Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,276
Mtangazaji wa Marekani Ellen Degeneres 'alimbagua' bingwa wa olimpiki katika mbio za mita 100, Usain Bolt, kwa misingi ya rangi.
Hii ni baada ya mtangazaji huyo wa runinga ya marekani, kuweka picha akiwa amemdandia Usain Bolt na kuandika kwenye Twitter kwamba ameshapata mbinu mpya ya kuwashinda wapinzani wake.
Mashabiki wa Bolt wamelaani picha hiyo wakisema ni kumnyanyasa Bolt na kumfananisha na farasi ama punda.
Ellen Degeneres, amejibu shutma za mashabiki wa bingwa wa mbio za mita 100 Olimpiki Usain Bolt kuwa yeye si mbaguzi wa rangi.
Ellen anayetambuliwa kwa machachari yake, amesema mashabiki wa Bolt wameielewa vibaya picha hiyo na kujitetea yeye si mbaguzi wa rangi na anapinga kitendo hicho.