Salaam Wanajukwaa,
Kumekuwa na kelele nyingi sana juu ya Tanzania 'Wonderkid' Walid/Clement Mzize hasa juu ya Thamani yake ambapo kwa mujibu wa Maelezo ya Klabu yake na mashabiki wa Young African SC ni kuwa Thamani ya Mzize ni zaidi ya US dollar Milioni Moja ($1,000,000).
Hapo hapo kutokana na maelezo ya Manager wake anasema Mzize alikuwa analipwa Mil 2 na baada ya kupambana sana na Klabu ya Yanga ndipo akawa analipwa Milioni 15.
Mambo ni mengi, ila haya mambo ya mishahara mara nyingi ni siri, sasa tusije kufikia huko mpaka tukaanza kujua ya sirini kama yale ya Feisal kulishwa Ugali🙂. Ili Yanga waseme kuwa Mzize thamani yake ni kubwa kama ambavyo wanasema, basi wamuongezee tu Mshahara angalau kufikia Milioni 30.
Maisha ya Mpira ni Mafupi sana, Mzize asije kusemwa kama akina Ajibu na wengine ambao walipata offer kadhaa huko nje wakazipiga chini na ukizingatia ndio kwanza ana 'MIAKA 20'.
NB: Wakati Yanga wanapandisha thamani ya Mzize kufikia $1,000,000, waangalie pia namna ya hiyo negotiation yao suala la Maslahi binafsi ya Mchezaji. Anaweza kuuzwa Dola milioni Moja halafu akawa anaenda kulipwa Mil 25/mwezi. wakati akiwa Yanga akilipwa milion 15, anaweza kupata zawadi kutoka kwa wadau wa Yanga ikafika mpaka mil 3-5 kwa mwezi.
Kumekuwa na kelele nyingi sana juu ya Tanzania 'Wonderkid' Walid/Clement Mzize hasa juu ya Thamani yake ambapo kwa mujibu wa Maelezo ya Klabu yake na mashabiki wa Young African SC ni kuwa Thamani ya Mzize ni zaidi ya US dollar Milioni Moja ($1,000,000).
Hapo hapo kutokana na maelezo ya Manager wake anasema Mzize alikuwa analipwa Mil 2 na baada ya kupambana sana na Klabu ya Yanga ndipo akawa analipwa Milioni 15.
Mambo ni mengi, ila haya mambo ya mishahara mara nyingi ni siri, sasa tusije kufikia huko mpaka tukaanza kujua ya sirini kama yale ya Feisal kulishwa Ugali🙂. Ili Yanga waseme kuwa Mzize thamani yake ni kubwa kama ambavyo wanasema, basi wamuongezee tu Mshahara angalau kufikia Milioni 30.
Maisha ya Mpira ni Mafupi sana, Mzize asije kusemwa kama akina Ajibu na wengine ambao walipata offer kadhaa huko nje wakazipiga chini na ukizingatia ndio kwanza ana 'MIAKA 20'.
NB: Wakati Yanga wanapandisha thamani ya Mzize kufikia $1,000,000, waangalie pia namna ya hiyo negotiation yao suala la Maslahi binafsi ya Mchezaji. Anaweza kuuzwa Dola milioni Moja halafu akawa anaenda kulipwa Mil 25/mwezi. wakati akiwa Yanga akilipwa milion 15, anaweza kupata zawadi kutoka kwa wadau wa Yanga ikafika mpaka mil 3-5 kwa mwezi.