Massenberg
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 1,173
- 1,373
Mimi ningependekeza zinunue magari na vifaa vya zimamoto nchini kote kwa kadri itakavyowezekana. Ni ushenzi wa hali ya juu kwa jiji kama Dsm lenye watu takribani milioni 5 halafu lina fire station moja tu ambayo magari yake ni kama mnavyoyajua.
Mkoani Manyara gari la zimamoto lipo Babati ambapo ni umbali wa kama saa nzima kutoka mji mdogo wa Katesh ambao eti unategemea gari hilo hilo.
Wenzetu Uingereza sheria imetamka kwamba likitokea tukio la dharura la kuhitaji zimamoto, gari la wagonjwa au polisi basi wahusika wanapaswa kufika eneo la tukio ndani ya dakika 8, zikizidi hapo bila sababu ya msingi mtu anawajibishwa na kufikishwa mahakamani.
Sisi tulibugi step wapi?
Mkoani Manyara gari la zimamoto lipo Babati ambapo ni umbali wa kama saa nzima kutoka mji mdogo wa Katesh ambao eti unategemea gari hilo hilo.
Wenzetu Uingereza sheria imetamka kwamba likitokea tukio la dharura la kuhitaji zimamoto, gari la wagonjwa au polisi basi wahusika wanapaswa kufika eneo la tukio ndani ya dakika 8, zikizidi hapo bila sababu ya msingi mtu anawajibishwa na kufikishwa mahakamani.
Sisi tulibugi step wapi?