Updates: Mvua Dar leo tarehe 23/04/15

Updates: Mvua Dar leo tarehe 23/04/15

DAKA MTUMBA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2014
Posts
1,288
Reaction score
805
Wakuu tupeane updates za mvua hapa jijini Dar na athari zake.

Huku maeneo ya Ukonga sijapata taarifa yoyote mbaya,pia hakuna tatizo la msongamano mkubwa wa magari kwa muda huu.

Maeneo ya Kipunguni "A" kituo cha bonanza nasikia kuna gari imegonga mti baada ya kuteleza.

Barabara ya kinyerezi sijapata updates zozote,maeneo ya gongo la mboto ulongoni kwa kina(Jot wa ze Commedy)nasikia hali si shwari sana maana kuna mtu wa maji mkubwa uliopasua kutafuta njia ili kuelekea mto msimbazi.

Kitunda pako poa.

Ntaendelea kuwajuza kila ntakapopata taarifa mpya hasa upande huu wa UK.

Mlioko katikati ya jiji na pembezoni pia tupeni taarifa ili kuwazaidia wadau na wapita njia ili kujihami na hadha ya mvua.
 
DAKA MTUMBA

mimi binafsi nakushukuru na kukupongeza kwa kujituma.
Kama wewe ni kijana, basi this can be a very good business idea. hongera
 
Last edited by a moderator:
Updates:maeneo ya vingunguti mji mpya kama unatokea buguruni kwa mnyamani kuingilia kwenye reli upande wa kulia kwenye mji mpya huko nasikia ni shida ata Pikpik haiendi maana kuna utelezi mkubwa na madimbwi,so mnao kaa mitaa hiyo kama ukichukua Pikpik basi tambua kwamba huko hakupitiki na mwisho ni relini.........
 
Wabongo sie badao sana yaani mtu anajitolea kukupa tu hali halisi ilivyo hasa kwa siku kama hii na Mafoleni yetu ya Dar mna m crash??Hivi kweli?kwa wenzetu hali ya hewa ni kitu muhimu sana tena kabla hujatoka sehemu ulipo...Big up mtoa uzi umeandika jambo la maana sana
 
Achana nao.... hao ni watu tu.Maeneo ya Tabata imepiga ile mbaya..hali ni shwari sasa hakuna mafuriko.Foleni mbaya toka buguruni kwenda Tabata....barabara ya vingunguti ina tope na utelezi..chukuwa tahadhari.
 
Jamani sisi tupo safarini tunakuja Dar natunaenda maeneo ya kwa Azizi Ally,tuna gari ndogo toyota na lengo letu tuingilie pale mbezi tutokee kinyerezi-majumba6-nyerere road,jee pako salama?
tunaomba msaada wakuu maana safari ni ndefu na foleni ya kimara kisha buguruni mbona tutakoma!!
 
Jamani sisi tupo safarini tunakuja Dar natunaenda maeneo ya kwa Azizi Ally,tuna gari ndogo toyota na lengo letu tuingilie pale mbezi tutokee kinyerezi-majumba6-nyerere road,jee pako salama?
tunaomba msaada wakuu maana safari ni ndefu na foleni ya kimara kisha buguruni mbona tutakoma!!
Mkuu hiyo njia ya mbezi-kinyerezi-majumba6 haifai.
Maana mbezi-kinyerezi hakuna rami so nasikia kuna tope jingi na gari zina teleza sana,so endelea na morogoro rd kisha kama mandera rd tembea.Othereise uwe na 4WD car ingawa bado ni tabu sana mkuu!!
 
Mkuu hiyo njia ya mbezi-kinyerezi-majumba6 haifai.
Maana mbezi-kinyerezi hakuna rami so nasikia kuna tope jingi na gari zina teleza sana,so endelea na morogoro rd kisha kama mandera rd tembea.Othereise uwe na 4WD car ingawa bado ni tabu sana mkuu!!

Ahsante mkuu ubarikiwe sana kwa msaada wako.
Ngoja tuongeze mafuta kabisa tusije hadhirika kwenye foleni.
 
Jamaa kafanya kitu kikubwa sana.Maana mie binafsi nilikua sijui kama dar kuna mvua na nilitaka kupita njia ya kinyerezi na jamaa kasema njia hiyo haipitiki kutokana na mvua.
 
Tahadhari.
Maeneo ya UK-Gomz-Chanika-Masaki-Mvuti-Dondwe mvua imeanza upya so kwa mlioko mbali na ni wakazi wa maeneo hayo wahini majumbani kwenu.......
 
Mkuu hiyo njia ya mbezi-kinyerezi-majumba6 haifai.
Maana mbezi-kinyerezi hakuna rami so nasikia kuna tope jingi na gari zina teleza sana,so endelea na morogoro rd kisha kama mandera rd tembea.Othereise uwe na 4WD car ingawa bado ni tabu sana mkuu!!

Anaweza pita. Matope yaliyopo ni yakuchafua gari tu lakini gari hazikwami.
 
Back
Top Bottom