Wazungu watakaa wanakusubiri utengeneze Nuclear facilities eh? South Africa wenyewe wame-decomission nuclear facilities zao. Not sure wanatumia kiasi gani sasa hivi.
Iran taifa kubwa wananyanyaswa, sembuse Tanzania?
Mambo mengi tunalipua lipua. Infrastructures zetu mbofu. Barabara zinatushinda kutengeneza, madini tunashindwa kuchimba wenyewe. Ije kuwa Nuclear energy?
Thread nyingine nimesoma hao watengeneza bio-gas huko Tanga, target yao ni 2017. Utakuaje na target mbali hivyo wakati teknolojia ipo?
C'mon, i think we jumpin the gun innit?
Jamani kabla ya kujibu. Jaribuni kusoma kwanza. South Africa walikuwa na program za ulinzi na za power. Walizo-decomission ni zile za matumizi ya ulinzi lakini Nuclear Reactors kwa matumizi ya umeme wanazo lakini utoaji wake wa umeme ni 6%. Na kuna mipango ya kuongeza uzalishaji huo.
http://www.world-nuclear.org/info/inf88.html
Kuhusu mada ya Tanzania kuwa na Nuclear Reactors za umeme kuna uwezekano tena mkubwa. Lakini ni lazima tubadilishe mind-set zetu.
Sasa hivi teknologia ya umeme tuliyonayo ni ya kununua na hakuna research zote zinazofanyika na wataalamu wa mashirika hayo.
Kwa upande wa Nuclear ni lazima kwanza tume na taasisi za utafiti na watu waliobobea katika masuala hayo(brain power) na wenye kulipwa vizuri. Tatizo linalokuja ni kuwa priority za mambo ya research nzito hazipo kwenye makaratasi ya serikali.
Hakuna nchi yoyote dunia yenye vinu vya Nuclear na ikawa itategemea watu wenye digrii ya kwanza kuendesha mitambo hiyo.
Wazungu watakaa wanakusubiri utengeneze Nuclear facilities eh? South Africa wenyewe wame-decomission nuclear facilities zao. Not sure wanatumia kiasi gani sasa hivi.
Iran taifa kubwa wananyanyaswa, sembuse Tanzania?
Mambo mengi tunalipua lipua. Infrastructures zetu mbofu. Barabara zinatushinda kutengeneza, madini tunashindwa kuchimba wenyewe. Ije kuwa Nuclear energy?
Thread nyingine nimesoma hao watengeneza bio-gas huko Tanga, target yao ni 2017. Utakuaje na target mbali hivyo wakati teknolojia ipo?
C'mon, i think we jumpin the gun innit?
Bin Maryam,
Na wewe kabla ya kujibu, uwe unasoma vizuri mtu anachoandika. Kuna sehemu nimesema 'not sure wanatumia kiasi gani'. Kwavile wewe unajiona mjuaji wa kuperuzi, sasa mimi nimesomea haya mambo. Jua kwamba, Nuclear plant iwe ya mambo ya silaha au power generation, basi plant yoyote ile, inaweza kuwa de-comissioned, kwasababu plant zote zina shelf life. Kwa mfano, kuna plant inaitwa Sellafield huku UK. Kwavile unabidii ya kusoma, basi google. While you are on it, tafuta na Chernobyl. Ukishafanya hivyo, fikiria na situation tuliyo nayo Congo/Rwanda/Uganda....halafu upige mahesabu ya hiyo Nuclear reactor na usalama wake Tanzania.
Tukirudi Tanzania, kwanza kabisa, huwezi ukaongelea teknolojia ya Nuclear energy wakati bado hatujautumia utajiri wa coal (waliochukua Kiwira coal mine wanajua wamepata nini) uliojaa kusini mwa Tanzania. Pili, gesi na mafuta yapo na yatapatikana zaidi.
Ukijua haya, basi huwezi ukasema 'Sasa hivi teknologia ya umeme tuliyonayo ni ya kununua na hakuna research zote zinazofanyika na wataalamu wa mashirika hayo'. Kama wewe kweli unajua kusoma, basi soma zaidi, utagundua kwamba, one does not need to re-invent the wheel. Teknolojia ipo, na nina imani kabisa utajiri uliopo Tanzania (gas/coal), unaweza maliza matatizo ya umeme for atleast the next 25 yrs (thats my guess) na zaidi. Na katika kipindi hicho ndio watu tuwe tunafikiria teknolojia ya Nuclear. Na ukiwa unaongelea research ya Nuclear, jaribu kutafuta costs za kuwa na Nuclear research facilities.
Na hivi unabidii ya kusoma, wenzako wanachangia 6% to national grid. Mipango yao kuongeza hadi sijui 30% ni miaka si chini ya 20. Na hawa wana-experience ya hiyo kazi. Changanya yote hayo na the fact tunategeme bajeti yetu kutoka donors kwa 40%, halafu uniambie utatengeneza Nuclear reactor.
Ooh, by the way, siku unaanzisha Nuclear facilities Tanzania, nibonyeze (nipe miaka 5 prior warning), foundation ninayo, nikitaka kupata experience hiyo huku katika Nuclear facilities, naweza kabisa, CV inaniruhusu. Na usikute wapo waTanzania nje ya nchi wanafanya kazi katika facilities hizo. Na kama unafanya research vizuri na kusoma, basi utaona, waIran, waChina, waHindi, wapo wanafanya kazi katika facilities za ulaya. maTaifa makubwa yananunua na kuiba teknolojia. Unless Tanzania ina mpango wa kutawaliwa na wamarekani, basi, tuwaruhusu waweke Nuclear facilities.
anyways, i am out!! goodluck with dreams that have no basic foundations!!
Posti yangu nilijibu hoja ya kwamba South Africa wa-decomission. Ukweli walichofanya ni ku-decomission Nuclear Weapon program lakini Nuclear Reactors wanazo. Kinachozungumziwa hapa ni matumizi ya Nuclear katika masuala ya umeme.
Ndio plant zinaweza kuwa de-comissioned lakini za Plant ya South Africa yenye mitambo hiyo bado inafanya kazi. Nenda kwenye web site ya ESKOM.
Na katika posti yangu nimesema uwezekano upo tena mkubwa lakini inabidi tubadili MIND-SET.
Hata makaa ya teknologia ya makaa ya mawe, solar, gass hatuwezi kuitumia kama tunakuwa na MIND-SET tuliyokuwa nayo sasa. Hata kama tutaiba technologia, ni lazima mwizi huyo hawe amesoma.
Gas na Makaa ya mawe haifanyi nchi isiwe na Nuclear reactor. Nigeria mwaka huu imeanza kufanya research za kutumia nguvu hizo.
Kwanini Tanzania iogope situation iliyopo Congo/Rwanda/Uganda? Kwa taarifa nilizonazo Congo (Zaire) wanacho Kinu cha Nuclear na ni cha kwanza barani Afrika ingawaje kwa sasa kiko domant.
Suala la watanzania wenye CV za Nuclear na teknologia nyingine halina mpango kama waliopo madarakani hawakuitaji au hawana sera zenye kuitaji mchango wako. Waliopo madarakani ndio wenye fedha. Na hata de-comissioning ya Nuclear Tech. iwe ya silaha au Enegy zimefanyika kwa sababu waliopo madarakani (wanasiasa) walihamua hivyo.
Unajua wewe unaongelea mambo bila kufuatilia historia kwanini mambo yako kama yalivyo. Congo kupata Nuclear power, kuna sababu. Ukitaka kujua zaidi, labda hii article itakujibu na itajibu security fears nilizotaja hapo juu;
http://www.guardian.co.uk/congo/story/0,,1954795,00.html
Hiyo itakujibu involvement ya Belgium na USA, na bahati ya utajiri wa Congo yenyewe.
Kama watu wanaweza ku-sign contract ili tupate less than 3%, kwanini mtu ashindwe kuuza Uranium rods? Ndugu yangu, we have got our priorities wrong.
Kitu ya Congo imejengwa na wamarekani. SA, wamejenga wazungu. Sio kwamba weusi hawawezi, naamini wacongo wataweza u. Ila Mswahili akipata upenyo wa kuiba, anaiba, consequences badae. Mugabe anaweza kushikilia mashamba makubwa, kazi isifanyike. Mtu anaweza kushikilia machimbo ya makaa, kazi isifanyike. When you own something, the least you can do is get the production going.
Cost ya kutengeneza nuclear plant ni economical in the long run. Ila sasa cost inakuja kwenye de-comissioning, environmental waste etc. Sasa basi,hebu kaa upige mahesabu, angalia priorities zetu zimekaa vipi, ndio utaona kwamba Nuclear technology ni ndoto ya mbeleni, sio sasa.
Kama kuna mtu wa wizara ya nishati na madini (jina limebadilika??), basi atoe estimate za resources za Tanzania, halafu tupige mahesabu.
Inabidi uelewe kwamba, kwa stage ya Tanzania, ni cheaper na economical kutumia coal na gas/oil inayopatikana. Nchi iliyo mbali katika technologia ya Nuclear ni France (hardly anynatural resources) na USA. Angalia kwanini vita vinafanyika Iraq, Iran etc in the name of oil. Ni kwamba, for the next 15 to maybe 50 years, its all about oil. Ni rahisi (cheaper) ku-fund vita kwaajili ya ku-control mafuta na umhimu wake, kuliko kuhangaika na Nuclear.
Kumbuka technology hii wanayo wenzetu tayari. Tanzania wakitaka kwenda huko watatafutiwa kila sababu wasiguse anga hizo. Unless kuna involvement ya wazungu. Halafu jua kwamba kunanchi zingine za ulaya hazina Nuclear power au hawatumii kabisa (nadhani Austria ni moja ya nchi hizo, unless wamechange hivi karibuni).
Wewe hujatambaa, unataka u-break-dance?
Mswahili atafanya dili rods na kuzinadi e-bay! Mafundi wetu wa ujenzi wanakataa kuvaa buti, kofia na glavs ati zinaleta joto. Mafundi wa foundry hawataki kuvaa miwani ati wao ni wazoefu. Mafundi wa umeme wanacheki chaji kwa kulamba. Kwenye hayo mareactor utawakuta wanataka kuzishika hizo rod kwa kutumia mikono mikavu. Wengine mission town watajaribu kuzikwapua huku wamezificha kwenye sehemu nyeti. We are not serious enough. Tusiende huko, tutajiua.
Mh, Fundi kweli unakandamiza kimarekani! yaani wataalamu wa nuclear reactor wako garage bubu pale kidongo chekundu! Kama tuna gas powered turbine pale songas sioni tatizo la kuwa na other sources. exploration ya uranium inaendelea vizuri, kama wewe ni mhandisi wa nuclear energy unakaribishwa sana.
Fundi Mchundo. Amen! Happy New Year to you.
First commercial nuclear reactor ilianza operations Soviet Union 1954, ikafuatwa na ya uingereza in 1956 na wamarekani 1957. Wakati huo, hizi ndizo zilikuwa superpowers za dunia. Sisi hatujafikia hapo. Tuendeleze Bio, solar na other alternative energy sources ambazo ziko within our reach. Tukazanie kuongeza efficiency katika matumizi ya umeme. Haya ya Nuclear ni kama vile tunavyokazania kujenga skyscrapers wakati tuna fire engines za kuhesabu, wakati hatuna waste treatment plants ( raw sewage bado tunai"pump" baharini, wakati bado sehemu kubwa tunategemea septic tanks! Priorities zetu ziko "warped". What would we be trying to proove by going nuclear? Who are we trying to impress?
Mkuu Eddy! Wakati wa ukame mwaka uliopita wataalam walishauri kuwa maji yamefika absolute minimum kwa hiyo ni lazima mitambo izimwe kwa usalama wake! Wakuu wakaamrisha waendelee ku'generate' na kuomba wanachi wamuombe mwenyezi Mungu alete mvua! Sasa, imagine, wataalam wa nuclear reactor wamegundua kuna hitilafu na wanatakiwa kuizima kwa tahadhari, hawa waheshimiwa wetu watawaambia nini ukichukulia kuwa wakati huo pengine hiyo reactor ndiyo inayotoa sehemu kubwa ya umeme kwenye grid? Nakuhakikishia watamwambia mtaalam ajitahidi kuvuta kidogo wakati KAMATI inashughulikia. Hivi leo tunahangaika kuwapeleka na kuwarudisha mahujaji Mecca tutauweza mtambo wa aina hii? Kuna sehemu nimesoma kuwa wakubwa wametoa maagizo kwamba hao mahujaji warudi kwa udi na uvumba tarehe fulani kwa vile waliishamueleza Mheshimiwa Rais! Unaamini kuna watendaji kweli nchini mwetu ambao wanaweza kusimamia kidete taaluma yao? Pamoja na gharama kubwa ya kujenga hiki kinu tatizo kubwa ni namna ya kudispose spent fuel ambayo mara nyingi inakuwa weapon grade? Unadhani tutaweza yote hayo na kuhakikisha haipotei? Leo hii wavuvi wa ngalawa wanaotumia baruti wanatupeleka mchakamchaka itakuwa watu waliokamia kweli kuipata hiyo fuel? Leo hii tunashindwa kumaintain CAT scans katika mahospitali yetu ( private na public) itakuwa mtambo kama huu! Bado wakati wetu. Kama alivyosema mkuu mmoja, ngojeni tutakapoondoka labda mtaweza kubadilisha kilichoitwa mind-set. Sio wakati sisi tupo.