Uongo wa TANESCO mwisho leo - September 14, 2015

Uongo wa TANESCO mwisho leo - September 14, 2015

Yaani hawa watu wamekata umeme huku kijichi sasa hivi.....

Jana yenyewe walikata hadi saa nane usiku kama sikosei

Nina hasira nao...tutakutana october 25
 
Tatizo nao washatuona sie wajinga. Tutaishia kulalamika umu umu kwenye mitandao tuu
 
Tusilalamike jamani...october 25 ni zamu yetu kuwatia atabu ili tuheshimiane...
 
Tanesco kwenye taarifa ya habari ya chanell leo waseme mgao wa umeme utamalizika rasmi ijumaa baada ya kumalizika kwa zoezi la kuunganisha bomba la gesi .

Waliozea kuishi kwa uwongo hawawezi kuishi kwa ukweli ngoja tuone .
 
Tanesco kwenye taarifa ya habari ya chanell leo waseme mgao wa umeme utamalizika rasmi ijumaa baada ya kumalizika kwa zoezi la kuunganisha bomba la gesi .

Waliozea kuishi kwa uwongo hawawezi kuishi kwa ukweli ngoja tuone .
Kwanini Mkurugenzi mkuu aliongea jumatatu ilopita kuwa zoezi lingechukua siku 7 tu ambapo j.3 hii ndo ilikua siku ya 7 na mgao bado unaendelea?
 
Yaani alivyofanyiwa tu zengwe Prof Muhongo...

Hali ya umeme kukatika hovyo ilirejea kama zamani...
 
Dawa ni kuitoa ccm madarakani tusidanganyike Ndugu zangu hawa jamaa wameshindwa kila sekta tusipowatoa hali hii haitoisha
 
hakuna mwaka uliowahi kupita bila mgao wa umeme hapo ndipo wanatudhihirishia ahad zao ni uwongo
 
Kuna deal la mtoto mmoja wa kigogo kufanya majaribio kwa mafuta ya Ndege baada hapo alipwe chake ndio hizo gesi zenu zianze kufanyiwa majaribio; huu ndio ukweli; mengine yote geresha!
 
Wakiona nyomi ya lowassa tu wanapata maelekezo toka ngazi za juu wakate ili isionekane kwenye TV
 
Yaani leo saa 11 alfajiri wameshauchukua shati nimepasi nusu ikabidi nivae la jana.
 
mashirika ya umma yangekua yanalaaniwa... Tanesco laana zangu mngezipata zamani sana, mngekuwa mnaokota makopo sa hizi
 
Tanesco mmekua watu wa kutukatia umeme kila siku na kutulaza giza. mlisema mtakata kwa wiki mbili sasa imekua mwezi na imekua kero kwa sisi tunaotegemea umeme. Kama imeshindikana acheni mfumo wa zamani ufanye kazi
 
Tanesco wanatupa wakati mgumu sana
 

Attachments

  • 1442464890965.jpg
    1442464890965.jpg
    23.5 KB · Views: 204
Na kweli ndugu na kama arusha watakuwa wanakaribia miezi mitatu sasa duh bora wawaze tena upya,
 
Back
Top Bottom