GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,689
- 109,117
Sijaona bado ulazima huo wa kujihangaisha kwenda kileleni Mlima Kilimanjaro na kuzindua jezi zetu Simba SC ili tu kufunika tukio la Yanga SC la wao kuzindua zao Ikulu ya Malawi mbele ya Marais wawili wa Malawi na Tanzania.
Na si lazima kila Yanga SC ikija na kitu kipya cha ubunifu basi na sisi Simba SC tuanze kulazimika kutafuta tukio la kuwafunika Yanga SC na tuzungumzwe Simba SC tu.
Haya tumejipanga na hadi kutangaza kuwa Jezi zetu Simba SC tunaenda kuzindulia kileleni Mlima Kilimanjaro na tukio kuwa televised na Azam TV. Je, ikitokea siku hiyo hali ya hewa ya huko Mlimani ikabadilika na kuwa mbaya au si rafiki hizo jezi zetu tutazindundulia wapi?
GENTAMIYCINE naheshimu mno ubunifu wa matukio mbalimbali ya Simba SC na napenda kuona ubunifu zaidi ila sipendi ubunifu wa kishamba, kienyeji na wenye mhemko. Kwani mnaweza kudhani mnaing'arisha Simba SC kimatukio, kumbe ndiyo mkawa mnatuanika wana Simba SC wote (GENTAMIYCINE nikiwemo) kuwa ni 'mapimbi' kweli kweli na tukaanza kuchekwa na watani zetu Yanga SC.
Na nimetoka kutizama weather forecast ya Ijumaa ijayo, siku ya tukio itakuwa ni baridi kali na mawingu kule kileleni hivyo naona kabisa kama Msemaji wetu Simba SC Ahmed Ally ndiyo atapanda kule juu na jezi zetu mpya anaweza asirejee mazima, huku camera man wa Azam TV nae Pumu (Asthma) ya ghafla kumkamata na kushindwa kuchukua matukio yote muhimu.
Na si lazima kila Yanga SC ikija na kitu kipya cha ubunifu basi na sisi Simba SC tuanze kulazimika kutafuta tukio la kuwafunika Yanga SC na tuzungumzwe Simba SC tu.
Haya tumejipanga na hadi kutangaza kuwa Jezi zetu Simba SC tunaenda kuzindulia kileleni Mlima Kilimanjaro na tukio kuwa televised na Azam TV. Je, ikitokea siku hiyo hali ya hewa ya huko Mlimani ikabadilika na kuwa mbaya au si rafiki hizo jezi zetu tutazindundulia wapi?
GENTAMIYCINE naheshimu mno ubunifu wa matukio mbalimbali ya Simba SC na napenda kuona ubunifu zaidi ila sipendi ubunifu wa kishamba, kienyeji na wenye mhemko. Kwani mnaweza kudhani mnaing'arisha Simba SC kimatukio, kumbe ndiyo mkawa mnatuanika wana Simba SC wote (GENTAMIYCINE nikiwemo) kuwa ni 'mapimbi' kweli kweli na tukaanza kuchekwa na watani zetu Yanga SC.
Na nimetoka kutizama weather forecast ya Ijumaa ijayo, siku ya tukio itakuwa ni baridi kali na mawingu kule kileleni hivyo naona kabisa kama Msemaji wetu Simba SC Ahmed Ally ndiyo atapanda kule juu na jezi zetu mpya anaweza asirejee mazima, huku camera man wa Azam TV nae Pumu (Asthma) ya ghafla kumkamata na kushindwa kuchukua matukio yote muhimu.