Usafiri wa umma ukipatikana mtupe taarifa

Usafiri wa umma ukipatikana mtupe taarifa

Chance ndoto

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2017
Posts
4,618
Reaction score
10,789
Katika hali isiyokawaida, jana baada ya kumuona Simbachawene akiongea, sikutegemea usiku wa kuamkia leo ningerudi kwa taabu nyumbani. Nimefika Buguruni nikakuta watu wanakimbizwa na wanajeshi, wanawaambia wasitembee.

Ilipofika saa saba usiku, mambo yalikuwa hivyo.

Leo asubuhi natoka barabarani niende ofisini kwa kuwa nina sababu ya kutoka. Hakuna usafiri; bodaboda ni gharama na nazo zinapita moja moja sana. Sikutegemea kutakuwapo na kafyu.

Kweli maandamano yanatikisa nchi.

Usafiri wa umma ukipatikana mnipeni taarifa.
 
Kesho utamsiki shekhe anasema anaipongeza serikali kwa kudumisha amani.

Hii ndo tafsiri ya Amani? Matatizo ya kusolve kwa Table unataka tumia Gun, Lazima utawale kwa shida TU
 
Sasa hivi Kutembea barabarani kwenye hii sikukuu ya Uhuru ni sawa tu na uhaini🐼
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom