Nyamayao
JF-Expert Member
- Jan 22, 2009
- 6,966
- 2,352
Nyamayao ukiwa na tatizo hasa ugonjwa kama umekusumbua kwa muda mrefu na umetumia dawa zinazotakiwa na huponi hakika utakachoambiwa utumia ili upone utatumia.
Mie nilivyoambiwa na yule Dr niliacha kujisafi kwa ndani siingizi kidole/maji kwa ajili ya kujisafisha, alinipa dawa nikatumia na tokea wakati ule sijasumbuliwa tebna na fungus
Niliulizwa kwa nini unasafisha kule?? nikamwambia Dr najisafi kwa sababu kuna uchafu kule, nikaulizwa huwa unatoka wapi?? huo uchafu unasababishwa na nini??, na Dr akaniambia niache mara moja kufanya ivyo kwa kuwa hata maji tunayotumia kujisafi kule ni ya bombani (dawasco) kwa wale walioko bongo, sio masafi kivile, akaniambia labda nikitaka kufanya ivyo nitumia product za oriframe wanazo kwa ajili ya ujisafi kule, na akanitajia na nyingine( sikumbuki jina), Ila mie binafsi nikaona isiwe tabu, nilipokuwa kigoli , shuleni, chuo mbona nilikuwa sisafishi? na sikuwahi kupata haya matatizo? nikatupa mbali habari ya kusafisha kule, na nipo poa tu.
Dr aliniambia kule panajisafisha penyewe.vingi tunaponzwa na huu utandawazi.
ndio mana nikakuuliza maji uliyokuwa una2mia ni salama?.....nadhani hizo fungus ziliababishwa na maji hata mie nilipokuwa dar nilipata fungus coz ya maji nilijitibu na kuanza ku2mia maji salama huko na tatizo likaisha mpaka leo, hiyo red Ikunda jamani jamani jamani....speechless kwa kweli...yaani hapana aisee, kama usafi nao ni utandawazi tena bac kasheshe 2pu......