Hallow, Great thinkers!!!!
Pamoja lawama na takataka zote anazotupiwa Edward Lowassa. Pamoja na mabaya yote aliyonayo Edward Lowassa kama mimi na wewe tulivyo na mabaya yetu, tutakuwa hatumtendei haki Edward Lowassa kama tusipo yatangaza mazuri yake.
Kwangu mimi, Edward Lowassa namuona kama
1. kiongozi bora na anayeweza kusimamia maamuzi yake
2. Kiongozi ambaye yupo tayari kuchukua maamuzi mazito hata kama yataudhi wengi ilimradi yana maslaha kwa taifa
3. Kiongozi ambaye anaweza kulifikisha taifa pale tunapohitaji
Baadhi ya mambo makubwa ambayo huwezi kuyataja bila kumtaja Edward Lowassa ni Uthubutu wake wa kuuvunja mkataba kati ya serikali na city water. Ni yeye aliyeasisi na kusimamia mradi wa shule za kata, though hazifanyi vizuri. Ni Edward Lowassa angalau alionesha nia ya kuleta mvua artificial na ninaamini kama Lowassa angeendelea kuwa PM leo hii uwajibikaji serikalini ungekuwa na mkubwa sana.
Nimegusa tu mazuri ya Laigwanani Lowassa, mazuri yapi ya Lowassa unayajua? Yaandike hapa
Sina tatizo na namba moja hapo juu, tatizo langu linaanzia namba mbili pale uliposema "ilimradi yana maslaha kwa taifa" hapo nina tatizo kidogo. ukiangalia tokea huko nyuma alipokuwa anasimamia kitengo cha maafa na kujinufaisha (maslahi binafsi - hapo simtofautishi na mtu anayewakwapua majeruhi wa ajali) na alipokuwa waziri mwenye dhamana ya nyumba na ardhi - madudu aliyofanya, kwa kifupi tumwamini Nyerere aliyemwona moja kwa moja kwamba hafai uongozi ngazi ya juu. anachapa kazi kweli, lakini kuelekea wapi?
Tuangalie hili la shule za kata. sikatai kwamba mapinduzi yanahitaji nguvu kubwa, lakini kitu chochote katika ngazi hiyo kinahitaji umakini wa hali ya juu. maslahi ya taifa yanakudai ufanye jambo jema ambalo linadumu na linahitaji muda mrefu kutekeleza. maslahi ya kweli ya taifa humgharimu yule anayeyasimamia. sifa ni mara chache kwenda kwake maana yanaweza kukamilika wakati yeye hayuko madarakani.
mkakati wa kweli wa kuinua elimu Tanzania haiwezekani utekelezwe kwa staili hii ya shule za kata. kulikuwa na shinikizo kubwa la kisiasa, na kuburuzana. huwezi kufanya jambo kubwa linalodai kushirikisha wataalamu na wadau wengine wa elimu, kwa kuwaburuza. nani atatekeleza au kusimamia utekelezaji? tunahitaji phase one, two three, inayoeleweka.
Lowasa anachapa kazi kwa msingi wa populism, kujitafutia sifa za haraka haraka kwa maslahi binafsi. tunahitaji wachapa kazi ndio, lakini si kwa staili ya Lowasa.
Hilo la tatu ndio kabisaaa, Lowasa hawezi kutufikisha pale tunapohitaji. kujiuzulu kwake kwa kashfa ni kielelezo tosha cha utendaji wake. kwa support aliyokuwa toka kwa JK, aliwezaje kudondoka? ni wazi maji yalifuata mkondo. na kashfa iliyomwangusha bado ndio kwanza inarindima, na inanuka jitihada kubwa za ngazi za juu kufunika kombe mwanaharamu apite