Captain Lelionka
Member
- Oct 26, 2010
- 52
- 29
Ushauri Jamani,
Mke wangu ni mlalamishi sana pia ana wivu uliopindukia.Tulikuwa tukifanya kazi ofisi moja kwa kweli nilikuwa nikipata shida sana yaani nikicheka na msichana yeyote ofisini basi ni kwamba nampenda. Bahati nzuri nikahamishwa kikazi tena nimehama Mkoa kabisa lakini toka nilipohama amekuwa ana lawama za ajabu.
Yaani kila siku ofisini anaonewa yeye kila mtu anamnyanyasa yeye mpaka nakosa amani ukijaribu kufuatilia kiundani unagundua yeye ndio mkorofi. Jambo ni maswala ya urembo wake analalamika eti simpi hela ya saloon mara simnunulii nguo. Nikijaribu kumuuliza hivi wewe katika mshahara unaopata kwanini usitenge hela ya saloon inakua ni ugomvi ndani ukimpa hela kama laki mbili kwamba zitunze basi anaona kesha kuwa kama tajiri.
Ndani ya siku mbili ukiuliza anakwambia katumia elfu hamsini ukiuliza zimefanya nini unaonekana unamnyanyasa kisa anatoka familia ya kimaskini. Napata taabu jinsi ya kuishi na huyu mwanamke. Nimezaa nae mtoto mmoja lakini hatujafunga ndoa. Hawapendi rafiki zangu ilishatokea siku akamsingizia rafiki yangu kuwa amemtongoza.
Ushauri jamani nakosa raha kabisa
Mke wangu ni mlalamishi sana pia ana wivu uliopindukia.Tulikuwa tukifanya kazi ofisi moja kwa kweli nilikuwa nikipata shida sana yaani nikicheka na msichana yeyote ofisini basi ni kwamba nampenda. Bahati nzuri nikahamishwa kikazi tena nimehama Mkoa kabisa lakini toka nilipohama amekuwa ana lawama za ajabu.
Yaani kila siku ofisini anaonewa yeye kila mtu anamnyanyasa yeye mpaka nakosa amani ukijaribu kufuatilia kiundani unagundua yeye ndio mkorofi. Jambo ni maswala ya urembo wake analalamika eti simpi hela ya saloon mara simnunulii nguo. Nikijaribu kumuuliza hivi wewe katika mshahara unaopata kwanini usitenge hela ya saloon inakua ni ugomvi ndani ukimpa hela kama laki mbili kwamba zitunze basi anaona kesha kuwa kama tajiri.
Ndani ya siku mbili ukiuliza anakwambia katumia elfu hamsini ukiuliza zimefanya nini unaonekana unamnyanyasa kisa anatoka familia ya kimaskini. Napata taabu jinsi ya kuishi na huyu mwanamke. Nimezaa nae mtoto mmoja lakini hatujafunga ndoa. Hawapendi rafiki zangu ilishatokea siku akamsingizia rafiki yangu kuwa amemtongoza.
Ushauri jamani nakosa raha kabisa