Umeanza kubisha kabla hata ya kuelewa concept yenyewe haha! alafu unajifanya mwanasayansi.
Unadhani kwa nini hizo images wanazoonyesha wanasema ni za miaka ya nyuma? Mwanga umesafiri miaka bilioni kadhaa ukafika hapa leo, picha tuliyopiga sio ya leo ni ya mwanga uliosafiri toka kipindi kile, kungekua na technology ya kukupeleka kwenye hizo galaxies leo hii ndani ya sekunde basi ungefika ungeona pako tofauti kabisa na picha zinazopigwa na telescopes.
So speed ya mwanga ni ileile, ambacho wewe hujaelewa tu ni kua picha tunazopiga leo si za kinachoendelea leo leo bali ni kitu kilichotokea miaka bilioni kadhaa ya nyuma ila sisi tunakiona leo, ni kama tunaona into the past vile, ila sio past yetu, ni past ya hizo galaxies za mbali, same goes kama kuna watu huko na wana telescopes basi hawatuoni, wanaona dunia ilivyokua miaka bilioni kadhaa nyuma kulingana na umbali waliopo. Yawezekana leo hii huko kwao kuna advanced civilizations kama sisi tu ila they can't bridge the distance gap, hilo ndo tatizo kubwa.
Time is relative usisahau hicho kitu. Ungesoma physics in deep ungeelewa. Soma ujue tuna-calculate vipi distance ya objects kutoka duniani utagundua kua ni sayansi moja very accurate.