Us Green Card Lottery

Nawajua family friends ambao walipata na familia nzima wakahamia. Baba akasoma PhD ya Economics, mama Pharmacy. Wana watoto sita na wote wamesoma vizuri - engineers, MDs na kabinti kao ka mwisho kanasoma Robotics na Artificial intelligence/Renewable Energy/Environmental Engineering Cambridge UK.

Ukipata hii kitu ukifika tu fanya kila uwezalo usome hata kama ni kwenda kumwangukia Bill Gates miguuni. Uzuri pia karibu vyuo vyote vina program za kusomesha watoto masikini na wewe ukisema kuwa u mgeni kutoka Afrika na unataka urudi home baada ya shule unaweza kujikuta unaingia hata Harvard kupiga kitabu bure.

Na ukiomba mara moja ukakosa usikate tamaa - omba tena na tena....
 

Mkuu kwanza za masiku... Nakushukuru kwa maelezo yako yalionipa kitu kipya kwenye hili. Kwa hiyo kumbe mtu ukichaguliwa na ukitaka maisha yawe rahisi baada ya kufika huko ni kufanya academic extension kivyovyote vile!!?

Nimekupata mkuu na maneno yako yamezidi kunitia wazimu wa kukomaa na hii kitu mpaka kieleweke. Hiyo ya kujaribu mara nyingi nyingi ndio nimepanga labda nikutane na vikwazo tu ambavyo ni sugu.
 
Nipo mkuu. Ni maisha tu yamechanganya. Ni mwendo wa kuzisoma namba tu tumemaliza za kawaida na sasa tumehamia za Kirumi.

Elimu ni muhimu sana hasa kama hutaki kufanya kazi za ulinzi airport na ku-flip burgers McDonald's au kuendesha taxis. Hili hata hivyo linategemea na malengo ya mtu na kama anataka kuishi maisha ya kufuata sheria. Otherwise kuna njia za mkato za kuuza ngada; na zinginezo japo uwezekano wa kufia gerezani ni mkubwa. Usikate tamaa kwani kusema kweli hata ile exposure tu inatosha kukupatia mambo mengi ya kufanya siku ukiamua kurudi nyumbani.
 
Bila shaka ni QSS FOTO KING
 
Kila la heri Mkuu Lizarazu. Jiandae kutuma nyingi sana hata kama ni elfu au hata elfu mbili hakuna neno.

 
Asante sana mkuu kwa Uzi wako hata kama Uzi una miaka 10 toka uwekwe..ila kwangu mimi I can certainly say that the particular thread is still valid &viable with my requirements despite the fact that it has been posted here for quite long time ( since 2007 till to date (2017)... Asante sana timu nzima ya JF.
 
Nimepitia Link ya Lottery naona wanafungua May 2 namimi nitajitosa kwenye hiyo application
 
Nimepitia Link ya Lottery naona wanafungua May 2 namimi nitajitosa kwenye hiyo application

May ni kuangalia majibu ya mwaka jana, kujiandikisha ni Oktober.
Kuna dalili kuwa hii Visa inaweza ikafutwa na uongozi wa Trump Marekani so ya mwaka jana au huu inaweza kuwa ya mwisho.
 
May ni kuangalia majibu ya mwaka jana, kujiandikisha ni Oktober.
Kuna dalili kuwa hii Visa inaweza ikafutwa na uongozi wa Trump Marekani so ya mwaka jana au huu inaweza kuwa ya mwisho.
Wamefungua tena for 2020
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…