Uraia wa Sioi utata mtupu,CCM kutangaza mgombea mpya ARUMERU leo!!

Uraia ndiyo kete kubwa ya magamba wanapotaka kukumaliza! huyu dogo atakuwa ni mmoja tu wa wengi waliopitia katika hujuma ya namna hii!!
 
Sasa huyo SIOI awapo Tanzania anakuwa na muhuri wa Tanzania kwenye Passport yake ya Kenya?..............hii ni vita vya 2015 kwani naamini bila shaka huyo kijana ana PASS YA KUSAFIRIA ya Tanzania hivyo swala kwamba si raia ni kwa sababu tuu Mh. Lowassa yuko nyuma yake

:canada:Ameukana uraia wa Kenya!?
 
hakuna swala la raia wa nchi mbili au tatu sheria zipo wazi, ukizaliwa nje ya Tanzania na wazazi wa Tanzania initially unakuwa na urai wa nchi mbili ulikozaliwa na Tanzania ukifikisha miaka 18 unatakiwa ukane uraia mmoja na kubaki na mmoja usipofanya hivo automatically unapoteza uraia wa Tanzania hivo huyu mheshimiwa kama hakukana uraia wa Kenya alipotimiza miaka 18 basi kwa sasa ni raia halali wa kenya na anaishi hapa kinyume cha sheria hivo anatakiwa sio kunyimwa kugombea ubunge tu bali kufikishwa mahakamani kujibu shtaka la kuishi nchini kinyume cha sheria!!

Mkuu,
Hauko sahihi kabisa. Kuzaliwa nje ya nchi hakukufanyi wewe uwe automatically raia wa ile nchi ulikozaliwa.

kwa mfano ukizaliwa Tanzania na wazazi wasio Watanzania wewe hauwi raia wa Tanzania.

Je huyo Sioi mzazi wake mmoja ni Mkenya? Kama wakati anazaliwa wazazi wake wote wawili walikuwa Watanzania, unachoandika hapo juu hakina ukweli wowote.
 
Feedback, japo sina chama na Chadema naikubali sana tuu, ila kwenye uchaguzi wa Arumeru, nasimama na Sioi na machalii wote wa AR wako nyuma yake!. Asipopitishwa na CC leo, ile kambi yote ya Sioi, watashiriki kampeni za CCM, ila kura Chadema!. Kiuhakika bila Sioi, CCM itaangukia pua!.

Igunga RA ni muoga kama kunguru siku za mwisho alijitokeza kuokoa jahazi, Sioi asipopitishwa Mmeru No. 1 hatatia mguu Arumeru!, CCM ni kifo cha mende straight away!.

Analysis yako imeshindwa kunitoa tongotongo.Imejaa ushabiki,tusubiri vyama vyote vikamilishe kutoa wagombea,tupime upepo wa kampeni walau wiki ya kwanza
 
Jamani hapa suala la uraia ni kiini macho tu mnafikiri wao walikuwa hawajui, hapa kinachozingatiwa ni maslahi, kwa serikali hii ya CCM hilo ni jambo dogo sana kumalizwa msishangae kesho na kesho kutwa kusikia Sioi ni mkuu wa wilaya.
 
Igunduliwe na nani EMT hawa hawa CCM?, tatizo hapa si uraia wa Sioi ila wameona hauziki hapa zinazitafutwa sababu tu za kumridhisha yeye na wafuasi wake kuhusu kuenguliwa, kwa vile CCM wana uwezo kabisa wa kusema juzi aliukana uraia wa Kenya and no one can question.

Au wanamfanyizia Lowassa kiana?
 
Hakuna kesi ya uraia hapa labda kwa kujifurahisha tu.

Huyo kijana amezaliwa baada ya Uhuru wa Tanganyika na baba yake wakati anamzaa alikuwa ni raia wa Tanzania. Huyu ni mtanzania piga ua labda tu awe amechukua uraia wa nchi nyingine alipokuwa mdogo.

Kuzaliwa nje ya Tanzania na mzazi mmoja Mtanzania hakukuondolei wewe Utanzania wako.

hao wanaoleta tetesi hata hawajui sheria za uraia za Tanzania zinasema nini.

Hii sheria ya uraia inatamka wazi juu ya hili.

Every person born outside the United Republic on or after Union
Day shall, with effect from the date of his birth, be deemed to have
become and to have continued to be, and with affect from the commencement of
this Act shall become and continue to be, a citizen of the United
Republic if at the date of his birth his father or mother is or was a citizen
Republic on or after Union of the United Republic otherwise than by descent, subject to the provi
sions of section 30.

mimi ni chadema, kwa uraia wa sioi sina tatizo mana huyu bwana kazaliwa ubalozini kenya,baba yake alikuwa afsa kule,sheria za kimataifa zinatambua ofisi let say ya ubalozi wa tanzania huko zambia ni si ardhi ya zambia.kwa mfano pale ofisi ya Us pale msasani peninsula ni ardhi ya marekani.leteni hoja
 
Analysis yako imeshindwa kunitoa tongotongo.Imejaa ushabiki,tusubiri vyama vyote vikamilishe kutoa wagombea,tupime upepo wa kampeni walau wiki ya kwanza
Mkuu unataka kutuambia baada ya wiki moja kampeni kuanza kama ukiona upepo haufai utambadilisha?, kina cha maji hakipimwi ukiwa ndani ya maji huu ndio wakati mwafaka wa kupima mgombea yupi anafaa kama wanavyofanya sasa CCM.
 
Masuala ya uraia nchini Tanzania yanasimamiwa na sheria ya uraia na.6 ya mwaka1995, pamoja na kanuni zake za mwaka 1997. Kwa mujibu wa sheria hiyo, zipo aina tatu za uraia nchini Tanzania ambazo ni:-
1. Uraia wa Tanzania kwa Kuzaliwa.
2. Uraia wa Tanzania kwa Kurithi.
3. Uraia wa Tanzania kwa Tajnisi.

Uraia wa Tanzania kwa kuzaliwa
Kwa mujibu wa sheria ya uraia ya na. 6 ya mwaka 1995, mtu yeyote anayekuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzaliwa ni yule aliyezaliwa nchini Tanzania na ambaye wakati wa kuzaliwa kwake mmoja wa wazazi wake alikuwa raia wa Tanzania.

Uraia wa Tanzania kwa Kurithi.
Mtu yeyote aliyezaliwa nje ya Jamhuri ya Muungano au baada ya Muungano atahesabika kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi kuanzia tarehe ya kuzaliwa kwake ikiwa siku ya kuzaliwa kwake mmoja wa wazazi wake ni raia wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzaliwa au Tajnisi. Hii ina maana kuwa kama wazazi wake walikuwa ni raia wa Tanzania kwa kurithi wakati wa kuzaliwa kwake mtu huyo hawezi kuwa raia wa Tanzania kwa kurithi.

Uraia wa Tanzania kwa Tajnisi.
Mtu yeyote ambaye siyo raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzaliwa au kurithi anaweza kuomba uraia wa Tanzania kwa tajnisi kwa mujibu wa vifungu na.8 na 9(1) vya sheria ya uraia ya mwaka 1995. Kwa mujibu wa sheria hiyo, mheshimiwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia masuala ya uraia nchini (kwa sasa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi) ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kutoa au kutotoa uraia wa nchi Tanzania kwa wageni waliiomba uraia.
 
Hakuna kesi ya uraia hapa labda kwa kujifurahisha tu.

Huyo kijana amezaliwa baada ya Uhuru wa Tanganyika na baba yake wakati anamzaa alikuwa ni raia wa Tanzania. Huyu ni mtanzania piga ua labda tu awe amechukua uraia wa nchi nyingine alipokuwa mdogo.

Kuzaliwa nje ya Tanzania na mzazi mmoja Mtanzania hakukuondolei wewe Utanzania wako.

hao wanaoleta tetesi hata hawajui sheria za uraia za Tanzania zinasema nini.

Hii sheria ya uraia inatamka wazi juu ya hili.

Every person born outside the United Republic on or after Union
Day shall, with effect from the date of his birth, be deemed to have
become and to have continued to be, and with affect from the commencement of
this Act shall become and continue to be, a citizen of the United
Republic if at the date of his birth his father or mother is or was a citizen

Republic on or after Union of the United Republic otherwise than by descent, subject to the provi
sions of section 30.
Asante Mkulima kwa kutuletea kifungu hiki, watu wanafikiri uraia wa Sioi una utata, tatizo lilopo huko CC and always has been ni maslahi ya pande zinazovutana.
 
Uangukaji wa chama likubwa kama CCM lazima uambatane na sarakasi nyingi! na bado nyingine nyingi zaja.
 
Kama kuna mtu wa karibu na mama mzazi wa huyu kijana Sioi hapa JF basi ningeshauri amtoe mwanae kwenye hizi siasa uchwara. Sioi ni kijana mdogo sana aliyefiwa na baba yake, bado yuko kwenye msiba, haihitaji hizi sakarasi za siasa za kuwindana. Inawezekana kabisa huyu kijana amezungukwa na watu wazima, watu ambao yeye binafsi anashindwa kuwaambia NO. Ni jukumu la mama mzazi kumsadia mtoto wake. Kwanza wanaotoka hili jimbo sio wagumba, wana watoto, wawapeleke watoto wao wakagombee. Mama Sioi mwokoe mwanao.
 
mimi ni chadema, kwa uraia wa sioi sina tatizo mana huyu bwana kazaliwa ubalozini kenya,baba yake alikuwa afsa kule,sheria za kimataifa zinatambua ofisi let say ya ubalozi wa tanzania huko zambia ni si ardhi ya zambia.kwa mfano pale ofisi ya Us pale msasani peninsula ni ardhi ya marekani.leteni hoja

Nimemfahamu marehemu Jerry Solomon Sumari kwa muda, sikumbuki kama aliwahi kufanya kazi kwenye ubalozi wetu huko Kenya!! Swali ni kwanini SIOI mwenyewe hakujaza sehemu ya uraia wake kwenye form yake?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Nimemfahamu marehemu Jerry Solomon Sumari kwa muda, sikumbuki kama aliwahi kufanya kazi kwenye ubalozi wetu huko Kenya!! Swali ni kwanini SIOI mwenyewe hakujaza sehemu ya uraia wake kwenye form yake?

Marehemu Jerry Solomon baada ya kuondoka Beki kuu alikwenda Kenya na kufanya kazi Shell Chemical Company of Eastern Africa na baadaye kuja Tanzania na kufanya kazi na kampuni hiyo hiyo na baadae kuanza shughuli zake dinafsi. Niyo ndiyo taarifa ya uhakika.
 
Ninavyoelewa mie, ukizaliwa nje ya Tanzania kwa wazazi wa Kitanzania, unatakiwa ku-declare uraia wako by age 18. Kama hujadai haki ya uraia kwa minajili ya wazazi wako, unakosa haki ya uraia wa Tanzania.

Kama huyu Sioi alizaliwa Kenya, alifanya declaration ya kuuchukua uraia wake wa Tanzania? Kama haja declare si Mtanzania, ni Mkenya.
 
This is nonsense, hata kama watu wanamchukia mtu lakini huu ni ujinga wa hali ya juu. Sioi ni Mtanzania , period. Huu ujinga wa kutetea ****** kwa sababu tuu mtu wanayemattack ni mkwe wake Lowassa ni ujinga uliopitiliza. Leo wamemwita Sioi sio raia tunakaa kimya, kesho watakuita wewe sio raia na kutakuwa hakuna wa kukutetea. CCM ni chama chenye ubaguzi wa hali ya juu! Tuliona walivyomwita Salum mwarabu kipindi cha kampeni, yule jamaa wa Tabora walisema ni msomali, sasa Sioi ambaye baba yake ni mtanzania na mama yake pia wanamwita sio mtanzania. The guy is holding a Tanzanian passport and they are saying is not a citizen, this is pathetic.
 
Back
Top Bottom