu tuliowaweka katika biashara.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 35 nimeoa na kubahatika kupata watoto wawili.
Nimeoa takribani miaka 6 iliyopita na mke wangu nilimtoa kijijini kutokana na hali yangu ya uchumi haikua sawa.
Changamoto iliyofanya kuandika huu uzi ni kwamba mke wangu habadiliki kabisa, ule ushamba wa kijijini bado anao. Nimejitahidi sana kumjali, kumpa pesa lakini habadiliki kabisa kuanzia uvaaji na hata kupendeza kitu ambacho hupelekea mimi kupata aibu kwa sababu inaonekana kama natesa familia.
Nimejitahidi kumpatia sehemu biashara zangu ili apate pesa na kununua baadhi ya mahitaji ya kujipendezesha lakini hakuna kitu.
Binafsi nampenda sana mke wangu, ni mpole na siyo msaliti ila nataka apendeze zaidi. Naombeni ushauri kama kuna njia naweza tumia ili mke wangu awe mzuri, bora na hadhi na apendeze. Inafika mpaka anazidiwa na wafanyakazi wangu tuliowaweka katika biashara.