University of Dar es Salaam(UDSM) Alumni - Special thread

University of Dar es Salaam(UDSM) Alumni - Special thread

Mimi nilikuwepo hapo 1972-75.

Nilihitimu na kutunukiwa BA in Janitorial and Bullshit science na baada ya hapo nikapangiwa kazi Nachingwea.
 
Mimi nlikuwa hapo 2006-2009 hadi namaliza chuo tuliwahi kugoma Mara kumi na moja...Mara maji hakuna, Mara boom limechelewa, Mara odong odwaa, kakatwa kugombea urais Wa chuo kiss mganda duhhhh.

2009huo mgomo ulinikuta,ambapo mkazi wa Hall II alipoteza maisha pale swimming pool,makaz ya Mkandala yaliharibiwa,na ndo hapo chuo kikaamua kuweka matenk makubwa mawili kila hall residence kama vile mabibo ,wakat huo wazir ea elim ni Maghembe.Ila pia ni kipindi hicho hicho na wahadhiri wa UDSM waligoma kwa siku kadhaa
 
Nilitiseka sana kutafuta kitabu Manitoba nilikua sijui utaratibu wa kuingilia mwenyewe kwenye kompyuta

Mkuu mimi library sijawahi ingia kusoma kabisa zaidi ya kufanyia ue tu ata utaratibu wake nilikua siujui 😝😝😝😝😝😝
 
2009huo mgomo ulinikuta,ambapo mkazi wa Hall II alipoteza maisha pale swimming pool,makaz ya Mkandala yaliharibiwa,na ndo hapo chuo kikaamua kuweka matenk makubwa mawili kila hall residence kama vile mabibo ,wakat huo wazir ea elim ni Maghembe.Ila pia ni kipindi hicho hicho na wahadhiri wa UDSM waligoma kwa siku kadhaa

Huo mgomo wa lecturers ndio uliongozwa na dr nyahoro nn alikua mtata sana huyu mzee katusumbua sana na kozi lake la foundation engineering second yr 😊😊😊
 
Mimi nilikuwepo hapo 1972-75.

Nilihitimu na kutunukiwa BA in Janitorial and Bullshit science na baada ya hapo nikapangiwa kazi Nachingwea.

Duuuh hiyo course nadhani currently haipo mkuu.......wewe ni nyani mzee😆😆😆😆
 
Huo mtindo ulikuwa zaidi pale hall 5 na hall two...

Daa miaka mitatu tumekula exile za kutosha saana.

Hahahaha umenikumbusha mbali sana mambo ya exile hata mabibo ilikuwepo sasa unapenyezewa tu text oya usije rum niko na shemeji yako tumepiga sana kambi chini ya vimbweta pale tukiwa exile😝😝😝😝
 
Nna meengi ya kukumbuka UDSM,mazur na mabaya,yakufirahisha na kuhuzunisha,ila ukweli siku niliyomaliza mtihani wangu wa mwisho wa kumaliza UNDERGRADUATE PALE THEATRE 2 NILIFURAHI SANA MPAKA NIKAWA NATOKWA NA MACHOZI,SITASAHAU HII KITU ASILANI,NDO ILIKUA GRADUATION YANGU HIYO

Kweli ulikua una haki ya kutoa machozi mkuu maana pale si mchezo wazee wamejaa roho mbaya tu, sisi department yetu mwanamke alikua mmoja tu nae ni secretary ila lecturers na TA 's wote wanaume wametutesa sana mkuu hii imepelekea graduates wengi kua na roho za kikauzu😎😎😎
 
Mkuu mimi library sijawahi ingia kusoma kabisa zaidi ya kufanyia ue tu ata utaratibu wake nilikua siujui 😝😝😝😝😝😝

Engineering wengi hawaingiagi libral labda wakiingia wanaenda kujisomea vitabu vyao wanavyoingia navyo wenyewe au soft copy...

But libral kuna usingizi balaaaa
 
Engineering wengi hawaingiagi libral labda wakiingia wanaenda kujisomea vitabu vyao wanavyoingia navyo wenyewe au soft copy...

But libral kuna usingizi balaaaa

Library kule kumetulia balaa usingizi nje nje😊😊😊😊
 
  • Thanks
Reactions: itv
2009huo mgomo ulinikuta,ambapo mkazi wa Hall II alipoteza maisha pale swimming pool,makaz ya Mkandala yaliharibiwa,na ndo hapo chuo kikaamua kuweka matenk makubwa mawili kila hall residence kama vile mabibo ,wakat huo wazir ea elim ni Maghembe.Ila pia ni kipindi hicho hicho na wahadhiri wa UDSM waligoma kwa siku kadhaa
mkuu kama sijakosea ilikuwa 2008 na siyo 2009.
 
Bila kusahau UDASA, sisi tulikuwa tunapaita YUDASA, ukipeleka mtoto wa kike pale lazima akuheshimu. Boom likikata unarudi zako manzese kula maandazi.

Mimi series nimezijulia Chuo, enzi hizo mnaenda kuangalia prison break chumbani kwa mshkj mwenye desktop. Computer zenyewe zilikuwa zimejaa tutorial tu a.k.a pilau (movie za ngono)

Watu tulikuwa tunachukulia boom dirishani karibu na ofisi za auxiliary police pembeni ya faculty of business siku hizi Ndio UDBS

Hivi siku hizi pepa za matriculation zipo? Ulikuwa huingii Chuo bila kufanya hizo pepa

Kuna mtu alikuwa anaitwa Pasiense Mlowe alikuwa anagombania uraisi wa DARUSO akichuana na Mganda anaitwa Odong Odwaa, huo mpambano asikwambie mtu ulikuwa kiboko. Utawala wanamtaka Pasiense wakati wanafunzi wanamtaka Odong. Pasiense alikuwa na Msemo wake mmoja "tofautisha Kati ya hamu na shauku"

Niachie hapo Ila UDSM is the best, pamoja na vioja vyote Ila nili enjoy maana Ndio kilikuwa Chuo cha ndoto zangu. Kusoma UD enzi hizo ni title mtaani.
Haswaaaaa 100%
 
Sitakuja kusahau toka mwaka wa kwanza ckuwah Ku supp lakin mwaka wa Pili semester ya pil nilipata supplementary ya LL 2014, sikuweza kuichomoa hyo kozi na ikanibid ni carry mwaka wa tatu semester ya mwisho. Kilichonishtua ni kwamba sikuwah Ku supp sasa ile Ku supp Mara ya kwanza inakuwaje nashindwa kusapua mpaka naibeba hyo kozi mwaka wa tatu semester ya mwisho. Aisee mwaka wa tatu semester ya pil nimesoma kwa presha sana kutokana na hilo. Mwaka wa kwanza niliish hall 5 sasa mwaka wa pili na wa tatu nikawa naish msewe, changamoto za kwenda kusoma chuo usiku mm na jamaa zangu. Thanx God 2012 nilimalza fresh. Aisee Prof Said a Othman nusura anibakishe na hyo koz mwaka wa tatu, Cjui ingekuweje kushindwa Ku graduate kwa koz za arts wakat wazee wa koz ngumu wakivaa majoho.
 
Hii ni special thread wa ajili ya ex- Udsm students kushare moments mbali mbali tulizokutana nazo katika kipindi chetu cha masomo pale mlimani ziwe happy moments, sad moments etc.

Binafsi nilikua sijui history ya kikundi cha THE PUNCH, story za kina Nyerere kuchapa bakora.

Wanafunzi waliogoma enzi hizo, hebu tujiachie hapa kwa kuweka story mbali mbali tujifunze mambo mengi yaliyofanyika wayback tujifunze pia.

Mimi binafsi nilikuwepo pale tangu 2009-2013.

Ngoja ni share kidogo top 5 moments zangu na wengine mtiririke tuongeze siku.....

1. Nilitaka kuacha chuo week 1, 1st yr kisa ratiba ya vipindi nilichanganyikiwa kila kipindi kilicho kwenye ratiba nilikua naingia, brother mmoja ndo akanambia dogo hiyo ni ratiba ya college nzima akanisaidia kutick vipindi vyangu nikapata auheni (ushamba mzigo).

2. Tukiwa 2nd yr lecturers walikua aibu baada ya kwenda staff 8 kusimamia supplementary wanafunzi 5 wakafika wakajicheka wenyewe

3. Vituko vya dr.azafel fedha lwaitama alishawahi kuja darasani 2010 akatuambia jamani mwenzenu mwaka huu nakufa tukamuuliza kwanini akasema sheikh yahaya kasema mwaka huu wote tunaompinga jk tutakufa na mimi ni mmoja wao
Siku nyingine tena kaja kakuta ubao haujafutwa kaanza kuandika juu yake

4. Tukiwa 2nd yr ulitokea mgomo mkubwa wa kudai kuongezeka boom kutoka 5000-10000 kwa siku, sisi viongozi wa college yetu wakagoma wakasema wanataka walete official letter eti ili tujoin mgomo jamaa wakagoma matokeo yake wakaungana college zote kuja kutupiga college kwetu zilipigwa ngumi hatari matokeo yake tukafunga Mageti yote ya college yetu na hakuruhusiwa mtu yeyote kuingia ndani ya college kama hausiki ukikaidi kipigo cha haja kilikua kinatembezwa, tukaanzisha sasa ka mgomo ka kutaka mwenzetu mmoja aliekua amedisco arudishwe matokeo yake tukafukuzwa chuo kikafunga tulipo rudi wenzetu zaidi ya 100 walidisco kutokana na ratiba za mitihani tight

5. Kuingilia madirishani kwenye shuttle, purukushani zake zilikua si mchezo wale wa mabibo wanaelewa vizuri nishataka kupasua fuvu la kichwa siku moja baada ya kujigonga kwenye dirisha, mambo ya shuttlepori na kukomunika(kula mikate na chai pale boom linapokata).

Watu waliokua wanaongooza kwa kuoana na kufunga harusi enzi hizo ni waalimu kila siku mara vikao vya kitchen party, engagement mara sendoff.

School of Business: Hawa walikuwa wazee wa show off kuanzia wanaume kwa wanawake,
Law school wazee wa ma suti muda wote.

Engineering: Hawa ni desa boys non-complicators, very rough

Haya wazee wa zamani tiririkeni na nyinyi tufurahi...
Bila shaka wewe jamaa utakua LL.B....Tanchi stori ulipewa na kabudi....
 
Hii ni special thread wa ajili ya ex- Udsm students kushare moments mbali mbali tulizokutana nazo katika kipindi chetu cha masomo pale mlimani ziwe happy moments, sad moments etc.

Binafsi nilikua sijui history ya kikundi cha THE PUNCH, story za kina Nyerere kuchapa bakora.

Wanafunzi waliogoma enzi hizo, hebu tujiachie hapa kwa kuweka story mbali mbali tujifunze mambo mengi yaliyofanyika wayback tujifunze pia.

Mimi binafsi nilikuwepo pale tangu 2009-2013.

Ngoja ni share kidogo top 5 moments zangu na wengine mtiririke tuongeze siku.....

1. Nilitaka kuacha chuo week 1, 1st yr kisa ratiba ya vipindi nilichanganyikiwa kila kipindi kilicho kwenye ratiba nilikua naingia, brother mmoja ndo akanambia dogo hiyo ni ratiba ya college nzima akanisaidia kutick vipindi vyangu nikapata auheni (ushamba mzigo).

2. Tukiwa 2nd yr lecturers walikua aibu baada ya kwenda staff 8 kusimamia supplementary wanafunzi 5 wakafika wakajicheka wenyewe

3. Vituko vya dr.azafel fedha lwaitama alishawahi kuja darasani 2010 akatuambia jamani mwenzenu mwaka huu nakufa tukamuuliza kwanini akasema sheikh yahaya kasema mwaka huu wote tunaompinga jk tutakufa na mimi ni mmoja wao
Siku nyingine tena kaja kakuta ubao haujafutwa kaanza kuandika juu yake

4. Tukiwa 2nd yr ulitokea mgomo mkubwa wa kudai kuongezeka boom kutoka 5000-10000 kwa siku, sisi viongozi wa college yetu wakagoma wakasema wanataka walete official letter eti ili tujoin mgomo jamaa wakagoma matokeo yake wakaungana college zote kuja kutupiga college kwetu zilipigwa ngumi hatari matokeo yake tukafunga Mageti yote ya college yetu na hakuruhusiwa mtu yeyote kuingia ndani ya college kama hausiki ukikaidi kipigo cha haja kilikua kinatembezwa, tukaanzisha sasa ka mgomo ka kutaka mwenzetu mmoja aliekua amedisco arudishwe matokeo yake tukafukuzwa chuo kikafunga tulipo rudi wenzetu zaidi ya 100 walidisco kutokana na ratiba za mitihani tight

5. Kuingilia madirishani kwenye shuttle, purukushani zake zilikua si mchezo wale wa mabibo wanaelewa vizuri nishataka kupasua fuvu la kichwa siku moja baada ya kujigonga kwenye dirisha, mambo ya shuttlepori na kukomunika(kula mikate na chai pale boom linapokata).

Watu waliokua wanaongooza kwa kuoana na kufunga harusi enzi hizo ni waalimu kila siku mara vikao vya kitchen party, engagement mara sendoff.

School of Business: Hawa walikuwa wazee wa show off kuanzia wanaume kwa wanawake,
Law school wazee wa ma suti muda wote.

Engineering: Hawa ni desa boys non-complicators, very rough

Haya wazee wa zamani tiririkeni na nyinyi tufurahi...
kumbe ulikuwa COET, hahaha UDSM noma sana
 
Udsm, kweli ninepamis sana, nilikua hapo from 2008_2011, nilikua nakaa pale hall one kwa maseneta hahaha imagine kwa maseneta walikua wanakaa wanaume tu ila mimi jike peke yangu nlikua a room mitaa ile, yano niliachiwa room na boyfriend halafu yeye akahamia mabibo, weekend ndo akawa anakuja, tukaja kugombana sasa si nikamuachia room yake nikahamia zangu hall seven ambapo ndo ilikua room yangu niliyopangiwa

Later then he became my husband na tuna watoto wawili, sema yeye alikua mwaka wa nne sheria wakati mimi nipo first year,

Nakumbuka nlikua apenda sana kulala,kuna kipindi cha asubuhi nlikua nakichelewa kila siku mpaka lecturer akanikariri
 
Bila kusahau UDASA, sisi tulikuwa tunapaita YUDASA, ukipeleka mtoto wa kike pale lazima akuheshimu. Boom likikata unarudi zako manzese kula maandazi.

Mimi series nimezijulia Chuo, enzi hizo mnaenda kuangalia prison break chumbani kwa mshkj mwenye desktop. Computer zenyewe zilikuwa zimejaa tutorial tu a.k.a pilau (movie za ngono)

Watu tulikuwa tunachukulia boom dirishani karibu na ofisi za auxiliary police pembeni ya faculty of business siku hizi Ndio UDBS

Hivi siku hizi pepa za matriculation zipo? Ulikuwa huingii Chuo bila kufanya hizo pepa

Kuna mtu alikuwa anaitwa Pasiense Mlowe alikuwa anagombania uraisi wa DARUSO akichuana na Mganda anaitwa Odong Odwaa, huo mpambano asikwambie mtu ulikuwa kiboko. Utawala wanamtaka Pasiense wakati wanafunzi wanamtaka Odong. Pasiense alikuwa na Msemo wake mmoja "tofautisha Kati ya hamu na shauku"

Niachie hapo Ila UDSM is the best, pamoja na vioja vyote Ila nili enjoy maana Ndio kilikuwa Chuo cha ndoto zangu. Kusoma UD enzi hizo ni title mtaani.
Odong interpol walinrudisha kwao uganda baada ya ule mgomo uliosababisha chuo kufungwa, watu wengi walifukuzwa wengine walirudia miaka kama Antony machibya by then alikua rais wa daruso, ila odong jamani walimweka central almost wiki mbili kabla ya kumsafirisha,kuna siku mimi na best yangu tulienda kumsalimia odong central tuliwekwa kando tulihojiwa kama vile tumeenda kumtembelea gaidi
 
Back
Top Bottom