Urais 2015: Bosi mstaafu TISS matatani

Urais 2015: Bosi mstaafu TISS matatani

thatha

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2011
Posts
15,340
Reaction score
1,573
Mkurugenzi mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa, TISS ambaye gazeti la SAUTI HURU limesema jina lake linalo kwenye mabano ameingia matatani baada ya kukiri kujiingiza katika siasa za Chama cha Mapinduzi , CCM.
Imedaiwa pia kuwa kibosile huyo wa zamani wa TISS Amemrubuni Mwenyekiti wa NCCR, James Mbatia ili aweze kuwashawishi Wakatoliki na UKAWA ili kumuunga mkono LOWASSA.

20140828_100051.jpg

source: SAUTI HURU.
 
TISS sio wajinga, hawawezi kujiingiza huko, msiwagombanishe na wananchi
 
nina imani na TISS, NDIO TAASISI PEKEE YA UMMA ILIYOBAKI TUNAYOIAMINI KUTUTETEA WANYONGE..HUYO ATAKUWA BOSS NJAA/MCHUMIA TUMBO
 
nina imani na TISS, NDIO TAASISI PEKEE YA UMMA ILIYOBAKI TUNAYOIAMINI KUTUTETEA WANYONGE..HUYO ATAKUWA BOSS NJAA/MCHUMIA TUMBO
Nadhani taarifa inamlenga Apson Mwang'onda, Mkurugenzi wa TISS mstahafu. Waliopo maadili ya kazi yanawabana. Hawawezi kujiingiza kwenye siasa za makundi
 
Nadhani taarifa inamlenga Apson Mwang'onda, Mkurugenzi wa TISS mstahafu. Waliopo maadili ya kazi yanawabana. Hawawezi kujiingiza kwenye siasa za makundi

Bila shaka bwana Lizaboni, kwa sababu gazeti linasema ni mstaafu sasa haijukikani kama ni huyo uliyemtaja au la
 
Si wamtaje tu Apson Mwang'onda, Habari yenyewe wameiokoteleza humu Jf Hili Gazeti nalo lina muhariri ..........basi tu ngoja niishie hapo.

Sidhani kama ni Sauti huru pekee wanaopata habari ktoka kwenye mitandao ya kijamii, na binafsi naona ni sawa tu kwa sababu kuna watanzania wengi hawana access na internet lakini wanafikiwa na magazeti, siyo vibaya wakazipata habari za mitandaoni kupitia magazeti na hata tv au redio
 
Si wamtaje tu Apson Mwang'onda, Habari yenyewe wameiokoteleza humu Jf Hili Gazeti nalo lina muhariri ..........basi tu ngoja niishie hapo.
Huyo boss mstaafu alikanusha lakini alisema akitaka kuwa kwenye hiyo kambi haoni ubaya wowote na hakuna wa kumzuia.Sasa hii kakiri sijui huyu mwandishi kaitoa wapi?
 
Sidhani kama ni Sauti huru pekee wanaopata habari ktoka kwenye mitandao ya kijamii, na binafsi naona ni sawa tu kwa sababu kuna watanzania wengi hawana access na internet lakini wanafikiwa na magazeti, siyo vibaya wakazipata habari za mitandaoni kupitia magazeti na hata tv au redio

Atukatai basi wawe wanataja chanzo
 
Washaurini wasiende shule kwa ze kapa amasivyo atamkombesha
 
Hawa Sauti Huru ni wajinga wajinga fulani hivi sasa wanaficha hilo jina wakati anajulikana kabisa kuwa ni Apson
 
Huyo boss mstaafu alikanusha lakini alisema akitaka kuwa kwenye hiyo kambi haoni ubaya wowote na hakuna wa kumzuia.Sasa hii kakiri sijui huyu mwandishi kaitoa wapi?

Kwa mtu muelewa , ndiyo kukiri kwenyewe huko
 
Hawa Sauti Huru ni wajinga wajinga fulani hivi sasa wanaficha hilo jina wakati anajulikana kabisa kuwa ni Apson

Teh teh, maadili ya kazi yao labda yanawakataza au wanajua kabisa kuna watu viherehere watawasaidia kumtaja.
 
Kwa mtu muelewa , ndiyo kukiri kwenyewe huko

Kwa hiyo wewe ukiulizwa kwamba kuna tetesi unataka kuhamia Chadema halafu ukakanusha kwamba sio kweli lakini ukaongezea kwamba hata ukitaka kuhamia Chadema hakuna wa kukuzuia.. Utakuwa umekiri kwamba wataka kuhamia Chadema..?
 
Back
Top Bottom