Ushauri juu ya marumaru (tiles )

Ushauri juu ya marumaru (tiles )

Nahifadhi hu uzi naomba na mimi nikumbushwe Mwezi wa tisa please
 
Mkuu ulipotaja Monalisa kuna kitu umenikumbusha. Hivi hawa jamaa wako katika kundi gani? Ni wafanyabiashara wa kawaida au ni wawekezaji? Je wawekezaji wanapashwa kuweka hesabu sahihi za transaction zao? Nauliza hivyo kwa kuwa nilielekezwa kwenda hapo Monalisa na jamaa yangu kwenda kununua board fulani kwa ajili ya ujenzi. Tulikubaliana bei na nililipa pale. Walinipa kikaratasi kimeandikwa kwa lugha ya kichina na kunielekeza kwenda Chang'ombe kwenye godown lao kupakia mzigo. Nilipofika Godown, niliwaonyesha hicho kikaratasi na wao walinipa huo mzigo. Delivery note waliyoniandikia pale godown, ilionyesha kwamba nimenunua huo mzigo katika duka fulani la hardware kariakoo. Pesa nilizolipa karibu 15M sikupewa receipt wala nini.

Kwa mtindo huu hawa jamaa si wanakwepa ushuru? Hata VAT hawalipi kwani malipo yangu hayakuwa na receipt.

Je kuna mwingine hapa JF aliyewahi kukutana na ujanja wa hawa wachina?

Tiba
Hukustahili kuchukua mzigo pasipo kuwa na risiti halali yenye kuonyesha TRA wamepata chao, otherwise nawe ulikwepa kodi au uliwafaidisha wao.
 
Nenda Hugo Tiles wapo Nyerere Road ilipokuwa ofisi ya exide those days. Next to Tansoma Hotel. Hapa nimewahi nunua tiles kwajili ya ujenzi wa kibanda cha wazazi kijijini, so far niko happy na tiles zao. Kwanza ubora ni mzuri, gharama ni ya kati, hazitelezi kama za kina huhaaaaaaaaaaaaaaaaa

Hawa nimeambiwa wanauza za Kiitaliano, ngoja nikawaone.
 
Hii topic nimeipenda sana. Binafsi nigependa kupata ushauri wa kubaki na terazo ama kuweka tiles, kipi ni afadhali, aesthetically zaidi. Naambiwa terazo ni ya zamani ila ni ya milele, je tiles?
 
Hii topic nimeipenda sana. Binafsi nigependa kupata ushauri wa kubaki na terazo ama kuweka tiles, kipi ni afadhali, aesthetically zaidi. Naambiwa terazo ni ya zamani ila ni ya milele, je tiles?

Mkuu mambo yote kwa sasa ni tiles. Hakikisha tu unanunua zenye ubora na si zile feki za mchina (ila ziko za ubora mzuri kabisa za wachina pia)
 
Wakuu tiles za Spain naa Italia bei haikamatiki, lol! Naanza kushawishika kwenda kwa za kichina sasa
 
Mkuu bei ikoje kwa hizi za Uarabuni kwa square metre e.g za ukubwa wa 40x40 cm au 45x45cm?

25,000 unapata vizuri sana. Ongea na Seif 0713296353 ni supplier, wana goddown Chang'ombe, yeye ndio yuko hapo, unaweza kwenda kukagua kama uko Dar.
 
kaka nashukuru aisee nilijua ntakuwa nimeshafikia stegi ya kuweka tiles ndo kwanza nahangaika na issue ya mbao za kazi sana ila soon ntafika.

Hakuna shaka ndugu yangu. Ujenzi ukishaanza tu lazima itafikia siku watu wanahamia, its just a question of time. Hongera sana na kila la heri...
 
Marejesho, Angalia usichukue zenye maua, chukua plain kwani zenye Nakshi sometimes zinapauka na maua yanapoteza mvuto wake.

Nyati hebu tupe taarifa ya maamuzi yako ulinunua wapi (duka gani)? Za size gani? Aina gani (ceramic, porcelain, granite9? Na kwa bei gani kwa square metre?
 
Wakuu hebu niambieni kwa mwenye uzoefu na tiles za South Africa. Nimekutana nazo kwa bei nzuri jijini DAR.
 
Back
Top Bottom