Usafi waanza kufanyika Soko la Kawe baada ya uchafu kukithiri kutokana na mvua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Kawe (1).jpg

Kawe (3).jpg
Baada ya Jamii Forums kuripoti kuhusu Soko la Kawe kuwa chafu kutokana na mvua zilizonyesha hivi karibuni Jijini Dar es Salaam, mamlaka zimeanza kuchukua hatua ya kufanya usafi sokoni hapo.

Barabara ya kuelekea sokoni hapo imeanza kufanyiwa marekebisho ya kuwekewa vifusi, ambapo awali kulikuwa na matope mengi, mazingira yaliyokuwa na taka nyingi nayo yamefanyiwa usafi.

Soko hilo lipo katika Jimbo la Kawe ambalo Mbunge wake ni Joseph Gwajima.


Pia soma > Dar es Salaam: Hali ya mazingira Soko la Kawe siyo nzuri kwa afya za watumiaji na wakazi
 
Back
Top Bottom