Habari zenu great thinkers wote, mimi natatizwa sana na hali ya umeme iliyopo sasa kwa jiji la dsm sehemu nyingine sijui.
Almost kila siku umeme unakatika asubuhi na kurudi kati ya saa 12 hadi moja usiku.
Kwa maisha ya watanzania wengi hasa wanaoishi mjini umeme ndio chanzo kikuu cha mapato ya mtu. Wengi wamejikita kwenye vibiashra/vishughuli vinavyohitaji umeme ili kujipatia kipato.
Halii hii imekuwa tete mno kiasi kwamba hata ule uwezo wa kuishi chini ya dola moja umezidi kupungua.
Naomba kama kuna wahusika humu wanisaidie kujibu maswali haya;
Tatizo hili litaisha lini?
Kuwepo kwa gesi kumeongeza au kupunguza nini kwenye mfumo wa umeme wa Taifa?
Je na hili nalo ni siasa?
Kwa nini Tanesco hawatangazi kuwa ni janga?
ASANTENI