Ushauri juu ya kazi ya Ualimu na Uaskari wapi penye unafuu

Mtoa Mada Tuambie Maamuzi Yako, Maana Ushauri Umetolewa Sana Hapa!
 
Kiongozi nakushauri usiache Ualimu. Kazi yeyote ile ya Uaskari...either Police au Jeshi(JWTZ) sio kazi ndugu yangu. Hao unao waona askari nao wanatamani watoke huku but wanashindwa coz they do not have other options za ajira .....nikiwa na maana hawana elimu ya kutosha (professional) au hata kama wanazo basi wamechelewa kufanya maamuzi magumu ya kutoka huko and they are late now to make hard decision hivyo wanaendelea kuwa watumwa huko jeshini/police.

MFANO:

Mimi nilijiunga na jeshi mwaka 2001 by then nikiwa form 6 leaver, kutokana na elimu yangu na uelewa wangu nilikuwa naumia sana kuona askari ....koplo au sajenti akiwa na mbavu za mbwa kutuburuza atakavyo na kutaka waheshimiwe as miungu kisa cheo.

Mwaka 2002 nika-join UDSM nikiwa bado askari nikasomea B.Ed na 2006 nilipomaliza nikapiga chini faster jeshi. Ukiwa uraiani unafaidi sana maisha na unakuwa huru. Jeshini amri za kufa mtu, kulinda guard, kufagia fagia kama mtoto wa primary na we hali ukiwa home unajidai baba wa familia...hahaha...acha hiyo makitu bana.

Leo hii am so happy na maisha ya Ualimu na nikikutana na askari wenzangu wananipongeza kwa maamuzi magumu niliyoyafanya na wananionea wivu sana.

USHAURI WA MWISHO:


1. Leo hii kama una degree ina maana utakuja kustaafu ukiwa na daraja H la mshahara! na kama ingekuwa leo hii unastaafu ualimu basi ungepata mafao yako kama Milioni 120 plus, je ni askari gani awe wa JWT au police ambae hana cheo kikubwa .....askari wa kawaida anaweza lipwa hiyo pesa???

2. Ualimu unakuwa free sana na mambo yako...fungua miradi ..ufugaji au biashara itakuongezea kipato kizuri sana but kazi ya uaskari ni utumwa.


NB: Mtoto wangu kamwe hata akose kazi lakini hawezi kufanya kazi ya utumwa ya Police au jeshi....NEVER!

Ndugu ulikuwa kambi ipi?Makutu au Ruvu?inaonekana Makoplo walikulima mitama na makofi sana.Lakini unaonekana una majivuno sana,by then form 6 ulidhani una elimu kuliko askari yeyote.
Kwenye blue unasema ukikutana na askari wenzako?wewe ni askari?ulikula kiapo cha uaskari au ulitoroka depo?Mura kazi ya jeshi kugangamala,ushauri wako sio!askari ndio anakulinda wewe na Taifa kwa ujumla.
 
Mtoa Mada Tuambie Maamuzi Yako, Maana Ushauri Umetolewa Sana Hapa!

mkuu Majigo,
kusema ukweli bado nnko njia panda,
kuna br wangu yy ni askari ambaye ni veiko inspector wa wilaya,
ndiye anaweza nisaidia kuingia huko na kuna jamaa alishawasaidia hadi kuwapa kofia nyeupe lakin ananiambia huko ni pabovu naweza kupigishwa lindo hadi miaka 3 ndo upate unafuu,
jambo ambalo naona bora kwenda masters mwaka huu ili nifanye kitu kingine ingawa mpango wa kusoma sikuwa nao,
 
Nadhani umeelewa

mkuu ABEDNEGO CHARLES,kiasi fulani ninaweza kuamua sasa,ila kiukweli ualimu ni kada ya chini kuliko kada zote kimaslahi,
na mwaka 1994,ndugu Edward G,Lowasa akizungumza na wanachuo chuo cha ualimu kigurunyembe alisema ''if you are here serching for the green pasture your in the wrong way''
 
wewee nenda jeshini wewee, angalia posho 300,000/, salary 500,000/= ,jumla 700,000 HAYO MAPATO NI KWA ASIYE NA CHEO AMBAYE HANA SHAHADA, MWALIMU WA DEGREE 534,000/=, toa kodi,cwt na makato ya heslb, inabak 390,000/=,
 
wewee nenda jeshini wewee, angalia posho 300,000/, salary 500,000/= ,jumla 700,000 HAYO MAPATO NI KWA ASIYE NA CHEO AMBAYE HANA SHAHADA, MWALIMU WA DEGREE 534,000/=, toa kodi,cwt na makato ya heslb, inabak 390,000/=,
jeshi jkt miaka 2,huku huna uhakika wa kazi,then miezi 6 monduli,
 
mshahara wa cheti na degree yako? Bora utafute private unapiga laki 8-9 na mazingira mazuri ya kazi after 5 yrz utakuwa mbali xna bt usisahau kupiga biashara au kilimo na ufugaji! Bt kama afya nzuri pia ukitimba polisi au jeshi unapiga ela zaidi
private! ajira mikononi mwa wanafunzi wakikugomea tu umefunga mabegi
!!!
 
Mkuu njoo haraka sana Polisi bonge la Dili! Njoo tukutumie kusafisha njia ya kuendelea kubaki Magogoni,
Njoo fasta make bado kuna akina Mwangosi wanatusumbua! ikishindikana basi tutakufanya TIGO uhangaike na waendesha Bodaboda! siyo utani baada ya muda utaenjoy sana, make yale mabao ya miatanomiatano za makonda wajeuri utazikusanya sana! njoo basi uwe fagio letu,! hachana na rushwa za katikati ya miguu, manake TAMWA na TGNP mhh! Huku hawapo, na hata PCCB tunakula nao saani moja!
Unasita nini Mkuu wahi haraka, ila ikibidi tuna KuBarlow fasta unafanya mchezo!

Mimi ni mwalimu mwenye shahada ya elimu baada ya kujiendeleza toka ualimu ngazi ya cheti,miaka 7 kazini,
baada ya kuona mambo hayaendi kabisa hapa kwenye ualimu kuna ndugu yangu kanishauri nihamie kwenye jeshi la polisi (uaskari), kwani maisha ni magumu na pamoja na kujiendeleza kielimu hakuna badiliko lolote nnlilolipata hadi sasa kuanzia mshahara uko palepale tu,
zaidi ya kupelekwa kibabe sekondari ya jirani na shule yangu ya awali bila hata kupewa stahili zangu za uhamisho,
naomba ushauri wa dhati kuhusu wapi penye unafuu,
 
E-bwana sikiliza Elimu uliyonayo inatosha sana kilichobaki ,angalia sehemu yenye kipato,usiogope ugumu wa kazi,angalia ANKARA.NAKUSHAURI UKIPATA JESHI WE NENDA,UALIMU MSHAHARA KIDOGO,BADO KUBURUZWA PALE PALE,UNATUPWA PORI,KUFUATA MSHAHARA MJINI UNATUMIA ROBO YA MSHAHARA WAKO,UALIMU MWANANGU SIO INSHU,MAAFISA ELIMU WENYEWE AMBAO MNALINGANA ELIMU,MACHOKO TU,WANABANA HAKI YA MNYONGE,MVUJA JASHO,PIGA UALIMU CHINI MZEE,"NI BORA NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI"
 
E-bwana sikiliza Elimu uliyonayo inatosha sana kilichobaki ,angalia sehemu yenye kipato,usiogope ugumu wa kazi,angalia ANKARA.NAKUSHAURI UKIPATA JESHI WE NENDA,UALIMU MSHAHARA KIDOGO,BADO KUBURUZWA PALE PALE,UNATUPWA PORI,KUFUATA MSHAHARA MJINI UNATUMIA ROBO YA MSHAHARA WAKO,UALIMU MWANANGU SIO INSHU,MAAFISA ELIMU WENYEWE AMBAO MNALINGANA ELIMU,MACHOKO TU,WANABANA HAKI YA MNYONGE,MVUJA JASHO,PIGA UALIMU CHINI MZEE,"NI BORA NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI"

ahsante kwa ushauri mkuu Charles,
ni ushauri makini sana na wenye uhalisia,
ila kiukweli idara ya ualimu sio kabisa ,iko nyuma sana,
nna miaka nane kazin lkn nna kiwanja tu cha laki 1.5
 
kazi ya ualimu ni nafuu na inampa mtu mda wa kufanya shughuli nyingine za kiuchumi pale anapo kuwa amemaliza mda wa kaz kwa maoni yangu, vilevile inampatia mhusika wakati mzuri wa kuwa karibu na familia kutokana anapata mda mwingi anapotoka kazini
 
ahsante sana mkuu,
umefunguka kwa uzoefu kitu ambacho kinanisaidia kupata picha halisi ya jeshi la polisi ilivyo,

Mkuu, sio kwa unazi wala mkumbo, kat ya hivo viwili ni bora uende polisi, nitafafanua:
1. Mishahara ya graduate wa polisi ni mikubwa kuliko ile ya graduate wa ualimu.
2. Ration ama posho kila katkat ya mwezi isiyopungua 150,000/=
3. Posho ya pango 18% ya Basic salary.
4. Graduate wa polisi anaingia lindo ktk mmuda usiozidi mwezi baada ya kupangiwa mkoa ama kituo cha kazi ili ajue nini kinafanyka upande huo kama sehemu ya kazi police lakn baada ya hapo ni kazi za office zaidi ndani ya jeshi kwani kuna vitengo vingi sn kule siku hizi vinahtaj proffessinals.
5. Suala la nyumba ni uamuzi wa mtu, ndio maana hata mtaani tunaishi nao hawa polisi lakini ukipenda vya bure viduara hutavikwepa though sahv nyumba nyng znajengwa kwa maofisa.

My take: Jiunge na polisi kwani pia kuna marupurupu zaidi yatokanayo na safari, ugeni, usimamizi ktk Nectas, nk
 
nashauri uende JWTZ na si upolisi ila kama unataka laana na kurogwa mapema nenda upolisi ndugu yangu utapoteza uelekeo ukiwa na elimu yako ila kama ni failure upolisi ni sehemu ya kutokea nadhan kuna nguvu ya mvutano kati ya usomi na uupolisi mengi utaayasikia ngoja wadau waje
 
Daah,hii kweli changamoto.Maana walio kule wanataka kuja huku na tulio huku tunataka kwenda kule. Ukweli wengi wameusema hapo juu,anzisha mradi ndugu,utaupenda ualimu,maana utakua free na mambo yako,hakuna kuitwa kazini kwa dharura wala nini! Hao askari raha yake ipo,ila uhuru wa kufanya mengine ni mdogo sana.Pia nina shahada,niliomba ujeshi,ila niliubwaga pindi jina langu na ya wengine yalipotoka kwaajili ya intavyuu,nilipima sana kuhusu kuuza uhuru wangu. Ila,fanya utafiti wa kutosha na ufanye maamuzi baada ya hapo. KILA LA HERI!
 
Bakia ualimu,askari ckazi nzuri,ckuhizi ualimu tofauti na zamani kwanza ukitaka kujua kama unafaa wale waliosomea degree nyingine kwa kufuata sifa wengi wameomba kazi ya ualimu wizarani kwa kuwa wamesota mtaani mpaka wanazeeka.Mimi nimechukua B .Aed nasubiri ajira january hii na nina mipango mingi kuhusu biashara au kilimo na c kutegemea mshahara.
 
kama huyo ndugu yako anania ya kukusaidia amwambie akulipie ada uongeze elimu kama anaona Degree ya Ualimu huipendi? somea fani nyingine kama sio kilaza eg. CDTI, WANYAMAPORI MWEKA, MISITU SUA, UDAKTARI MIFUGO NA KILIMO, UHASIBU IFM, BIASHARA CBE N.K, Asitamanie Wizi wanaofanya Matrafki wengi wanaishiaga pabaya wanakufa kinoma. Kama ulikua kilaza nenda upolisi ila ujue hakunaga CWT kugoma wala kuandamana ni kupenda nch kwa dhati hata kama unatetea fisadi, na kusema ndio afande hadi unachanganyikiwa ndo kama ada, serikali si jinga kuwapa reshen, Eg uko na wife bed 9t, mara simu, Aroo haraka sana dk 5 NMB Imevamiwa njöo ukiwa full over. Walimu wanapiga laki tano ya kuanzia take home, hela ya kujikimu 75*14, pia marupurupu yapo eg, ela za kuboresha elimu, tuitions, semina, necta, madenti wanakuheshimu unaombwa badala ya kulazimishwa, kama ni kiongozi ndo usiseme mafungu yanatumwa ya kufamtu eg kapitation, chakula cha mchana, chai ni juu ya shule, unajisomea, unaweza kufanya mibiashara yako na kilimo poa tuu, kila dei uko home na wife wako, tena kama na yeye ni ticha fuso ni fasta mna zimiliki, so mimi ni mchagaa kazi sichagui kama napiga laki 7~8 kwa mwezi + mke wangu laki 8= 1.6 @ month after 5 yrs ntakuwa na miliki pesa na mali yenye thamani ya zaidi ya mil. 200
 
kazi ya ualimu ni nafuu na inampa mtu mda wa kufanya shughuli nyingine za kiuchumi pale anapo kuwa amemaliza mda wa kaz kwa maoni yangu, vilevile inampatia mhusika wakati mzuri wa kuwa karibu na familia kutokana anapata mda mwingi anapotoka kazini

Upo sahihi mkuu,lakini kwa asiyejua ni ngumu sana kum-convice akubali huo ukweli.

Mfano: Mfano mimi niliamua kuacha kazi ya ualimu baada ya kuifanya kwa muda wa miaka 7, nilipata kazi niliyoona inalipa baada ya kupewa ofa ya Tsh.1.5 milion kwenye makaratasi before makato .......mungu wangu...yaliyonikuta ni balaaa tupu ndugu yangu:-
1. Baada ya makato nikawa nabakia na 1 M, nyumba ya vyumba 2,sebule+jiko Tsh. laki 2, Chai + breakfast kazini 120,000 kwa mwezi (hapo achana na bajeti ya home - familia).

2. In comparison nilitamani kazi yangu ya ualimu na nimerudi kwenye kazi yangu ya ualimu "believe or not" but habari ndio hiyo mkuu. Sababu ni kuwa difference ya take home ni laki 3 tu na tena hiyo hela ina-nicost kulipia nyumba na chakula kazini WAKATI tayari nikiwa mwalimu nimejenga nyumba yangu nzuri na najinafasi na familia yangu....huku viposho vya NECTA havikosekani na vinginevyo.....WHILE kule kwenye 1.5 Mil hakuna posho wala night...!

NB: Ukiwa mwalimu una bachelor ukijijenga na ukafanikiwa kustaafu hutakosa kufikia daraja H kama mwalimu wa secondary ambapo hutakosa Millioni 160 kama unastaafu leo hii, au kufikia daraja I kama mkufunzi wa vyuo vya ualimu ambapo kama unastaafu leo huwezi kosa million 200 plus.

Nakushauri tena fikiria mara mbili.......mvumilivu hula mbivu....hata huko jeshini kuna ranks....private, lans coplo, koplo, sajent, staff sajent n.k, the same applied to ualimu au kada nyingine yeyote ile.....wewe mwalimu umesoma kwa kujiendeleza sasa kwanini usiwe na subira?

Japo unasema ualimu mbaya lakini tambua leo hii kuna walimu wanapokea salary 1.8 Mill wengine 2.2 Mill and plus, it is just a matter of time bro!

Cc:gfsonwin......./ mwalimu mwenzangu.
 
Back
Top Bottom