Wanaume, mke kama huyu unamfanyaje?

that manzi

JF-Expert Member
Jun 19, 2023
351
1,137
NIFANYE NINI MKE WANGU AMETOA MIMBA ZANGU TANO?

Mimi ni kijana wa miaka 33, nimeoa na ndoa yangu ina miaka mitatu sasa. Ndoa yangu ilikua nzuri sana na tangu kuingia kwenye ndoa mimi na mke wangu tulikua tuko vizuri tu. Lakini lilikuja suala la kupata mtoto, kila tulipokua tukihangaika kupata mtoto ilikua ni shida sana, tulishapimwa mahospitalini na kuonekana wote hatuna tatizo.

Kwakua naamini katika Mungu nilikubaliana na ukweli kuwa ni mipango yake hivyo nikaamua kukaa kimya na kusubiri majibu. Wiki iliyopita mke wangu alianza kuumwa, alikua anaumwa sana tumbo, nilitaka kumpeleka hositalini akawa hataki, akaniambia kuna dawa amekunywa atajisikia vizuri.

Lakini hali yake haikua nzuri kabisa, alikua anazidi kuumwa tu, nililazimishia kwenda hospitalini ila aliniambia kuwa yuko sawa na kweli usiku huo alipata usingizi. Wakati akiwa kalala kuna meseji iliingia kwenye simu yake, mimi na mke wangu tunaaminiana, anashika simu yangu na mimi nashika yake.

Ilikua ni meseji ya rafiki yake na alikua anamuuliza kama anaendeleaje, huwa sina kawaida ya kusoma meseji zake kwani namuamini sana, lakini ile niliiona kwa juu na kwakua nilikua najua ni watu wanapendana ni marafiki basi niliona hakuna shida kumjibu kuwa angalau kapata usingizi. Niliifungua ile meseji na katika kujibu niliona meseji za juu yake.

“Yule Daktari hayupo, amefiwa na mke wake kasafiri, usiende Hospitali kwani ukienda kwa daktari mwingine mume wako atajua kuwa umetoa mimba, vumilia shogaa, kunywa hata vidonge vya usingizi asubuhi nitakupeleka mimi.” Meseji ya nyuma ilisema hivyo, mke wangu alijibu “Sawa lakini najihisi hata kufa, natamani kumuambia mume wangu kuwa sitaki mtoto tena.” Mke wangu alimjibu “Ukimuambia hivyo anakuacha mwenzako hana mtoto angalau wewe una wawili…”

Rafiki yake alimjibu hivyo na mke wangu hakujibu tena, meseji za nyuma kabisa zilikua zimefutwa. Kusema kweli nilihisi kuchanganyikiwa, sikutaka kuamini kuwa mke wangu ambaye tumekua tukihangaika mwaka watatu kutafuta mtotoametoa mimba, ilikua haiingii akilini pia kujua kuwa mke wangu ana watoto wawili, niliumia sana lakini sikusema chochote.

Niliscreenshot zile meseji na kujitumia, kisha nikafuta meseji ya rafiki yake ambayo alikua anaulizia hali yake ilia sijue kama nimeziona na sikumjibu tena rafiki yake. Asubuhi nilimuamsha mimi, na kumuambia kuwa nataka twnede hospitalini, aligoma lakini sikukubali, nilimuambia kabisa kuwa siwezi kumuacha afe kisa tu anaogopa kwenda hospitalini. Nilimsimamia akajiandaa nakumpeleka hospitali mimi mwenyewe.

Hakutaka niingie neya kwa Daktari kama kawaida yetu lakini sikujali, nilimpeleka kwa Daktari ambaye nafahamiana naye na nilishamuambia usiku kuwa nahisi kuna kitu kama hicho. Aliingia na kufanyiwa vipimo, kweli alikua katoa mimba na alikua hajasafishwa vizuri. Nilimhudumia mpaka nikahakikisha amepona, sikuongea kitu chochote na wala sikumuuliza kama alikua anaumwa nini, aliniambia tu tumbo lilichafukwa basi nikakubaliana naye.

Nilikaa kimya na kuanza kuchunguza vizuri, haikua shida kwani ndugu zake walikua wanajua kuwa najua ana watoto. Nilimtafuta tu mdogo wake, nikamtopa out na kuanza kuulizia habari za watoto wa dada yake kwani nilikua nahitaji tuwachukue.
“Unajua Dada yako anakua mpweke sana, hajanaimbia kuhusu kuwahcukua watoto ila nahisia naogopa, nataka nimfanyie sapraizi….” Nilimuambia.

Hapo ndipo alifunguka kuwa Dada yake alikua na watoto wawili ambao alizaa na wanaume tofauti na watoto wote wapo kwa Baba zao, hivyo hadhani kama hao wanaume wanaweza kumpa watoto. Aliniambia kuwa Dada yao ndiyo aliwapeleka alipokua chuoo akawatelekeza huko , ila baada ya kupata kazi alitaka kuwachukua Baba zao wakagoma ndiyo maana hakuhangaika nao tena, aliniambia labda niongee na Mama yake anaweza kunisaidia.

Mimi nilimuambia basi asimuambie Mama yake nitajua kitu cha kufanya lakini kusema kweli mpaka sasa hivi nimechanganyikiwa. Bado sijamuambia mke wangu kama najua kwua ana watoto, kibaya zaidi nimechunguza naklugundua kuwa ile mimba haikua ya kwanza, mke wangu alishatoa mimba zangu tano kwakua tu hataki mtoto kwa wkaati huo, nashindwa kuelewa nifanye nini, nachanganyikiwa sijui nimuulize mke wangu au nifanye nini, naomba ushauri wako ndugu.

copy and paste
 
IMG-20240101-WA0647.jpg
 
mkuu...kama hakutaki achana nae usisubiri akuue au umuue...!

yani mtu anamuamini rafiki yake kuliko wewe unae lala nae kitanda kimoja...? swala la kuzaa ni mipango yenu ambayo mnge kaa mkajadili na akakuweka wadhi tu kwa muda huo anadhani hayupo teyari kuzaa.

mngeelewana na mngeishi tu kwa furaha kuliko yeye kutoa mimba zako kwa siri. na nahisi kuna mtu bado anamngoja arudi warudiane...!

mimi bwana nimejiwekea hivi sasa mwanamke yeyote akitaka tuachane aniambie habari za kuoana.

huyo mwanamke inaonyesha ulimuoa kwa shinikizo lake ukadhani umepata kumbe umepatikana.

ndugu yangu hapo hujafika bali Umefikwa...chukua hatua mapema kabla mambo hayaja haribika kabisa.​
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom