Upungufu wa maua jike-Kilimo cha tikiti maji

ASHA NGEDELE

JF-Expert Member
Jul 5, 2011
784
326
Habari wakulima wenzangu,

Nimelima tikiti ekari mbili na linaendelea vizuri kwani halina ugonjwa wowote mpaka leo siku ya 34 tokea mbegu kupasuka.

Changomoto nayoipata kwa sasa ni mmea kuzalisha maua mengi sana lakini maua dume kwahio mpaka sasa matunda yalozalishwa ni machache sana. Hali ikiendelea namna hii naona hasara kubwa sana huko mbeleni. Wiki mbili zilizopita nlitumia mbolea ya Yara Nitrabor na kesho natarajia kutumia tena mbolea hio hio 10gm kila mche. Mbolea ya majani natumia Di-Grow pekee. Maji huwa naruka siku moja lakin nimeshauliwa nipige kila siku sababu kwa sasa jua ni kali sana na nalimia eneo la Kichanga sana.

Je,

1. Nifanye nini cha ziada ili nipate maua jike mengi ili matunda yazalishwe kwa wingi?

2. Matunda yakianza kutoka kwa wingi mfano siku ya 40, na kwa kawaida mbegu nayotumia matunda huwa yanakomaa kuanzia siku ya 60, hizi siku 20 zitatosha kweli matunda kunenepa na kuwa makubwa ambayo yatanipatia faida Sokoni? Au yatakomaa yakiwa na umbo dogo?

Asante
 
Habari wakulima wenzangu,

Nimelima tikiti ekari mbili na linaendelea vizuri kwani halina ugonjwa wowote mpaka leo siku ya 34 tokea mbegu kupasuka.

Changomoto nayoipata kwa sasa ni mmea kuzalisha maua mengi sana lakini maua dume kwahio mpaka sasa matunda yalozalishwa ni machache sana. Hali Duh
 
Kwanz unalijua ua jike?kama hulifahamu basi lazima ulijue kusema hayapo kumbe shida ni uchavishaji mdogo.Kwenye kilimo cha tikiti wadudu wachavishaji km nyuki ni muhimu sana vinginevyo utapata mtunda machache na mengine shape zake zitakuwa za ajabu.


Kuhusu mbolea mshauri wako simjui

Upigaji wa dawa kuwa makini kuna mda wadudu wachavishaji wanaweza kufa sababu ya dawa zako
 
Duh - hamna kabisa wakulima ambao wana utalaamu na uzoefu wa tikiti humu?
Mkuu Tatizo ni uchavushaji wadudu hasa nyuki ni wachache shambani au unawakimbiza mwenyewe.

Kipindi cha maua jihadhari sana kupiga dawa wakati wa asubuhi na mchana, kwa muda huo ndio muda hasa wa nyuki kufanya kazi yao.

Dawa ipigwe jioni kabisaaa, ili kuto wakimbiza nyuki.
 
Kwanz unalijua ua jike?kama hulifahamu basi lazima ulijue kusema hayapo kumbe shida ni uchavishaji mdogo.Kwenye kilimo cha tikiti wadudu wachavishaji km nyuki ni muhimu sana vinginevyo utapata mtunda machache na mengine shape zake zitakuwa za ajabu.


Kuhusu mbolea mshauri wako simjui

Upigaji wa dawa kuwa makini kuna mda wadudu wachavishaji wanaweza kufa sababu ya dawa zako
Sahihii kabisa
 
Siku 20 Zina tosha kabisa kunenepesha tikiti.

Mimi nalima hizo kitu. Niko buyuni kigamboni
 
Asha ngedere Mwajuma Ndalandefu hajambo! Pole sana, mimea uliichanganya kwa kuzidisha mbolea, ulipaswa kuweka nitrabor mara 1-2, basi, mbolea tosha, booster ya majani ni mara 1 after 2wks au 21 days..

Mbolea ikizidi mmea unafocus kukua na siyo kuzaa.

Ulifanikiwa kuvuna??

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Back
Top Bottom