Uncle Jei Jei
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 1,684
- 2,156
Sina mengine zaidi ya hayo, heading inajieleza vizuri.
Ni kweli mtakosa mapato, lakini mnaweza kujibidisha na kupata shughuli nyingine hata ikiwezekana kilimo.
Tuachieni hii miaka mitano ili tujionee wenyewe.
Msihangaike kwenda mahakamani maana huko mtapoteza fedha na muda wenu bure.
Msihangaike kuhamasisha maandamano maana police wakifyatua risasi na raia wakafa, mtalaumiwa bure!
Tuachieni miaka hii mitano tujihakikishie Kama kweli maana ya upinzani ipo kwenye vyama vya siasa au mioyoni mwa watu?
Kaeni pembeni tuone Kama kweli nyie ndio chanzo cha kukosekana kwa huduma za jamii huku kwetu?
Kaeni pembeni tuone Kama kweli nyie ndo mlikuwa sababu ya umasikini wa Watanzania wengi?
Kaeni pembeni ili wananchi waanze kufurahia maziwa na asali walivyovikosa miaka yote hiyo.
Nasema kaeni pembeni kwasababu mmejaribu kutusemea ila tumeshindwa kuwaelewa.
Haina haja ya Mmarekani na wa yuropa kuanza kutusemea! Waambieni nao watuache, tuna jambo letu miaka mitano hii.
Tena waambieni wawe wa kwanza kumpa kongole muheshimiwa kwa ushindi wake wa kishindo na madiwani na wabunge wote! Wasimseme wasije kumconfusi!
Kwa kweli mkijikalia pembeni mkaanza kufanya shughuli nyingine nje ya siasa kuanzia Leo mtakuwa mmetusaidia sana sisi wanyonge kuondoka kwenye unyonge wetu.
Mtakuwa mmetusaidia sana maana mishahara itapanda, huduma za jamii zitabireshwa, ajira zitapatikana, shule zitaboreshwa, uhuru na haki vitatamalaki na Mambo kede kede.
Msiandamane wala kulalamika lalamika ili msimconfyuzi mshindi akaanza kuloose focus na kugombana na nyie!
Muacheni na mtuache na sisi tuyaone wenyewe!
Ni hayo tu! Tanzania ni yetu watanzania, UN, USA na wengine hawawezi kutuonea huruma tusipoanza sisi kujionea huruma na hata wakituonea huruma watakuwa na jambo lao nyuma ya pazia!
Waambieni watuache tuyaone wenyewe!
Ni kweli mtakosa mapato, lakini mnaweza kujibidisha na kupata shughuli nyingine hata ikiwezekana kilimo.
Tuachieni hii miaka mitano ili tujionee wenyewe.
Msihangaike kwenda mahakamani maana huko mtapoteza fedha na muda wenu bure.
Msihangaike kuhamasisha maandamano maana police wakifyatua risasi na raia wakafa, mtalaumiwa bure!
Tuachieni miaka hii mitano tujihakikishie Kama kweli maana ya upinzani ipo kwenye vyama vya siasa au mioyoni mwa watu?
Kaeni pembeni tuone Kama kweli nyie ndio chanzo cha kukosekana kwa huduma za jamii huku kwetu?
Kaeni pembeni tuone Kama kweli nyie ndo mlikuwa sababu ya umasikini wa Watanzania wengi?
Kaeni pembeni ili wananchi waanze kufurahia maziwa na asali walivyovikosa miaka yote hiyo.
Nasema kaeni pembeni kwasababu mmejaribu kutusemea ila tumeshindwa kuwaelewa.
Haina haja ya Mmarekani na wa yuropa kuanza kutusemea! Waambieni nao watuache, tuna jambo letu miaka mitano hii.
Tena waambieni wawe wa kwanza kumpa kongole muheshimiwa kwa ushindi wake wa kishindo na madiwani na wabunge wote! Wasimseme wasije kumconfusi!
Kwa kweli mkijikalia pembeni mkaanza kufanya shughuli nyingine nje ya siasa kuanzia Leo mtakuwa mmetusaidia sana sisi wanyonge kuondoka kwenye unyonge wetu.
Mtakuwa mmetusaidia sana maana mishahara itapanda, huduma za jamii zitabireshwa, ajira zitapatikana, shule zitaboreshwa, uhuru na haki vitatamalaki na Mambo kede kede.
Msiandamane wala kulalamika lalamika ili msimconfyuzi mshindi akaanza kuloose focus na kugombana na nyie!
Muacheni na mtuache na sisi tuyaone wenyewe!
Ni hayo tu! Tanzania ni yetu watanzania, UN, USA na wengine hawawezi kutuonea huruma tusipoanza sisi kujionea huruma na hata wakituonea huruma watakuwa na jambo lao nyuma ya pazia!
Waambieni watuache tuyaone wenyewe!