Habari wanajamii?
Natumaini tuko byee kabisa tukisukuma gurudumu la maendeleo kuelekea nchi ya asali na maziwa.
Ni hivi nimepata skolashipu ya kutokea chuo kimoja kinaitwa Vanderbilt University kiko hapo Nashville, Tennessee. Kama kawaida kuwa mbali na nyumbani huwa ni vizuri kuwa karibu na wa nyumbani. Lakini basi kama ambavyo ili upate unga unasaga nafaka nami ili nipate watanzania wanaoishi huko inabidi nije mahali kama hapa.
Kwa kifupi ningependa kama kuna watanzania wanaopatikana hapo Nashville basi sio vibaya kufahamiana. Kama kuna mkuu yeyote anayesoma huu ujumbe unaweza kutupa uzoefu na kuja inbox ukipenda.
Natanguliza shukrani nyingi sana.
Natumaini tuko byee kabisa tukisukuma gurudumu la maendeleo kuelekea nchi ya asali na maziwa.
Ni hivi nimepata skolashipu ya kutokea chuo kimoja kinaitwa Vanderbilt University kiko hapo Nashville, Tennessee. Kama kawaida kuwa mbali na nyumbani huwa ni vizuri kuwa karibu na wa nyumbani. Lakini basi kama ambavyo ili upate unga unasaga nafaka nami ili nipate watanzania wanaoishi huko inabidi nije mahali kama hapa.
Kwa kifupi ningependa kama kuna watanzania wanaopatikana hapo Nashville basi sio vibaya kufahamiana. Kama kuna mkuu yeyote anayesoma huu ujumbe unaweza kutupa uzoefu na kuja inbox ukipenda.
Natanguliza shukrani nyingi sana.
