Mediocrist
JF-Expert Member
- Jan 27, 2015
- 1,709
- 993
Pole sana mkuu ila ni moja katika njia za kutafuta hili nalo litapita mkuu kesho yetu itakuwa vizuri naamini maana katika hii dunia kila mtu ridhiki yake huja kwa wakati wake hasara ni moja ya mapito ya opportunist hata uki invest lazima ukubali hasara pia bila kuwa unaangalia faida tu pekee.Mkuu hawa jamaa imebidi tu tuwafate mguu kwa mguu kujua zaidi juu ya kile kilichotokea. Majibu yao ni kwamba nafasi 11 zilizotangazwa zilitangazwa kimakosa na walifanya marekebisho ikawa nafasi 1 badala ya 11. Kwa hiyo selection ya watu 4 wenye ufaulu wa alama 90 na 80 umezingatia uwiano wa nafasi moja tu. Tuliendelea kuwauliza kuwa kama mlifanya marekebisho ya nafasi kutoka 11 hadi 1 kwa nini walishindwa kuujulisha umma, hapo walikosa majibu sahihi badala yake waliendelea kutuomba tu samahani kwa kusema makosa yametendeka kwa kushindwa kuujulisha umma kwa Wakati.
Badala ya majibu hayo sisi tuliondoka kwa kushukuru tu kwa yote yaliyotokea. Kwa sasa tunajiandaa na maandalizi ya kurudi mikoani tulikotoka tukaendelee na harakati za kutafuta riziki. Bado naamini Kesho yetu ni kubwa sana pia nimejifunza jambo kutokana na kilichotokea bila kuangalia HASARA tulioingia mifukoni.