TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,914
- 23,077
BARIDI YA MOROGORO HAINA ADABU
1. Ya moyoni ninayo, mengi kujaza kapu
Yaani tena yahusuyo, baridi iumizayo pafu
Baridi adabu hamnayo, nawapa yake makavu
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
2. Mimi sasa nipo, Uluguru kwa pembeni
Haihitaji hata malipo, milima hii angalieni
Kipupwe hasa kijapo, hakukaliki hasa milimani
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
3. Baridi mwaka huu, imefika kwetu pembeni
Tupia jinsi juu, haijari atupia nani
Yapenye hata fuvu, mzungu kapitia dirishani
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
4. Mshono yangu sweta, juzi kati nkatupia
Nkatokeza hasa matata, wadhani ninao rupia
Asubuhi baridi kanikamata, sweta yangu kashambulia
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
5. Baridi hii haijafunzwa, hasa huko itokako
Wakubwa wadogo wakunjwa, mpaka waone mchoko
Baridi haijui mgonjwa, wote ni viboko
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
6. Wanywa chai mwawindwa, baridi iko mafichoni
Wanywa supu hamjapitwa, baridi hii kutibueni
Midomo yenu kuunguzwa, na mchemsho asubuhini
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
7. Jana nikajitupa gurioni, baridi dawa mtafutia
Nikajipanga hata mfukoni, muuza dawa asijenkatalia
Kwa mapatano makini, mkoti sufi nkajitwalia
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
8. Dawa nyingine nimepata, kufanya kazi kinguvu
Shamba mboga nimepata, baridi timua kimabavu
Kulima dawa matata, baridi haileti uvivu
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
9. Mazao mboga nikipata, pesa mshibo uhakika
Reli kasi tutapata, haraka sokoni kufika
Bombadia nayo kupita, Kihonda kubeba karotika
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
10.Baridi ishikishwe adabu, sisi tufanyapo kazi
Rais kafuta sababu, sisi kutofanya kazi
Baridi siyo sababu, kaweka furusa wazi
Baridi ya Morogoro, sasa imefunzwa adabu.
===
Mtunzi TUJITEGEMEE wa JF.
-----
Ushairi wangu wa kwanza wenye beti kumi kuwahi kuutunga na kuuandika ndani ya masaa manne. Naomba Maksi juu ya uwezo wangu wa kiswahili na utunzi. Pia unipapo maksi naomba unipe na mapungufu yangu endapo sitapata maksi zako za 100 kwa 100.
Karibuni.
1. Ya moyoni ninayo, mengi kujaza kapu
Yaani tena yahusuyo, baridi iumizayo pafu
Baridi adabu hamnayo, nawapa yake makavu
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
2. Mimi sasa nipo, Uluguru kwa pembeni
Haihitaji hata malipo, milima hii angalieni
Kipupwe hasa kijapo, hakukaliki hasa milimani
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
3. Baridi mwaka huu, imefika kwetu pembeni
Tupia jinsi juu, haijari atupia nani
Yapenye hata fuvu, mzungu kapitia dirishani
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
4. Mshono yangu sweta, juzi kati nkatupia
Nkatokeza hasa matata, wadhani ninao rupia
Asubuhi baridi kanikamata, sweta yangu kashambulia
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
5. Baridi hii haijafunzwa, hasa huko itokako
Wakubwa wadogo wakunjwa, mpaka waone mchoko
Baridi haijui mgonjwa, wote ni viboko
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
6. Wanywa chai mwawindwa, baridi iko mafichoni
Wanywa supu hamjapitwa, baridi hii kutibueni
Midomo yenu kuunguzwa, na mchemsho asubuhini
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
7. Jana nikajitupa gurioni, baridi dawa mtafutia
Nikajipanga hata mfukoni, muuza dawa asijenkatalia
Kwa mapatano makini, mkoti sufi nkajitwalia
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
8. Dawa nyingine nimepata, kufanya kazi kinguvu
Shamba mboga nimepata, baridi timua kimabavu
Kulima dawa matata, baridi haileti uvivu
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
9. Mazao mboga nikipata, pesa mshibo uhakika
Reli kasi tutapata, haraka sokoni kufika
Bombadia nayo kupita, Kihonda kubeba karotika
Baridi ya Morogoro, kweli haina adabu.
10.Baridi ishikishwe adabu, sisi tufanyapo kazi
Rais kafuta sababu, sisi kutofanya kazi
Baridi siyo sababu, kaweka furusa wazi
Baridi ya Morogoro, sasa imefunzwa adabu.
===
Mtunzi TUJITEGEMEE wa JF.
-----
Ushairi wangu wa kwanza wenye beti kumi kuwahi kuutunga na kuuandika ndani ya masaa manne. Naomba Maksi juu ya uwezo wangu wa kiswahili na utunzi. Pia unipapo maksi naomba unipe na mapungufu yangu endapo sitapata maksi zako za 100 kwa 100.
Karibuni.
Last edited: