UPDATE: Vifo vya Ajali Ngaramtoni vyafikia 25

duh !

‎na hapo ukisikia 25 ni idadi inatangaza serikali ili kupunguza tu taharuki ila uhalisia hapo ni majanga makubwa sana.

‎nadhani waliokua eneo la tukio ndio wanaujua ukweli.

‎ila yote kwa yote

‎إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّآ إِلَيْهِ رَٰجِعُونَ
 
Write your reply...hii ajali ina watu wa kuwajibishwa, ni wale walioruhusu gari hiyo kutembea bila Kuwa na kile kigari hutangulia mbele kwa ajili ya usalama
Kile kigarii kwa maeneo ya mjini naonaga hakina kazi unakuta kimetangulia mbele kabisa katikati yake na gari la mizigo kuna gari kibaooo.. Na kile hakizuii gari la mizigo lisifail brake ila kutoa tahadhari tuu kuwa gari linalokuja size yake limezidi upana wa kawaida wa gari.
 
Kusema ni Tukio la kigaid si rahisi, unatakiw ufanye reasoning.. hilo ni lori na ametoka huko alikotoka, kakoleza speed, pia alikuwa anaonesha ISHARA ya kusogeza gar pembeni ila watu hawakumuelewa anamaanisha nini.

Inasemekana gari imefel kilometa 3 nyuma.. so kulikuw na warning signs kazionyesha.

Tukio la kigaidi huwez kubet kias hicho kwamba gar fulan itakuw point fulani.. without gari nyingine kuingilia kati kwa distance ya km3.

Yaan umuweke TARGET wako ukiwa km3 uje umgonge sio rahisi.
Hilo gari lingeingia mitaa ya idd yangetokea makubwa zaidi ya hayo
 
Hilo gari lingeingia mitaa ya idd yangetokea makubwa zaidi ya hayo
Leo nimepiga makofi Dereva wa hivi vipanya, nikachukua na funguo mpumbav kabisa.

Kapaki katikati ya barabara et anasubiri abiria mmoja ajazilizie. Kaweka folen ya gari kama 5 na wala hajishtukii.

Nafkir Serikali iangalie sana hawa madereva wa hizi daladala.. akili zao sio nzuri.

Hasa ARUSHA kuna shida sana.
 
Habari wadau

Nipeni muda kidogo nitawajuza uharibifu ni wa kiwango gani lakini ukweli ni kwamba hali ni mbaya sana, watu wengi wamefariki.

Kwa wasiojua Ngaramtoni ni Arusha, Nairobi Road.

Kwa kifupi ni kwamba imeua wazungu wengi sana. Walikuwa kwenye Coaster pamoja na Raia na waendeshaji wa hiyo Truck pia.

=============

Watu 15 wameripotiwa kufariki dunia katika ajali iliyohusisha Lori la Mizigo (Semi Trailer) na magari madogo matatu iliyotokea katika eneo la By Pass Ngaramtoni, Wilayani Arumeru ambapo chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika.

Kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda, Lori hilo aina ya Scania lenye namba za Usajili ZF 6778 lilikuwa likionesha ishara Taa za Hatari likiwa katika mwendo mkali na baadaye kuyagonga magari matatu ambayo ni Basi dogo la Abiria (Hiace), Basi la Shule ya New Vision lililokuwa na Watumishi wa Shule na Gari lingine dogo.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP, Justine Masejo, amethibitisha taarifa hiyo na kuwataka Wananchi kufika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru kutambua Miili ya waliofariki katika ajali hiyo.

...............

UPDATE:

ARUSHA: Idadi ya Vifo kutokana na ajali iliyotokea Februari 24 eneo la Ngaramtoni na kuhusisha Lori na magari mengine madogo Matatu imefikia 25 huku wengine 21 wakijeruhiwa

Tumeskia wazungu nao pia walikuwepo

Tupe taarifa ya wazungu waliofarik
 
Nikisema Ile ajali ni mtu alijitoa mhanga Nitakuwa nimekosea?
Kwa vile kama alikuwa ni Dereva ilikuwa haina sababu kufika pale ajali ilipotokea. Yalikuwepo maeneo mengi nyuma ya kuiingia shambani Ikawa salama na Isilete madhara yeyote. Mimi kama Dereva wa mda mrefu nadhubutu kusema lile ni shambulio
Ingawa Tanzania unadhani shambulio NI visu na risasi. Mwenye akili ananielewa Asante.

Sisikii Police anayeongelea uzembe wa Ile Gari yenye mzigo kama ule kutembea bila escorts
Siku zote tulikuwa tunaona haya magari yakitanguliwa na Gari inayotoa utambulisho wa kinachokuja nyuma.
Hao police walikuwa Barabarani siku hiyo Kutokea Namanga hadi NGARAMTONI wanaweza kutueleza nini mfano

Tukisema huyu Dereva alivinunua vyombo vya usalama Barabarani tutakuwa tumekosea?

There is something wrong ???????
 
Habari wadau

Nipeni muda kidogo nitawajuza uharibifu ni wa kiwango gani lakini ukweli ni kwamba hali ni mbaya sana, watu wengi wamefariki.

Kwa wasiojua Ngaramtoni ni Arusha, Nairobi Road.

Kwa kifupi ni kwamba imeua wazungu wengi sana. Walikuwa kwenye Coaster pamoja na Raia na waendeshaji wa hiyo Truck pia.

=============

Watu 15 wameripotiwa kufariki dunia katika ajali iliyohusisha Lori la Mizigo (Semi Trailer) na magari madogo matatu iliyotokea katika eneo la By Pass Ngaramtoni, Wilayani Arumeru ambapo chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika.

Kwa mujibu wa taarifa za mashuhuda, Lori hilo aina ya Scania lenye namba za Usajili ZF 6778 lilikuwa likionesha ishara Taa za Hatari likiwa katika mwendo mkali na baadaye kuyagonga magari matatu ambayo ni Basi dogo la Abiria (Hiace), Basi la Shule ya New Vision lililokuwa na Watumishi wa Shule na Gari lingine dogo.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP, Justine Masejo, amethibitisha taarifa hiyo na kuwataka Wananchi kufika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru kutambua Miili ya waliofariki katika ajali hiyo.

...............

UPDATE:

ARUSHA: Idadi ya Vifo kutokana na ajali iliyotokea Februari 24 eneo la Ngaramtoni na kuhusisha Lori na magari mengine madogo Matatu imefikia 25 huku wengine 21 wakijeruhiwa

Nilipoona tu Timu moja Kongwe barani Afrika imepata Ushindi mnono na wa Kuwavusha hatua muhimu ya Mashindano kama walivyokamia nilijua tu kuwa kutakuwa na Malipo makubwa ya Kafara ili Kuyalipa / Kuyashibisha Majini ambayo hata Mtu wao aliyeko Misri kayasema.
 
Nilipoona tu Timu moja Kongwe barani Afrika imepata Ushindi mnono na wa Kuwavusha hatua muhimu ya Mashindano kama walivyokamia nilijua tu kuwa kutakuwa na Malipo makubwa ya Kafara ili Kuyalipa / Kuyashibisha Majini ambayo hata Mtu wao aliyeko Misri kayasema.
Hadi vifo hua unasafiria umaarufu ..jingamavi kweli
 
Back
Top Bottom