Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

Ushauri kati ya jiko la umeme vs gesi

Jiko la umeme nafuu zile zenye plate za induction zile ni energy server. Mimi nina familia ya watu 6 natumia umeme tuu gharama zake kwa mwezi ni 80,000 wakati nikitumia gas mtungi wa 52,000 natumia wiki tatu tuu. Mm naona umeme ni rahisi ukipata jiko ambalo ni energy server.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama kwa mwezi unatumia umeme wa 80k kwa jiko la umeme na Gas unatumia 52k kwa wiki 3 maana yake bado gas ni rahisi kwa mwezi unatumia Kama 67+k tu
 
Nunua Majiko yote Ila kwenye matumizi Tumia Gesi na unapohisi Muda wa kujaza mtungi upo vibaya

Hamia kwenye umeme kwa wiki moja au mbili,hela ikishakaa sawa unaenda jaza mtungi wako gesi

maisha yanaendelea kwa kupikia gesi ila sikushauri uwe na Jiko la gesi peke yake wala pia siwezi

kukushauri uwe na Jiko la umeme peke yake,Nina uhakika hata Jiko la mkaa unalo na la kuni pia ikibidi

Kufupisha story unapokua una famlia na upo kwako sio kwenye nyumba za kupanga naongelea kwako

Majiko lazima yawe yote

1.La mkaa
2.La kuni
3.La Gesi
4.La Umeme

Haya majiko yote hapo juu hutakiwi kuyakosa kama kweli wewe una familia ukiwa kama baba/mama

hakikisha maswala ya jikoni umemalizana nayo isitokee sababu ya wewe kutopata chakula hapo home.
Suala la back up ya gas, nunua mitungi miwili.


Gas ikikata unabadilisha mtungi, baadae au baada ya siku kadhaa unaenda kuuzaja ulioisha.
 
Kama unataka unafuu jipange ununue cooking range ya beko ya kuanzia plate 4 inaweza kua mixed umeme na gas au gas pekee (zipo brand nyingi ila nna uzoufu na beko)

Mtungi wa 15kg unakaa miezi minne na wiki moja kwa matumizi ya kawaida ya familia ya watu wanne, kwa familia yako ya watu 10 unaweza kufikisha miezi miwili.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hii ikoje?
 
INisha wahi mtembela tajiri nmoja mkubwa sana Arusha, kwanza vyakula vyake vinapikiwa kwenye mkaa na kuni, na ni ana pesa si za mawazo mawazo kama. So nakuelewa sana, Majiko ya mkaa na kuni yanatumika sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo tajiri kupikia mkaa na kuni kuna halalisha mkaa na kuni ni bora kuliko umeme na gas?
 
Nyama ya kuchoma kwenye OVEN hata si ielewi kwanza

ukiwa mla nyama sana huwezi chomea nyama kwenye oven

mahotelini yenyewe nyama wanachoma in local ways ndio nyama inatoka Tamu

umeshawahi kula chipsi mayai iliyopikiwa kwenye gesi vs chipsi yai ya mkaa?

Jiko la kuni ni kwa ajili ya Event, Birthdays event zote sherehe sherehe zote tunatumia Kuni

Jiko la mkaa unapikia vitu vinavyochelewa kuiva kama makande,Ngararum,nk nk

Kuna vyakula ili usikie Taste na ujue umekila kweli hicho chakula Pikia Mkaa.
Naongezea tu aina ya moto unaopikia una determine ladha ya chakula.
 
Kwenye gas jumlisha 52000(gas)+15000(umeme)=67000
Gesi kasema 52,000 kwa wiki tatu=siku 21
Umeme kasema 80,000 kwa mwezi =siku 30
Hesabu ya umeme ni 80,000÷30×21=56,000.

Hivyo kwa wiki tatu pamoja na matumizi yake mengine, umeme atatumia 56,000.

Hiyo 67000 umeitolea wapi!? Kwa hesabu hii bado kwake umeme ni nafuu zaidi.
 
Back
Top Bottom