Ukweli ni kwamba CCM haina Mgombea Urais 2025, ndio chanzo cha kulogana na kuchafuana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,723
218,285
Huu ndio Ukweli unaofichwa , huyu aliyepo hana uwezo wa kupambana Jukwaani (Chama chake kinajua) , hata hivyo alishawahi kukiri mwenyewe hadharani , ikaandikwa na gazeti la Chama chake , ili kuondoa Taharuki ikakanushwa , hata hivyo awali ni awali , na wala hakuna awali mbaya , sisi tumeshika lile neno la mwanzo tu .

Baada ya Makada kutambua kwamba nafasi ya Urais ya Chama chao iko wazi wameanza kuparurana , unaambiwa hali ni mbaya kiasi cha kufikia kulogana , Yale aliyoyasema Kikwete kwamba wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani yamerejea kwa kishindo .

Lakini katika hawa wanaccm mnaowaona leo yuko hata mwenye uwezo wa kuwa Rais wa Nchi ? Watoto wa viongozi waliotegemewa kupewa nafasi hiyo kama Urithi wa Wazazi wao wote wameboronga , hawavutii na hawatamaniki , watu wameshika mafaili yao zikiwemo idadi za nyumba zao ndogo za kimagumashi , wakthubutu kutangaza nia tu Mkeka unaanikwa ! hakuna hata mmoja wao anayeweza kupambana na Wapinzani Jukwaani , Ni nani atayeweza kupangua hoja za Chadema Majukwaani ?

Taarifa zinadokeza kwamba hata matumizi ya dola ili kuibeba ccm hata kwa wizi yamefifia mno , hii ni kwa sababu mashinikizo ya watoa hela kutoka Ulaya na Marekani kutaka Wakurugenzi wa Halmashauri na Polisi wasiguse karatasi ya kura ni makubwa mno na yanamaanisha hasa ( Mbeleko imetoboka )

Hali ni mbaya kuliko mnavyofahamu , muda si mrefu mtaanza kusikia makubwa zaidi

Tuendelee kutega sikio

FB_IMG_1648410131191.jpg
 
Huu ndio Ukweli unaofichwa , huyu aliyepo hana uwezo wa kupambana Jukwaani (Chama chake kinajua) , hata hivyo alishawahi kukiri mwenyewe hadharani , ikaandikwa na gazeti la Chama chake , ili kuondoa Taharuki ikakanushwa , hata hivyo awali ni awali , na wala hakuna awali mbaya , sisi tumeshika lile neno la mwanzo tu .



View attachment 2830279
Sasa CHADEMA mna hoja gani sasa hivi zaidi ya kulalamika badala ya kujenga hoja?
Wiki hii yote mmeshinda mnajadili masuala ya mkutano wa CCM na kujiuzulu kwa Katibu Mkuu Chongolo kana kwamba yamo kwenye mipango na katiba ya chama chenu.
Wananchi wanatarajia nyinyi kama chama cha upinzani mngechukua Ilani ya CCM ya 2020-2025,muichambue na kuwaeleza Wananchi nini CCM waliahidi hawajafanya na nyinyi mkipewa mamlaka mtafanya kwa mtindo gani.Sasa kutwa kusubiri migogoro itokee serikalini na CCM ndiyo mupate cha kuongea!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Bora aliyepo aondoke tu, hawezi hiyo kazi, ni chawa tu ndio wanaomsifia.

Nimeshangaa nauli za mabasi ya mikoani na daladala kutaka kupandishwa tena, less than a year toka zilipopanda mwanzo, hii ni ajabu na tusi kwa raia wa hii nchi.

Kuna wajanja wanamchezea sana huyu kiongozi aliyepo, wamemkamata akili hafurukuti kabisa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Sasa CHADEMA mna hoja gani sasa hivi zaidi ya kulalamika badala ya kujenga hoja?
Wiki hii yote mmeshinda mnajadili masuala ya mkutano wa CCM na kujiuzulu kwa Katibu Mkuu Chongolo kana kwamba yamo kwenye mipango na katiba ya chama chenu.
Wananchi wanatarajia nyinyi kama chama cha upinzani mngechukua Ilani ya CCM ya 2020-2025,muichambue na kuwaeleza Wananchi nini CCM waliahidi hawajafanya na nyinyi mkipewa mamlaka mtafanya kwa mtindo gani.Sasa kutwa kusubiri migogoro itokee serikalini na CCM ndiyo mupate cha kuongea!

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
Mijadala ya JF siyo mijadala ya Chadema , uwe natofautisha
 
Bora aliyepo aondoke tu, hawezi hiyo kazi, ni chawa tu ndio wanaomsifia.

Nimeshangaa nauli za mabasi ya mikoani na daladala kutaka kupandishwa tena, less than a year toka zilipopanda mwanzo, hii ni ajabu na tusi kwa raia wa hii nchi.

Kuna wajanja wanamchezea sana huyu kiongozi aliyepo, wamemkamata akili hafurukuti kabisa.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Yeye mwenyewe hana hamu
 
Huu ndio Ukweli unaofichwa , huyu aliyepo hana uwezo wa kupambana Jukwaani (Chama chake kinajua) , hata hivyo alishawahi kukiri mwenyewe hadharani , ikaandikwa na gazeti la Chama chake , ili kuondoa Taharuki ikakanushwa , hata hivyo awali ni awali , na wala hakuna awali mbaya , sisi tumeshika lile neno la mwanzo tu .

Baada ya Makada kutambua kwamba nafasi ya Urais ya Chama chao iko wazi wameanza kuparurana , unaambiwa hali ni mbaya kiasi cha kufikia kulogana , Yale aliyoyasema Kikwete kwamba wanaccm hawaachiani maji ya kunywa mezani yamerejea kwa kishindo .

Lakini katika hawa wanaccm mnaowaona leo yuko hata mwenye uwezo wa kuwa Rais wa Nchi ? Watoto wa viongozi waliotegemewa kupewa nafasi hiyo kama Urithi wa Wazazi wao wote wameboronga , hawavutii na hawatamaniki , watu wameshika mafaili yao zikiwemo idadi za nyumba zao ndogo za kimagumashi , wakthubutu kutangaza nia tu Mkeka unaanikwa ! hakuna hata mmoja wao anayeweza kupambana na Wapinzani Jukwaani , Ni nani atayeweza kupangua hoja za Chadema Majukwaani ?

Taarifa zinadokeza kwamba hata matumizi ya dola ili kuibeba ccm hata kwa wizi yamefifia mno , hii ni kwa sababu mashinikizo ya watoa hela kutoka Ulaya na Marekani kutaka Wakurugenzi wa Halmashauri na Polisi wasiguse karatasi ya kura ni makubwa mno na yanamaanisha hasa ( Mbeleko imetoboka )

Hali ni mbaya kuliko mnavyofahamu , muda si mrefu mtaanza kusikia makubwa zaidi

Tuendelee kutega sikio

View attachment 2830279
Inawezekana ulichoongea kuhusu CCM ni kweli ila so far hakuna mbadala wa CCM kwa upinzani huu.
 
Kwanza kabisa naamini hata wewe mwenyewe unafahamu kuwa ulichoandika ni uongo mtupu usio na ukweli wa aina yoyote ile.

Pili napenda kukwambia kuwa mgombea wa CCM Ni Rais Dkt Samia Suluhu Hasssan.huyo ndiye chaguo la wana CCM na kiu ya watanzania.hivyo ni lazima CCM iwapelekee Watanzania chaguo lao na hitaji lako ili kukata kiu yao kubwa waliyo nayo ya kuhitaji utumishi wa Rais samia kwa awamu nyingine tena ,baada ya kukoshwa na kuvutiwa na uchapa kazi wake uliotukuka uliyogusa maisha ya mamilioni ya watanzania na kuleta Tabasamu na matumaini katika mioyo ya watanzania.

Tatu ndani ya CCM Hakuna migogoro wala mivutano,.chama ni kimoja ,wana CCM Ni wamoja na sote tunasonga mbele kwa pamoja.ndio maana mambo yanakwenda na ilani Inaendelea kutekelezwa kwa kasi ya mshale.

Nne ni kuwa CHADEMA haina mtu wala kiongozi wala mgombea mwenye uwezo wa kushindana na Rais samia jukwaani na katika sanduku la kura. Ni nani kutoka CHADEMA mwenye ubavu wa kusimama na Rais samia?

CHADEMA ni saccos tu au mradi binafsi wa familia kujipatia kipato cha kuendeshea maisha na ndio maana mwaka 2015 mbowe aliamua akodishe chama chake hicho cha CHADEMA ili atunishe akaunti yake na hakumfanya chochote wala kumuhoji wala kuinua midomo yenu ,maana anawajua akili zenu ni kama manyumbu na hamna Chenu ndani ya Sacco's yake hiyo.

Kwaajili yako hiyo hiyo ya kuvukia barabara unafirikiri mtanzania yupi mwenye akili Timamu anayeweza wapa kura yake ya urais enyi wasaka tonge wa CHADEMA mnaofanya kazi ya kujaza matumbo yenu kwa Ruzuku za chama na michango ya walalahoi mliowafanya kama mahayawani?

Chama mmeshindwa kujenga hata ofisi? Mmeshindwa hata kumiliki Tv tu kwaajili ya kueneza sera zenu japo hamna? Sasa nani wa kuwapa kura yake? Si ni ninyi mlitafuna pesa za sabodo bila huruma? Zipo wapi pesa za join the chain? Zilipatikana kiasi gani? Zilifanya kazi gani?

Ninyi ni madalali wa kisiasa na mnaofanya ujasiriasiasa. Ndio maana kila senti utakayokatisha mbele ya chama Chenu lazima muilambe bila kuacha alama.
 
Lakini katika hawa wanaccm mnaowaona leo yuko hata mwenye uwezo wa kuwa Rais wa Nchi ? waliotegemewa kupewa nafasi hiyo wote wameboronga , hawavutii na hawatamaniki , hakuna hata mmoja wao anayeweza kupambana na Wapinzani Jukwaani , Ni nani atayeweza kupangua hoja za Chadema Majukwaani ?

Hali ni mbaya kuliko mnavyofahamu , muda si mrefu mtaanza kusikia makubwa zaidi

Tuendelee kutega sikio
Sii kweli kuwa CCM haina mgombea wa urais 2025, mgombea urais wa JMT 2025 ni mmoja tuu, Samia, ila kufuatia hoja hii, anaweza akaomba kupumzika!, CCM kuna a pool of 100 able people wa kuchukua urais!.

Ila pia suppose usemayo ni kweli, kuna mtu gani Chadema wa kumpa Ikulu yetu, na hata chama, kuna chama gani cha kuipa ikulu yetu, na kama ni Chadema, ni Chadema ipi?

Chadema bado sana!.

P
 
Back
Top Bottom