Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,723
- 218,285
Huu ndio Ukweli unaofichwa , huyu aliyepo hana uwezo wa kupambana Jukwaani (Chama chake kinajua) , hata hivyo alishawahi kukiri mwenyewe hadharani , ikaandikwa na gazeti la Chama chake , ili kuondoa Taharuki ikakanushwa , hata hivyo awali ni awali , na wala hakuna awali mbaya , sisi tumeshika lile neno la mwanzo tu .
Baada ya Makada kutambua kwamba nafasi ya Urais ya Chama chao iko wazi wameanza kuparurana , unaambiwa hali ni mbaya kiasi cha kufikia kulogana , Yale aliyoyasema Kikwete kwamba wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani yamerejea kwa kishindo .
Lakini katika hawa wanaccm mnaowaona leo yuko hata mwenye uwezo wa kuwa Rais wa Nchi ? Watoto wa viongozi waliotegemewa kupewa nafasi hiyo kama Urithi wa Wazazi wao wote wameboronga , hawavutii na hawatamaniki , watu wameshika mafaili yao zikiwemo idadi za nyumba zao ndogo za kimagumashi , wakthubutu kutangaza nia tu Mkeka unaanikwa ! hakuna hata mmoja wao anayeweza kupambana na Wapinzani Jukwaani , Ni nani atayeweza kupangua hoja za Chadema Majukwaani ?
Taarifa zinadokeza kwamba hata matumizi ya dola ili kuibeba ccm hata kwa wizi yamefifia mno , hii ni kwa sababu mashinikizo ya watoa hela kutoka Ulaya na Marekani kutaka Wakurugenzi wa Halmashauri na Polisi wasiguse karatasi ya kura ni makubwa mno na yanamaanisha hasa ( Mbeleko imetoboka )
Hali ni mbaya kuliko mnavyofahamu , muda si mrefu mtaanza kusikia makubwa zaidi
Tuendelee kutega sikio
Baada ya Makada kutambua kwamba nafasi ya Urais ya Chama chao iko wazi wameanza kuparurana , unaambiwa hali ni mbaya kiasi cha kufikia kulogana , Yale aliyoyasema Kikwete kwamba wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani yamerejea kwa kishindo .
Lakini katika hawa wanaccm mnaowaona leo yuko hata mwenye uwezo wa kuwa Rais wa Nchi ? Watoto wa viongozi waliotegemewa kupewa nafasi hiyo kama Urithi wa Wazazi wao wote wameboronga , hawavutii na hawatamaniki , watu wameshika mafaili yao zikiwemo idadi za nyumba zao ndogo za kimagumashi , wakthubutu kutangaza nia tu Mkeka unaanikwa ! hakuna hata mmoja wao anayeweza kupambana na Wapinzani Jukwaani , Ni nani atayeweza kupangua hoja za Chadema Majukwaani ?
Taarifa zinadokeza kwamba hata matumizi ya dola ili kuibeba ccm hata kwa wizi yamefifia mno , hii ni kwa sababu mashinikizo ya watoa hela kutoka Ulaya na Marekani kutaka Wakurugenzi wa Halmashauri na Polisi wasiguse karatasi ya kura ni makubwa mno na yanamaanisha hasa ( Mbeleko imetoboka )
Hali ni mbaya kuliko mnavyofahamu , muda si mrefu mtaanza kusikia makubwa zaidi
Tuendelee kutega sikio