Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

jarib jiko la umeme wakupandishe tariff iwe ya kiwanda

la hasha tumia Induction Cooker, ya 2000 Watts inaivisha nyama (kilo moja) ndani ya dk 20 tu, iko fasta sana
Mkuu induction cooker hiyo bei gani. Natarajia nijilipue niinunue hata mwakani uko nikiamua kujipikia.
 
Kwa Ufupi.
Unafuu.ni kuwa jiko la multiple 2plate gas ___2plate umeme + Ovena.
faida yake
gesi kunawakati inaisha chakula hakijaiva unahamishia kwenye umeme unmaliza mapishi.

Umeme kuna mda unakuwa low voltage + kukatika au kufanyiwa matengenezo line means... huwezi kupika

Matumizi.
Unit.za umeme kwa Siku maximum
Asubuhi.mchana na Jioni. 3unit= 2500/*30------75000

Ges. Mtungi wa 53k unaweza kutembea nao mpka mwezi na nusu.

NB: gharama huweza kuongezeka kutokana na mtumiaji .
Pia. Nimuhimu kuhakikisha Usalama Unazingatiwa ili kuepuka Ajali za moto.
Gesi ni hatari umeme pia ni hatari .
 
Sasa tule nini mkuu, mbadala wa maharagwe ni nini.
Ujue kule Miami, Frolida USA, wali harage ni very expensive meal..
Tatizo letu sisi wa-TZ tunakula vitu ambavyo vinakaa sana kwenye jiko, mfano maharage au mtu anapika makande hayo ni mavyakula ya ku-discourage kabisa. Yaani maharage ya 2000/- yanatumia engergy ya 5000/-

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unanisema mimi mkuu
Hakun kitu nachukia km mazaga zaga kwenye nyumba! Hahhaa .uwe na kijiko cha nje km mama zetu! Mie jiran aliniambia jenga karo la kuoshea vyombo nje.tena akaniconnetc na fundi kbs..nikamwambia jiko kubwa hivi tena nianze kuchafua uwanja kujenga makaro? Akikuona unapanda maua anakuambia kwann usipande mahind na migomba mwanangu? Maua yansaidia nn sasa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nna mpango wakununua Induction cooker ya blackstone, vipi efficiency yake hasa matumizi ya umeme, je ushawahi kupikia maharagwe, je ulitumia dakika ngapi?
nilibahatika kukamata ya mjerumani around 60k used Zenji, ila uku Dsm naona kuna za Blackstone, zinagonga 100k ivi kwa mpya, 2000W

inapika vizuri mno ufanisi wa 98%,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nilibahatika kukamata ya mjerumani around 60k used Zenji, ila uku Dsm naona kuna za Blackstone, zinagonga 100k ivi kwa mpya, 2000W

inapika vizuri mno ufanisi wa 98%,
Aaah nilidhani inaenda laki nne kumbe hela kidogo hivo. Nataka kuchukua ya 'plate' mbili itanicost ata laki mbili uko. Ghetto langu litakuwaga la nguvu
 
Nunua Majiko yote Ila kwenye matumizi Tumia Gesi na unapohisi Muda wa kujaza mtungi upo vibaya

Hamia kwenye umeme kwa wiki moja au mbili,hela ikishakaa sawa unaenda jaza mtungi wako gesi

maisha yanaendelea kwa kupikia gesi ila sikushauri uwe na Jiko la gesi peke yake wala pia siwezi

kukushauri uwe na Jiko la umeme peke yake,Nina uhakika hata Jiko la mkaa unalo na la kuni pia ikibidi

Kufupisha story unapokua una famlia na upo kwako sio kwenye nyumba za kupanga naongelea kwako

Majiko lazima yawe yote

1.La mkaa
2.La kuni
3.La Gesi
4.La Umeme

Haya majiko yote hapo juu hutakiwi kuyakosa kama kweli wewe una familia ukiwa kama baba/mama

hakikisha maswala ya jikoni umemalizana nayo isitokee sababu ya wewe kutopata chakula hapo home.
Kabisa umenena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi natumia mkaa,umeme,gesi naona matumizi yanakwenda vizuri.familia ya watu 7
 
kwako ni ya kizamani sana yawezekana ipo hivyo

ila kwangu majiko yote yapo kuanzia mkaa,kuni

Ukishakua mfugaji hasa kuku,na hupitishi wiki hujachinja

utaelewa maana ya Jiko la mkaa lina kazi gani.

Huwezi elewa umuhimu wa Jiko la kuni ila ipo siku 1 utaelewa.

Mkaa + kuni wala sio uzamani Chief ni basi tu huna matumizi na haya majiko.
Sijawahi kuelewa na sitakaa elewa.

Mke wangu hawezi shinda jikoni anapuliza kuni au mkaa.

Hata niwe na familia kubwa vipi, kuni na mkaa ni marufuku kwangu.

Wazazi wangu wenyewe hawatumii kuni na mkaa, mi ni nani nitumie?

Kwanza sio mazuri kiafya, yanachelewa kupika. Muda wa kukoleza. Muda utakaokaa kukoleza mkaa, gesi ishamaliza kupika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom