Kalunguine
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 2,543
- 134
Magazeti ya leo yameandika kuwa Sumari ana asili ya kenya so anatakiwa ajieleze.Kugombea kupitia CCM kuna hitaji moyo mgumu.
Ha ha haaa!! Mkuu umenifurahisha sana. Tupinge kwa nguvu zetu zote Wakenya kugombea uongozi hapa Bongo!Haturuhusu Wakenya kugombea nafasi ya uongoza hapa bongo
Wanajamvi! Mh. Spika kasema kweli kuwa magazeti ya leo ndo yameandika kuwa Sioi sio raia wa Bongo kwani alizaliwa Kenya! Kwa hilo sibishi ila naomba nami niulize swali! Je kama mama kaenda kutibiwa India (kama kawaida ya viongozi) kisha akajifungua mtoto huko huyo mtoto atakuwa raia wa India?! Wanajamvi nisaidieni!
yaani hata awekwe nani CCM hawawezi kushinda ARUMERU....
CCM yataka kumtosa mtoto wa Sumari Arumeru. |
Mkuu Pasco ni jana tu ulitudhihirishia kuwa Sioi atakuwa mgombea na atashinda inakuwaje tena, halafu ile plan A yetu ya washili itakuwaje au William naye ni mshili.Hata mimi nimeishtukia, hii ni habari njema kwani hivi ni vita vya panzi!. Kiukweli tukubali tukatae, angesimama Sioi, Chadema ingekuwa na kazi ya ziada!. Akipitishwa mwingine yoyote ni ushindi wa kiulani kama kumsukuma mlevi!.
Feedback, japo sina chama na Chadema naikubali sana tuu, ila kwenye uchaguzi wa Arumeru, nasimama na Sioi na machalii wote wa AR wako nyuma yake!. Asipopitishwa na CC leo, ile kambi yote ya Sioi, watashiriki kampeni za CCM, ila kura Chadema!. Kiuhakika bila Sioi, CCM itaangukia pua!.Mkuu Pasco ni jana tu ulitudhihirishia kuwa Sioi atakuwa mgombea na atashinda inakuwaje tena, halafu ile plan A yetu ya washili itakuwaje au William naye ni mshili.
Nakukumbusha tu tamko la UVCCM-Arumeru kuwa kamati kuu isiporudisha jina la Sioi na wao watakuwa na mgombea wao.
Sasa kama hatapitishwa kwa kigezo cha uraia watamwombaje raia wa kigeni (Kenya) awasaidie kampeni. Kuhusu ushindi wa Chadema hiyo haina mjadala nilishasema hata waunganishe majina Sioi na William waitwe Siwi CCM itashindwa tu, ngoja niseme msemo wa Nape kwa jimbo la Arumeru Mashariki CCM mnalo.Feedback, japo sina chama na Chadema naikubali sana tuu, ila kwenye uchaguzi wa Arumeru, nasimama na Sioi na machalii wote wa AR wako nyuma yake!. Asipopitishwa na CC leo, ile kambi yote ya Sioi, watashiriki kampeni za CCM, ila kura Chadema!. Kiuhakika bila Sioi, CCM itaangukia pua!.
Igunga RA ni muoga kama kunguru siku za mwisho alijitokeza kuokoa jahazi, Sioi asipopitishwa Mmeru No. 1 hatatia mguu Arumeru!, CCM ni kifo cha mende straight away!.
Kamati kuu ya CCM ndio inaitwa NEC!!?? na sio CC!!??Inasemekana mchakato ni mkali ndani ya kikao kinachoendelea cha nec ya ccm na asilimia kubwa hawamtaki SIOI kwa kua ushindi wake wa uteuzi uligubikwa pia na rushwa,ngoja tuendelee kufatilia na yeyote atakaye pata taarifa aziweke hapa!!