Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

Habari wana JF.

Nimejikuta njia panda, Naomba mwenye kujua anisaidie. Kwa familia ya watu 10, ni lipi jiko sahihi kwa maana ya gharama na matumizi yake kwa ujumla?

Nataka kuchukua moja wapo weekend hii!

Kama hizo Njemba zako 10 zinakula sana Ugali nakushauri nunua la Umeme ila kama wanakula mno Wali nunua la Gesi Mkuu.
 
Acha ubaguzi ungeandika watoto 6 ungekufa???Eti watoto wanne na watoto wa kufikia wawili wote si watoto wanatofauti gani???? Style hiyo uloandika inaonyesha tu unawatenga

Sent using Jamii Forums mobile app
Lengo lake halikuwa kubagua, alishaona akisema watoto 6 kutakuwa na maswali mengi + ushauri humohumo; Akaona afafanue maana tayari huyo aliyeuliza 10? Inaonesha kahamaki.
 
Jiko la umeme nafuu zile zenye plate za induction zile ni energy server. Mimi nina familia ya watu 6 natumia umeme tuu gharama zake kwa mwezi ni 80,000 wakati nikitumia gas mtungi wa 52,000 natumia wiki tatu tuu. Mm naona umeme ni rahisi ukipata jiko ambalo ni energy server.

Sent using Jamii Forums mobile app
80,000 mwezi vs 52,000 wiki tatu.
And u think 80,000 kwa mwezi ni nafuu zaidi, aisee!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wana JF.

Nimejikuta njia panda, Naomba mwenye kujua anisaidie. Kwa familia ya watu 10, ni lipi jiko sahihi kwa maana ya gharama na matumizi yake kwa ujumla?

Nataka kuchukua moja wapo weekend hii!

Jiko la gesi huwa lina gharama ndogo kwa upande wa fedha lakini huwa ni rahisi sana kukugharimu maisha ya watu, na mara nyingi huwa linagharimu maisha ya watu na si ya mtu. Ikitokea mara nyingi lazima liondoke na watu zaidi ya mmoja!
 
Nunua Majiko yote Ila kwenye matumizi Tumia Gesi na unapohisi Muda wa kujaza mtungi upo vibaya

Hamia kwenye umeme kwa wiki moja au mbili,hela ikishakaa sawa unaenda jaza mtungi wako gesi

maisha yanaendelea kwa kupikia gesi ila sikushauri uwe na Jiko la gesi peke yake wala pia siwezi

kukushauri uwe na Jiko la umeme peke yake,Nina uhakika hata Jiko la mkaa unalo na la kuni pia ikibidi

Kufupisha story unapokua una famlia na upo kwako sio kwenye nyumba za kupanga naongelea kwako

Majiko lazima yawe yote

1.La mkaa
2.La kuni
3.La Gesi
4.La Umeme

Haya majiko yote hapo juu hutakiwi kuyakosa kama kweli wewe una familia ukiwa kama baba/mama

hakikisha maswala ya jikoni umemalizana nayo isitokee sababu ya wewe kutopata chakula hapo home.
 
Gesi plate 4 ndo mpango mzima
Iko fasta sana na gharama ni nafuu

umeme nakumbuka tulikua nalo zamani ni ishuuu hizo billi ilibidi kukaa na Tanesco vizuri
Jioni umeme unakua hauna nguvu basi hamuivishii.,sijui cz kila nyumba unakua unatumika.. ss sijui siku hizi labda yako tofauti
 
Back
Top Bottom