Urais 2015, kundi langu ni CCM

Urais 2015, kundi langu ni CCM

tueleze namna ulivyo shiriki kuawatu Arusha kama ahadi yako..
 
Maambukizi mapya! CCM imejaa mashetani balaa! Hawana hata hofu ya Mungu

Unashangaa hayo....ona haya mkuuuuuu

j7.jpg
 
Inasikitisha sana....Chama ambacho huwezi mtofautisha mzee na mhuni...

Ni balaa ndugu yangu;

Chama cha Mateja
Chama cha Mabakaji
Chama cha Mazinzi
Chama cha Majangili
Chama cha Majizi
Chama cha Malaghai.......................What new do you expect from them

J3.jpg
 
gud approach.. ila tu kama unatenda unachohubiri.
katika mtihani mkubwa kabisa tuliopata kuupitia watanzania tangu uhuru, nadhani kupata mgombea wa CCM 2015 ndio mtihani mgumu zaidi. na hii ni kwa sababu yule anayepigiwa debe na wana ccm wanaofanya maamuzi ndiye asiyefaa kuliko wote.
mungu namuomba awape ujasiri akina NAPE
Mkuu, ninakubaliana na wewe.

Kama CCM itapita bila mtikisiko katika uteuzi wa mgombea Urais ( kama zitabaki serikali mbili) basi hii itakuwa ni ajabu ya mwaka.

CCM itapumua kama katiba itaruhusu serikali tatu. Kama zitabaki serikali mbili, ninaona mtifuano wa ajabu ukiwadia.

Hiki ni kipindi kwa mara ya kwanza ambapo CCM haina mgombea ambaye watu wanaweza wakasema "This is the one".

1995, Mwl. Nyerere alitumia nguvu zake katika kumuweka Rais Mkapa. Mwaka 2005, Watanzania walikuwa tayari wameisha mchagua Rais Kikwete hata kabla ya mchakato kuanza.

Kwa sasa ni mwaka mmoja na nusu kabla ya mchakato lakini hakuna mgombea ambaye ni potential katika macho ya wanaCCM kitu ambacho kinachangia watu wengi kujitokeza na katika kufanya hivyo, ndipo makundi yanajitokeza mpaka tunasikia kina Mwigulu Nchemba nao wanasema wanaweza kugombea.
 
Last edited by a moderator:
Wana jf Salaam,

Nimelazimika kusema machache kutoa ufafanuzi kufuatia uzi wa Mwita Maranya na wengine wenye fikra hizo. Mwita ama kwa kutokujua historia yangu na uzito wa nafasi niliyonayo amenipa ufusia wa mgombea arais au kundi la mgombea. Kwa historia yangu na kwa nafasi yangu ndani ya chama huu sio muda wa kuwa na kundi. KUNDI LANGU NI CCM. NITAWAUNGA MKONO WAGOMBEA WA NGAZI ZOTE WATAKAOKABIDHIWA JUKUMU LA KUPEPERUSHA BENDERA YA CCM 2015 KWA MJIBU WA KATIBA NA KANUNI ZA UCHAGUZI NDANI YA CCM.

Mosi, historia yangu kwenye siasa, mimi sio matokeo ya jitihada za kundi lolote kufika hapa. Niligombea ubunge nikiwa sijulikani na kundi lolote na wala sikutengenezwa na kundi lolote.Ungekuwa wakati wa kutafuta kundi ungekuwa huo maana nilikwenda kugombea nikiwa sina baisikeli, pikipiki wala gari. Ungekosa sifa zote kuhusu mimi, moja tu ungepewa na wanaccm ni kwamba mimi sina kundi na sitokani na makundi yanayokinzana, sina chuki na kundi lolote na wala siegemei kundi lolote. Hivyo hivyo nilishinda kwa kishindo uchaguzi ndani ya chama moja ya sababu nikutokuwa na ugomvi wala chuki na wanaccm na sina sababu na sioni faida ya kuingia kwenye makundi katika ngazi hii na muda huu. AM THE ACTOR AND DIRECTOR OF MY OWN IN POLITICS.

Pili kwa nafasi yangu mimi ni mkuu wa utumishi na utawala. Nimekuwa msiri wa mbele kuzuia watumishi wote na viongozi wa kuchaguliwa kutoingia kwenye makundi ya wagombea mpaka pale chama kitakapo watangaza kupitia NEC ya CCM. Nimetoa maelekezo hayo mikoani na wilayani kwa barua. Haiwezekani nitoe maelekezo kuwazuia wenzangu halafu mimi niwe kwenye kundi lililowazuia wenzangu. Ndio maana sijawahi shiriki kikao, mazungumzo yeyote ya kundi la mgombea, wakala wa mgombea au mgombea.

Tatu, kwa nafasi yangu naingia vikao vyote vya maamuzi ya chama vitakavyowajadili wagombea kwa mujibu wa katiba. Natakiwa kuwatendea haki wagombea wote. Sipaswi kuwa na upande katika mazingira hayo kwani huwezikutenda haki ukiwa nawe ni mjumbe wa vikao huku una mgombea. Nani atawatetea au kuwatendea haki wengine wasiokuwa 'wakwako' kiongozi ukiingia kwenye makundi.

Nne kuwa na kundi kunakusabisha kuchukiwa na wanaccm wenye makundi yao au wagombea wao kisirisiri. Mimi naungwa mkono na wana ccm wote kwa sifa hiyo ya kujenga chama na kuwaunganisha wanaccm. MAKUNDI YOTE WANAONA NAWATENDEA HAKI PUNDE KUNA KITU KINAHITAJI UAMZI.

Ukiwauliza wanaccm wakutajie watu watatu ambao wana imani nao wanaoweza kuwaunganisha na kuwapa ushindi nami nipo.

Nikuulize swali Mwita, umekiri mwenyewe kuwa wanaccm wanamatumaini makubwa namimi ya kuwavusha, umekiri pia kuwa napendwa na vijana. Ila umenipa ufuasi kwenye makundi ya wagombea, ULIWAHI KUNIULIZA BINAFSI NIKAKWAMBIA SIGOMBEI HATA UHANGAIKE KUBASHIRI KUWA MIKI NIMFUASI WA KUNDI FULANI.? MIMI NI KIUNGO NA KIONGOZI WA CCM NA MAKUNDI YOTE NDANI YA CCM.

CHAMA CHETU NI CHAMA CHA UTARATIBU NA MIMI NDIO MSIMAMIZI MKUU WA UTARATIBU NDANI YA CHAMA. KUNDI LANGU NI CCM.

kiungo wa kutoa roho za watanzania wezako..wewe ni shetani mkubwa.
 
mwigulu katika vijana wahuni, arrogance wapumbavu na kudharauliwa milele ni wewe, hata kabila lako la wanyiramba unawaibisha daima, watakao hukumiwa na historia milele ni wewe, swala la kundi lako mie najua kundiko lako nila kuwaua watz na kutengenza kesi FAKE kwa wapinzani wenu, SHAME UPON YOU, HUNA LOLOTE CHUKI TU IMEKUJAA

Mwigulu ni JANGA...Songela Zigizigi

j4.jpg
 
mwigulu poor leader

Mwigulu Nchemba a.k.a Jonas Savimbi, Bosco Ntaganda na Kiongozi wa Lords Resistance Army!

Hongera nimekupata! Unaweza kuniazima hata kabomu kamoja? Kule Arusha halikubaki hata moja? Nina shida nalo tafadhali.
 
................................ nilikwenda kugombea nikiwa sina baisikeli, pikipiki wala gari. .........................................

Umeongea mengi mazuri lakini suala la kuongopa wazi wazi hujataka kuliacha kama Mwenyekiti wa chama chako. Je uchunguzi ukifanyika utabaini kwamba wakati unaenda kugombea ubunge ni kweli ulikuwa huna baisikeli, pikipiki wala gari? sentensi hiyo umeiweka mwanzoni kabisa kuwafanya watu wasiendelee kusoma ulichoandika mbele
 
If that is the case, kwa nini umechangia na unaendelea kuchangia?. You must be thick as two short planks beyond reasonable doubt!.

Watu wengine mnashangaza sana.

Coz a stupid thread should be treated same way

Chukua popcorn...weka soda...pata kitu hapo

j5.jpg
 
Ukiacha ku-pretend tutakujua

Sasa hivi hatuwezi kukujua, unasema A na hali matendo yako ni B

Semi zako zinajikanganya, unasema hukufikishwa hapo na mtu, na uligombea ukiwa huna baskeli, Haya unadhani una jeuri ya kumtunishia misuli aliyekupendekeza nafasi hiyo?

Unataka kusema hauko biased 100%?
Thanx sixgates. watu wengi hawanijui vizuri.
 
bora uwe mchawi kuliko mnafiki ccm acheni unafiki .
 
Mkuu umesomeka na umeeleweka kwa wenye akili zao
Piga kazi mkuu
 
Mwigulu Nchemba a.k.a Jonas Savimbi, Bosco Ntaganda na Kiongozi wa Lords Resistance Army!

Hongera nimekupata! Unaweza kuniazima hata kabomu kamoja? Kule Arusha halikubaki hata moja? Nina shida nalo tafadhali.

au alivyo muua wakala wa chadema kule Igunga na alivyo ratibu mauwaji ya mwenyekiti wa chadema kata ya usa river
 
MWANAMUME huyu wanamuogopa CDM hata kivuli chake.

Kwa usalama wao ni bora wamuogope.Kama mtu aliweza kumchonga mwanachama mwenzake kwa tindikali na kumufanya kuwa jini la kuwaletea kura unadhani ni mtu wakaida huyo.Ambae hana uoga na mtu huyu ujue kuwa huyo mtu hana huruma na uhai wake au nae ni mshirika wa vitendo vyake vichafu.
 
Back
Top Bottom