Upandaji wa gharama za maisha

malsa

Member
Feb 29, 2012
6
0
Habari wadau,
Nomba tuchangie hili na vipi tuta ipress serekali kuingilia kati katika biashara hii huria.
Jana nimetoka kazini nikipita sehemu kununua gas ajili ya matumizi ya nyumbani,nilinunua gas kwa tsh 52,000 na yule muuzaji akaniambia kuanzia jumatano gas itakua inauzwa tsh 58,000 roho iliniuma sana na kutamani kulia, maana maisha yanazidi kua magumu,vitu vya msingi ambazo ni basic needs zinapanda bei na serekali ipo kimya tu.mishahara ni midogo na uongezekaji kwake ni kugumu pia.Mwaka 2009 ile gas ya klo 15 ilikua inauzwa tsh 12,000 leo ni Tsh 52,000 hivi hii ni sawa kweli?Free market inapaswa kuoperate lakini katika uchumi wowote duniani hamna 100% free market cse kuna vitu vingine lazima serekali iingilie kati ili watu waweze ku afford gharama za masiha,bei ya mkaa kwa gunia sasa ni tsh 45,000. Kusema kweli maisha ni magumu sana. Nchi zilizoendelea vitu kama gas na vyakula ni rahisi sana sababu hivi ni basic lakini kwetu inakua tofauti.Jamani serekali ipo wapi,au haya ndo maisha bora kwa kila mtanzania? INAUMA NA KUTIA HASIRA.
 
Tulikuwa na nafasi ya kuleta mabadiliko, miezi kama 15 iliyopita na tukaichezea. Sasa ngoja kwanza Somo liwaingie vizuri. Anyway dawa ni rahisi sana, kwa kuwa sisi (wananchi) ndio waajiri wa serikali, basi dawa yake ni kuiondoa madarakani. Lakini wakati tunasubiri hiyo 2015 ni lazima tuwe na mipango ya muda mfupi.

Mipango hii ipo mingi sana, but nitajikita kwenye miwili tu
Njia moja wapo ni kuwasilisha malalamiko yetu kwa wabunge wetu, ili wayasemee bungeni (sijui nao bado wanasimamia maslahi yetu) na ikiwezekana wasiunge mkono budget ya serikali mpaka kodi kwenye vitu vya msingi kama hivyo itakapoondelewa kama si kupunguzwa.

Njia ya pili na rahisi zaidi ni kuingia barabarani, mpaka kieleweke. Unakumbuka, kilichotokea Zambia, kipindi mkate ulivyopanda bei? (tatizo watanzania ni watu wa ajabu sana)
 
Malsa, hebu niambie sisi tulijifunza nini kwa hawa wenzetu

Zambia, maandamano (sio ya vyama vya siasa) kupinga kupanda kwa bei ya mkate
Uganda , "walk to work"
Congo, Maandamano na Mishumaa ya usiku
Nigeria, Maandamano kupinga, ongezeko la kodi kwenye mafuta


Halafu angalia Tanzania sasa
Mgao mkuu wa umeme, watu kimyaa
Kupanda kwa bei ya mafuta (gasolin), watu kimyaa
Kupanda kwa gharama za maisha, watu kimyaa
Kupanda kwa mafuta ya taa, watu kimyaa
Kupanda kwa gharama za umeme, watu kimyaaaa
Kuporomoka kwa thaman ya shilingi watu kimyaaaa
Matumizi mabaya ya rasilimali na ufisadi watu kimyaaa

Na hapa niwashukuru CDM kwa kuonyesha njia, lakini maandamano yale yangekuwa na nguvu zaidi kama yasingekuwa na chembe ya siasa (si mnawaona MAT). Tatizo watanzania hawaoni uhusiano wa mambo haya na serikali iliyapo madarakani. Until then, mambo yatazidi kuwa magumu sana
 
Malsa, hebu niambie sisi tulijifunza nini kwa hawa wenzetu

Zambia, maandamano (sio ya vyama vya siasa) kupinga kupanda kwa bei ya mkate
Uganda , "walk to work"
Congo, Maandamano na Mishumaa ya usiku
Nigeria, Maandamano kupinga, ongezeko la kodi kwenye mafuta


Halafu angalia Tanzania sasa
Mgao mkuu wa umeme, watu kimyaa
Kupanda kwa bei ya mafuta (gasolin), watu kimyaa
Kupanda kwa gharama za maisha, watu kimyaa
Kupanda kwa mafuta ya taa, watu kimyaa
Kupanda kwa gharama za umeme, watu kimyaaaa
Kuporomoka kwa thaman ya shilingi watu kimyaaaa
Matumizi mabaya ya rasilimali na ufisadi watu kimyaaa

Na hapa niwashukuru CDM kwa kuonyesha njia, lakini maandamano yale yangekuwa na nguvu zaidi kama yasingekuwa na chembe ya siasa (si mnawaona MAT)

Tatizo watanzania hawaoni uhusiano wa mambo haya na serikali iliyapo madarakani. Until then, mambo yatazidi kuwa magumu sana

Watanzania sisi ni waoga.
 
Watanzania sisi ni waoga.
Bora umeliona hilo Mkuu,
In life we dont get what we want, but we get in life what we are. Na sasa ndio tunapata matunda ya uoga wetu. Serikali inajua uoga wetu,kwa namna tunavyoreact kwenye issues na ndio maana wanafanya watakavyo. Kuna msemo unasema, "you can discover what your enemy fears most by observing the means he uses to frighten you" by Eric Hoffer.

Kwa nini kwenye saga la MAT, Serikali iliufyata?
Ni baada ya kuona Madaktari hawaogopi chochote, even if it cost their employments or the lives of our fellow Tanzanians. Oooh my God, kumbe bado hawajamalizana, sasa tusubiri tena kile ambacho kesho itatuletea. The clock is ticking my friend
 
Ni kweli unalolizungumza mkuu,hapa inabdi kuandamana.kukaa kwentu kimya ndo kunasababisha kuzidi kuumia.Inabidi wananchi tuandamane kushinikiza serekali ijali wnanchi wake na gharama za maisha zishuke.Kila kitu kipo juu mishahara midogo tutafika wapi?Jamani watanzania tuamke tuache uwoga gata middleeast changes zimetokana na wanachi wenyewe. SS tunaumia ila kuna watu wanachezea pesa hapa hapa bongo.
 
Kuna mtua aliwahi kuniambia TANZANIA NA INDIA NDO NCHI PEKEE AMBAZO WANACHI WAKE NI WAOGA KAMA NINI, INDIA HUWEZI KUTA MAANDAMANO WAHINDI NI WAOGA SANA, NA BONGO NDO HIVYO HIVYO,

BACK TO THE POIN

1. Hili la maisha kuwa magumu nalo ni fundisho kwetu, wewe unazania ni kwa nini nchi za ulaya population yao inashuka? Mfano Urusi imeamua kutoa motisha kwa wamama watakao jifungua serikali itale, ni kwamba wazungu baada ya maisha kuwa magumu wameamua hata kuzaa hawazai tena, mzungu anazaa mtoto mmoja basi.

2- SAA ZINGINE SISI WENYEWE NDO TUNAFANYA MAISHA YAWE MAGUMU WALA SI SERIKALI,

-SIMU YA MKONONI- Wazungu hawawezi kupigia mtu simu kama hana ishu ya muhimu sana na kama ni swala la ndugu wanasalimiana kila hata baada ya miezi 3 na siku hiyo wanaweza ongea kwenye simu saa nzima.

- SISI WABONGO KILA DAKIKA NI KUSALIMIANA TU, MTU ULIMSALIMIA JANA NA LEO TENA TENA JUST KUMPA HAI TU, HAYA NI MATUMIZI YASIYO KUWA NA MAANA, MASWALA YA TAFADHALI NIONGEZEE CREDIT YAKO HUKU EAST AFRICA TU TENA KWA WINGI TANZANIA

KUHUSU BAJETI YAKO,

1. Watanzania hauwezi kupanga bajeti kama wazungu, mzungu anapanga bajeti ya mwezi mmoja na anastick kwenye bajeti yake hiyo so wabongo

- Ni wangapi wanaenda Supermarket au shoping sehemu yoyote ile na list ya vitu vya kununua na unstick wkenye hiyo list?i
- Watanzania tunaamka asubuhi kwenda kazini lakini jioni mtu anarud na VIATU na havikuwa kwenye bajeti yake kisa tu amekuta vinatembezwa.

- Maswala ya kutoana Lunch, Breakfast na Dinner yako huku kwetu, tunapenda sana sifa, kwa wazungu hakuna FREE LUNCH WAKUU NA HII NI KUTOKANA NA BAJETI ZAO

Vitu vingine vinavyo changia kuwa na matumizi makubwa ni
1. Kutashindana kula mtaani, hasa waliopanga, make huwa kuna mashindano ya nani anapika chakula cha ghalama,

2. SIMU KAMA BILIVYO SEMA

3. NDUGU. JAMAA NA MARAFIKI- Hapa napo ndo tatizo lilipo. Extende famally

4. Kampani za kusaidiana kwenda Viwanja, kampani za kusaidiana kwenda viwanja ni tatizo sana na mimi huwa naziepuka mno, make HISTORIA HAITAKUMBUKA KMPANI ZAKO BALI UMEFANYA NINI KINACHO ONEKANA
- Kampani za makazini nazo ni shida

5. SHEREHE ZISIZO ISHA- Hizi sherehe zinakula sana pesa na mimi hapa nimeamua moja kukubali lawama tu, usipo angalia unaweza kuwa unatumia hadi 4 milioni kwa mwaka kwenye kuchangia HARUSI, UBALIKIO, KIPA IMARA, SHEREHE ZA KUAGA, NA GRADUATION, NOW DAY HADI WALE WA BABY CLASS WANAFANYIWA SHEREHE


ULIWEZA KUSTICK KWENYE BAJETI YAKO YA KILA MWEZI HUTAONA MAISHA MAGUMU ILA MAISHA YANAKUWA MAGUMU KWA SABABU YA SIFA ZETU MTAANI NA KWA WASHIKAJI NA WAFANYAKAZI WENZETU
 
Mkuu kwa upande wa kupanda gharama za gesi za majumbani ni kwamba inaonekana hii biashara ina mikono ya wakubwa serikalini hasa pale wizara ya nishati na mafisadi wanaowaendesha watendaji wake. Watu wa TPDC walishasema wanauwezo wa kupaki gesi inayopatikana hapa nchini kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na ikauzwa kwa bei nafuu kabisa lakini serikali imewakatalia bila kutoa sababu ya msingi na kuwaacha Oryx waki-monopolize soko. Wakubwa wana bahasha zao huko Oryx.
 
Kuna mtua aliwahi kuniambia TANZANIA NA INDIA NDO NCHI PEKEE AMBAZO WANACHI WAKE NI WAOGA KAMA NINI, INDIA HUWEZI KUTA MAANDAMANO WAHINDI NI WAOGA SANA, NA BONGO NDO HIVYO HIVYO,

BACK TO THE POIN

1. Hili la maisha kuwa magumu nalo ni fundisho kwetu, wewe unazania ni kwa nini nchi za ulaya population yao inashuka? Mfano Urusi imeamua kutoa motisha kwa wamama watakao jifungua serikali itale, ni kwamba wazungu baada ya maisha kuwa magumu wameamua hata kuzaa hawazai tena, mzungu anazaa mtoto mmoja basi.

2- SAA ZINGINE SISI WENYEWE NDO TUNAFANYA MAISHA YAWE MAGUMU WALA SI SERIKALI,

-SIMU YA MKONONI- Wazungu hawawezi kupigia mtu simu kama hana ishu ya muhimu sana na kama ni swala la ndugu wanasalimiana kila hata baada ya miezi 3 na siku hiyo wanaweza ongea kwenye simu saa nzima.




Population inaingiaje kwenye mfumuko wa bei?
Mie nimepanga bajeti ya mwezi mzima lakini kila nikienda dukani nakuta bei imepanda,tatizo ni system na sio wananchi!
 
Ni kweli unalolizungumza mkuu,hapa inabdi kuandamana.kukaa kwentu kimya ndo kunasababisha kuzidi kuumia.Inabidi wananchi tuandamane kushinikiza serekali ijali wnanchi wake na gharama za maisha zishuke.Kila kitu kipo juu mishahara midogo tutafika wapi?Jamani watanzania tuamke tuache uwoga gata middleeast changes zimetokana na wanachi wenyewe. SS tunaumia ila kuna watu wanachezea pesa hapa hapa bongo.

Mkuu napingana na ww kwenye hili,wazungu wenzetu wameshaendelea sana na sio ugumu wa misha ambao umewafanya waache kuzaa.Huko ulaya na chi nyingi zilizoendelea vyakula na vitu kama gas ni rahisi sana.Hapa kwetu serekali inapiga kampeni ya watu kunywa maziwa wakti mtanzania wa kawaida kunywa maziwa ni issue.Yaani hapa kwetu kula chakula kitu ni issue ajili ya bei zilivyo juu. Ss hivi sukari bei ni tsh 2300 kilo moja,kila bidhaa unayoiona ipo juu,dagga nazo kilo mpka elfu nne zile za mwanza na za kigoma ndo hazishikiki je mtanzania akimbilie wapi?Nina msupport mchangia mada pale anaesema watanzania ni waoga,uwoga unatupeleka pabaya kwani kila siku tunazidi kuumia tunanyamaza kimya.
Wanachi inabidi tusemame na kuihinikiza serekali itazame jambo hili kwa kina,kama gas tunaweza kuzalisha hapa kwetu kwa nn inunuliwe kutoka sehemu ingine?kama gas bei kubwa basi acheni tutumie mkaa tupange namna yakutunza mazingira na mkaa tutumie na sio kukutoa kwenye mkaa wakati huko tunakokimbilia hamna wepesi.
 
Mkuu napingana na ww kwenye hili,wazungu wenzetu wameshaendelea sana na sio ugumu wa misha ambao umewafanya waache kuzaa.Huko ulaya na chi nyingi zilizoendelea vyakula na vitu kama gas ni rahisi sana.Hapa kwetu serekali inapiga kampeni ya watu kunywa maziwa wakti mtanzania wa kawaida kunywa maziwa ni issue.Yaani hapa kwetu kula chakula kitu ni issue ajili ya bei zilivyo juu. Ss hivi sukari bei ni tsh 2300 kilo moja,kila bidhaa unayoiona ipo juu,dagga nazo kilo mpka elfu nne zile za mwanza na za kigoma ndo hazishikiki je mtanzania akimbilie wapi?Nina msupport mchangia mada pale anaesema watanzania ni waoga,uwoga unatupeleka pabaya kwani kila siku tunazidi kuumia tunanyamaza kimya.
Wanachi inabidi tusemame na kuihinikiza serekali itazame jambo hili kwa kina,kama gas tunaweza kuzalisha hapa kwetu kwa nn inunuliwe kutoka sehemu ingine?kama gas bei kubwa basi acheni tutumie mkaa tupange namna yakutunza mazingira na mkaa tutumie na sio kukutoa kwenye mkaa wakati huko tunakokimbilia hamna wepesi.

NANI KA KWAMBI GESI KULE KWAO NI RAHISI? MKUU HUKO UFARANSA, LONDON NA KWINGINEKO WANAO MUDU KUNUNUA GES YA KUTOSHA KU WARM NYUMBA ZAO NI WALE WENYE PESA,

1. KAMPENI YA MAZIWA- UNASHINDWA KUNYWA MAZIWA ILA UNAWEZA KUNYWA BIA, SIMU YAKO HAIKOSI VOCHA TENA KWA KUWASILIANA NA MADEMU/MAMENI NA KWA ISHU ZISIZO KUWA NA MAANA, UNAWEZA KUWATOA WASHIKAJI AUT NA KUWAPIGA OFA, UNAWEZA KUNUNUA PAMBA ZA BEI MBAYA,

2. BEI ZA SUKARI NA DAGAA,- NI KWELI ZIKO JUU NDO MAANA NASEMA NI LAZIMA NA SISI TUJIFUNZE KUBANA MATUMIZI, HAPA MTAANI KWANGU KUNA JAMAA AMEKUJA KUNIKOPA PESA ET AKATOE MCHANGO WA HARUSI SH 50,000, UNATARAJIA NINI HAPA?
- HIVI UNAWEZA LIA MASHA MAGUMU WAKATI WEWE UNAENDELEA KUCHANGIA HARUSI, NA KUWAPIGA WATU OFA?
-WEWE UNZANI NI KWA NINI WAHINDI HAWAENDAGI BAA? AU NI PESA HAWANA?

Matumizi makubwa sana ya watanzania ni kwenye anasa na si kitu kingine
 
niliwahi kusema hapa siku moja, tunahitaji kuingia zaidi ya barabarani. Nkuu wetu ambaye tulimtegemea walau akemee na kutoa mwongozo yuko kimya, na siku akiongea utamsikia akilalamika. Mie nahisi tunahitaji kufanya jambo amabalo, hata hao wakuu wenyewe hatawalisahau na watakapolikumbuka, watakumbushwa kuwa hii nchi ni yetu sote na sote tuna haki ya kuishi kwa neema. By the way, mie naona tunaongea sana na keyborad with no sparks, sie ni kama majibwa yanayobweka saana, bali hayana meno ya kung'ata. Ni wazi kuwa kuorganise maandamano ndio issue kubwa, kila mtu ni mwoga wa maandamano, eti tunaogopa kuuawa.

Kuna njia moja inayoweza kusaidia hapa, sie ambao tuna uwezo wa kukutana walau hapa twaweza initiate kitu na wengine wakafuata. Ingawa tuko katika sehemu tofauti za TZ, ni wazi twaweza fanya jambo. tushauriane ni kipi tufanye, twaweza andaa vipeperushi, na kila mmoja wetu mwenye uwezo wa kuptint na kupata kopi walau 50, avitumie hivyo kutoa elimu kwa jamii, iliyo nje ya mitandao hii, huo utakuwa mwanzo mzuri. Elimu kwanza mengine huja automatically
 
niliwahi kusema hapa siku moja, tunahitaji kuingia zaidi ya barabarani. Nkuu wetu ambaye tulimtegemea walau akemee na kutoa mwongozo yuko kimya, na siku akiongea utamsikia akilalamika. Mie nahisi tunahitaji kufanya jambo amabalo, hata hao wakuu wenyewe hatawalisahau na watakapolikumbuka, watakumbushwa kuwa hii nchi ni yetu sote na sote tuna haki ya kuishi kwa neema. By the way, mie naona tunaongea sana na keyborad with no sparks, sie ni kama majibwa yanayobweka saana, bali hayana meno ya kung'ata. Ni wazi kuwa kuorganise maandamano ndio issue kubwa, kila mtu ni mwoga wa maandamano, eti tunaogopa kuuawa.

Kuna njia moja inayoweza kusaidia hapa, sie ambao tuna uwezo wa kukutana walau hapa twaweza initiate kitu na wengine wakafuata. Ingawa tuko katika sehemu tofauti za TZ, ni wazi twaweza fanya jambo. tushauriane ni kipi tufanye, twaweza andaa vipeperushi, na kila mmoja wetu mwenye uwezo wa kuptint na kupata kopi walau 50, avitumie hivyo kutoa elimu kwa jamii, iliyo nje ya mitandao hii, huo utakuwa mwanzo mzuri. Elimu kwanza mengine huja automatically

TATIZO NI KWAMBA SISI WATANZANIA HATUJAWAHI PITA MAISHA MAGUMU KAMA KENYA,

NA WATNZANIA NI WAOGA SANA NA HII VILEVILE INASABABISHWA NA HISTORIA YA NCHI YETU NA CHEKI HATA NCHI ZINGINE ZA KIJAMAA WALIVYO WAOGA KUANDAMANA,

1. CHINA
2. URUSI- Wanaandamana watu 400 tu
3. CUBA

Na ili mandamano yafanikiwe yanahitaji sapoti ya wadau wengi kama vile

1. Wafanyakazi wagome kwenda makazini

2. Watu wa TANESCO wakate umeme bila sababu

3. Watu wa maji wakate maji

4. Wanafuzi wasiingie madarasni

Hapa mandamano ya aina hii hayawezo dumu siku 2 kabla ya mkuu hajasalimu amri,

ILA HILI LA KUANDAMANA WAKATI SHUGHULI ZINGINE ZINAENDELEA KAMA KAWA WALA HALINA IMPACT SANA KWA WATAWALA WETU
 
maisha ja watazania ajawezi kupungua makali ata akija nani madarakani
pesa yetu iko weak sana , kila mwezi $ inapanada dhamani , ikipanda vitu vinapanda
na anatuna export capacity kwanza pili utalii tanzania ni ghali sana , watalii wanakimbia
chumba kulala unaambiwa $300, ni ghali kuliko nchi nyingi za ulaya
sidhani kama kutakua na nafuu
 
Tulikuwa na nafasi ya kuleta mabadiliko, miezi kama 15 iliyopita na tukaichezea. Sasa ngoja kwanza Somo liwaingie vizuri. Anyway dawa ni rahisi sana, kwa kuwa sisi (wananchi) ndio waajiri wa serikali, basi dawa yake ni kuiondoa madarakani. Lakini wakati tunasubiri hiyo 2015 ni lazima tuwe na mipango ya muda mfupi.

Mipango hii ipo mingi sana, but nitajikita kwenye miwili tu
Njia moja wapo ni kuwasilisha malalamiko yetu kwa wabunge wetu, ili wayasemee bungeni (sijui nao bado wanasimamia maslahi yetu) na ikiwezekana wasiunge mkono budget ya serikali mpaka kodi kwenye vitu vya msingi kama hivyo itakapoondelewa kama si kupunguzwa.

Njia ya pili na rahisi zaidi ni kuingia barabarani, mpaka kieleweke. Unakumbuka, kilichotokea Zambia, kipindi mkate ulivyopanda bei? (tatizo watanzania ni watu wa ajabu sana)

nimekubali mawazo yako, inaonesha unauchaji wakutosha, ila naomba niongeze jambo hapa tz hakuna uwiano wa mishahara k2 ambacho kinajenga matabaka kwa kasi kubwa, hapa nachosema mishahara yetu haitoshi kukidhi maitaji yetu muhumu, na maitaji muhimu ya kijamii lazma yawe ktk mafungu haya, basic needs, investiment&business,savings, na entertainment. Jamii yoyote inayomudu mafungu hayo manne ndio jamii endelevu lakin cc tunaishia ktk fungu la kwanza na yani basic needs na hatuli kidhi ataivyo.. Mishahara ipande haswa ile iliyo ya kima cha chini na kodi ziondolewe ktk mambo muhimu ya kijamii kama nilivyo bainisha.
 
Wadau kupanda kwa gharama za maisha kumeongezwa zaidi na serikali yetu kutokuwa na vipaombele katika maendeleo ya nchi. Hii inajionyesha wazi kwa nchi yetu:

kuendeshwa na matukio
kuwa na sera ambazo hazitekelezwi ipasavyo
kutokua na utaalamu wa kutosha na kama upo hautekelezwi vizuri.


Wadau mtakubaliana na mimi kwamba kwa kiasi kikubwa mfumuko wa bei umesasabishwa na kupungua kwa uzalishaji hasa katika kilimo ambapo ndio nyenzo kubwa ya mtanzania, wakati huo huo hamna juhudi kubwa za kitaalamu kuhakikisha tunakuwa na kilimo cha kisasa chenye tija kwa mtanzania.

Aidha mfumo wetu uliopo unawafanya vijana wetu kuwa ni watu wa kuajiriwa maofisini na kutafuta fedha tu,bila kujua bila kujikita katika sekta hii nyeti, uzalishaji utaendelea kupungua matokeo yake unaweza kuwa na fedha nyingi zenye thamani kidogo...
Wadau ni ajabu nchi yetu ina ardhi nzuri, bahari, maziwa makubwa, mito na mabonde lakini bado wananchi wake wanalia njaa.
nakubaliana na usemi huu "ukiwa na njaa ni ngumu kuwaza maendeleo."

Watanzania tuamke tuige mfano ya nchi zinazoendelea na zilizoendelea. Kama kikwazo ni serikali, chama, kabila, dini au kikundi cha watu ni wakati wa kufanya mabadiliko.

by MCRT.


 
Back
Top Bottom