blauzi
Member
- Aug 28, 2008
- 24
- 5
Mimi ni mvulana niko masomoni kwa sasa.(Nasoma Degree ya pili) Nina mpenzi wangu tuliyedumu nae kwa miaka 3 sasa. Nimeshamtambulisha nyumbani kwetu, na pia nafahamika kwao japo sijaenda kujitambulisha rasmi. Nikiwa kwenye harakati za kwenda kutoa posa kwao, yeye alipata ajira na hivyo kwenda kazini.Akiwa huko mawasiliano yamekuwa ni mazuri tu na sikupata shida wala wasiwasi juu ya penzi letu. Miezi miwili baada ya kulipoti kazini, alinipigia simu huku akilia na kuogopa kilichotokea,ambacho anadai ni shetani amemtokea. Ana mimba, anayodai shetani alimfanya amkubalie mwanaume mmoja walieshinda nae huko siku ya kuriporti kazini. Msababishaji bado hajapata taarifa za mimba hiyo.Anadai bado ananipenda na ANAOMBA RADHI. Mimi bado sijampa msimamo wangu kuhusu hilo.
Naombeni ushauri wenu wanajamvi, natafakari sana kabla sijatoa maamuzi magumu.
Naombeni ushauri wenu wanajamvi, natafakari sana kabla sijatoa maamuzi magumu.