Ungependekeza Bilion 600 za Dreamliner zitumikee wapi?

Ungependekeza Bilion 600 za Dreamliner zitumikee wapi?

Mkuu soko la ndege unalijua vizuri?
Ndio maana nchi za kibeparu zimeachia wafanya biashara kufanya kazi hii.
Litatushinda, na wote tutashuhuduaa humu
Mkuu Mangi, usikremu maisha kama wanavyo ya kremu watoto wa kidato cha nne na cha tano. Ulimwengu unakwenda ukibadilika sana, na njia za kuwaalika hao watalii na wageni huenda zikibadilika.
 
Sio mbaya wakiacha hela kwa jirani na huku wakaleta pia, msiambukizwe kuwa na roho mbaya kiasi hicho.
Mkuu Jogi unaelewa lengo la hizi ndege?. Utalii wakati mwingine huwa hauna huruma kama maisha yanavyotudanganyana.

Si suala la roho mbaya, hawa majirani zetu wa kaskazini ya mkoa wa Kilimanjaro hawajawahi kuwa na ruhuma. Inatulazimu tujipange ili katika siku zijazo watambue kwamba sisi sio wajinga kama walivyokuwa wakidhania kwa miaka mingi.
 
Unataka uwapangie maamuzi kuhusu ndege gani wapande na watue wapi?
Kaka Iparamasa, ukiwa na akili na ukawa na uwezo wa kutengeneza ushawishi kwa wanaozisoma hisia zako, basi kazi yako ya kuwaalika watalii waje Tanzania ni ndogo sana.
 
Billioni 600 zinaweza ajiri madaktari wapya 5000, manesi 10000, na kulipa mishahara yao kwa miaka kumi ya kipindi cha Magufuli. Bado kuna change ya kununua vifaa vita muhimu kila hospitali ya rufaa na kuokoa maisha ya watanzania wengi na bado kukawa na mabaki.

Better still asilimia kubwa ya matumizi ya mishahara ingeenda kwenye matumizi ya huduma zingine na bidhaa zinazochea uchumi. Serikari ingeoneka imetengeneza ajira huku pia uchumi ungepata mzunguko wa pesa.
 
Ingekuwa matakwa yangu ningejenga vyou vingi vya ufundi stadi vyenye mahitaji yote muhimu ya kufundishia walau viwili kila mkoa.

Kwa kujenga vyuo hivyo na kuweka mitaala itakayowezesha kuwapa vijana ujuzi na uwezo wa kujiajiri ingewafaa vijana wengi wa kitanzania.

Hali ya elimu ya sekondari kwa sasa ipo mahututi hususani shule za kata.Vijana wengi wanaohitimu kidato cha nne wanakosa sifa za kuendelea na elimu ya juu na pia hawaajiriki kutokana na ubomu wa elimu wanayoipata.

Kwa kufanya hivyo ingesaidia kukuza teknolojia na ubunifu na pia kuwapa vijana fursa ya kujiajiri.
 
No 4 umeongea la muhimu sana Mkuu.

Nilikuwa nacheki data za upatikanaji wa maji nchini kwenye mikoa mbalimbali..

Zaidi ya robo tatu ya Mkoa wote wa Tabora hawapati maji..

Na gharama zake zizikumbuki lakini nafikiri hazi zidi 100Bil.

Si bora kuwaondolea Tabora shida ya maji na sehemu nyingine za nchi...!!??

Huo m dreamliner nani ataupanda kuja kutalii hapa Tanzania... na asa ivi ndio tuna majanga ya ZIKA tena...shida tupu kwenye huo Utalii anaousema.

Maana alisema anataka ndege ya kuchukua watalii USA mpaka Tz.
mbona unamawazo ya kienyeji hivi? nani ka kwambia midege mikubwa kama hiyo inalipiwa cash? hivi hujiulizi Qatar hawana mafuta wala madini na wako jangwani na maisha yao nimazuri kuliko hata ya hao wazungu mliko enda kuosha macho huko ubelgiji. Hiyo ndege trip moja tu ya Dar New york inalipa mishahara ya mabalozi wote wa tanzania.

Hujiulizi kwanini ukipanda Ethiopia airline lazima upitishwe Addiss Ababa ahatakama unaenda Africa ya kusini? hujiulizi kwanini ukipanda kenya airways lazima upite Nairobi hatakama unaenda Zanzibar? Mbona mko kama mmetupwa jehanam kila siku kulalamika tu.
 
...Ningependa zitumike kuwa elimisha wananchi...lol

...serikali yeyote nzuri huinvest in its people.....

...hatusemi kununua ndege ni kubaya,ila ukifanya hivyo huku kuna watu wanakosa mkopo wa shule,lazima tuhoji weledi wako.....simply huku ni kukosa kufanya 'prioritization'.......

...binafsi nimepewa chance ya kusoma,ningependa na watu wote kny disadvantaged group wapewe nafasi ya kusoma,

..yes,wasome,watu wote,wapate elimu,lol

..kama mmoja alivyosema uchumi wetu unategemea kilimo,so elimu yetu iwe practical kwenye mazingira yetu...sio bora elimu tu
 
Billioni 600 zinaweza ajiri madaktari wapya 5000, manesi 10000, na kulipa mishahara yao kwa miaka kumi ya kipindi cha Magufuli. Bado kuna change ya kununua vifaa vita muhimu kila hospitali ya rufaa na kuokoa maisha ya watanzania wengi na bado kukawa na mabaki.

Better still asilimia kubwa ya matumizi ya mishahara ingeenda kwenye matumizi ya huduma zingine na bidhaa zinazochea uchumi. Serikari ingeoneka imetengeneza ajira huku pia uchumi ungepata mzunguko wa pesa.
Baada ya miaka kumi utawalipa nini? nani ka kwambia dege kama hilo linalipiwa cash? kwa taarifa yako dege hilo order iliwekwa na Andrew Chenge akaambiwa order imejaa labda waweke mwaka 2018 hapo wanaweza nunua moja.

Hiyo ndege moja mapato yake hatuhitaji kuita wawekezaji yanatosha kabisa, kwanza safari zake zitakuwa New york London Tokyo likija bongo nikubadilisha marubani tu linasonga tena. Qatar ka nchi kama zanzibar wanazo mia sie moja tu kihoro.
 
...Ningependa zitumike kuwa elimisha wananchi...lol

...serikali yeyote nzuri huinvest in its people.....

...hatusemi kununua ndege ni kubaya,ila ukifanya hivyo huku kuna watu wanakosa mkopo wa shule,lazima tuhoji weledi wako.....simply huku ni kukosa kufanya 'prioritization'.......

...binafsi nimepewa chance ya kusoma,ningependa na watu wote kny disadvantaged group wapewe nafasi ya kusoma,

..yes,wasome,watu wote,wapate elimu,lol

..kama mmoja alivyosema uchumi wetu unategemea kilimo,so elimu yetu iwe practical kwenye mazingira yetu...sio bora elimu tu
Wakipata mkopo wakasoma wakahitimu wataajiriwa wapi? tunanunua ndege ili wakihitimu ndio wawe marubani mafundi wa ndege na hata wakifeli basi wawe hata wagawa chai tatizo wanao hawana mvuto labda wafanye kazi wa kubeba cargo pale swissport.
 
Baada ya miaka kumi utawalipa nini? nani ka kwambia dege kama hilo linalipiwa cash? kwa taarifa yako dege hilo order iliwekwa na Andrew Chenge akaambiwa order imejaa labda waweke mwaka 2018 hapo wanaweza nunua moja.

Hiyo ndege moja mapato yake hatuhitaji kuita wawekezaji yanatosha kabisa, kwanza safari zake zitakuwa New york London Tokyo likija bongo nikubadilisha marubani tu linasonga tena. Qatar ka nchi kama zanzibar wanazo mia sie moja tu kihoro.

Mkuu kwa hio hao wanafunzi waliokosa mkopo wasubiri hilo lidubwana lianze ruti,wapate hela za mkopo?
 
Mkuu kwa hio hao wanafunzi waliokosa mkopo wasubiri hilo lidubwana lianze ruti,wapate hela za mkopo?
jamani mbona mawazo yako mgando wamekosa sio kwa sababu hamna pesa, hawana sifa, jamani mtamzeesha ndalichako kwa kutoa ufafanuzi kila siku, suala la kufaulu ni IQ na IQ haifundishwi ni ya kurithi, mwambie mwanao asiige k kwa tembo, mwambie ajiunge na vikundi vya ujasiliamali sasa hivi machinga hawafukuzwi nae ajiongeze.
 
Wakipata mkopo wakasoma wakahitimu wataajiriwa wapi? tunanunua ndege ili wakihitimu ndio wawe marubani mafundi wa ndege na hata wakifeli basi wawe hata wagawa chai tatizo wanao hawana mvuto labda wafanye kazi wa kubeba cargo pale swissport.

hahahahahahahahahhaha eti wakisoma ndio wawe marubani????Eddy acha utani .....
.........yaani wanafunzi wote hao wawe rubani kwenye hicho kindege kimoja??hizo job opportunities zitakazokuwa created na hio ndege,ambazo ni ndogo,linakua justified na wangapi wangenufaika na kusoma kama wangepata mkopo?

Eddy sio ubishi wa ki JF ,tumsaidie in our best ability Rais wetu,ku allocate resources carefully.
 
Ningependekeza fedha bilioni 600 zitumike katika hili

1. Kuboresha miundombinu ya Dar kwa kujenga barabara za mwendokasi nyingine katika sehem zenye msongamano.

. AU
2. Ningetumia fedha hizo kukopesha vijana wenye mpango mkakati wa biashara kuweza kujiajiri wenyewe.

AU
3. Ningesambaza umeme katika sehem ambazo umeme haujafika

AU
4. Ningesambaza huduma za Maji katika sehem kame

. AU
5. Ningeimarisha shule za msingi kwa kukarabati miundombinu.

Wewe unapendekeza nini?
Bilioni 6 hizo ni investment nzuri tuliyowahi kufanya tangu uhuru.JPM amelenga kukuza sekta ya utalii,sekta ambayo hatujaigusa kabisa,kwa kukata mtu wa kati watalii watakuja kwa wingi,kutakuwa na unafuu wa gharama za matembezi hayo,halafu multiplier effect kwenye ajira na kuongeza ujuzi.
 
hahahahahahahahahhaha eti wakisoma ndio wawe marubani????Eddy acha utani .....
.........yaani wanafunzi wote hao wawe rubani kwenye hicho kindege kimoja??hizo job opportunities zitakazokuwa created na hio ndege,ambazo ni ndogo,linakua justified na wangapi wangenufaika na kusoma kama wangepata mkopo?

Eddy sio ubishi wa ki JF ,tumsaidie in our best ability Rais wetu,ku allocate resources carefully.
Kwa taarifa yako JPM hili kalikuta kwenye drowing table na hili tuliliongelea sana humu, ila sijui umejiunga lini na hili jukwaa, hizi ndege order iliwekwa na Andrew Chenge akiwa waziri wa miundo mbinu na waziri Basil mramba akiwa waziri wa fedha wakaambiwa na boing kuwa order zimejaa hadi 2018 tena wakaruhusiwa kununua moja badala ya tatu walivyokuwa wameomba. Tatizo la nyumbu uwezo wa kufikiri ni mdogo
 
hahahahahahahahahhaha eti wakisoma ndio wawe marubani????Eddy acha utani .....
.........yaani wanafunzi wote hao wawe rubani kwenye hicho kindege kimoja??hizo job opportunities zitakazokuwa created na hio ndege,ambazo ni ndogo,linakua justified na wangapi wangenufaika na kusoma kama wangepata mkopo?

Eddy sio ubishi wa ki JF ,tumsaidie in our best ability Rais wetu,ku allocate resources carefully.
Tatizo lako ni utoto umejiunga humu 4th June 2016, hebu kaa kwanza ujifunze sio kukurupuka tu utadhani umelalia godoro la vitaraha.
 
Baada ya miaka kumi utawalipa nini? nani ka kwambia dege kama hilo linalipiwa cash? kwa taarifa yako dege hilo order iliwekwa na Andrew Chenge akaambiwa order imejaa labda waweke mwaka 2018 hapo wanaweza nunua moja.

Hiyo ndege moja mapato yake hatuhitaji kuita wawekezaji yanatosha kabisa, kwanza safari zake zitakuwa New york London Tokyo likija bongo nikubadilisha marubani tu linasonga tena. Qatar ka nchi kama zanzibar wanazo mia sie moja tu kihoro.
Shirika lenyewe tunaambiwa promotion campaign za ndani wamekodisha gari lenye kipaza sauti eti linaimiza uzalendo wa kupanda ndege na ukute gari lenyewe linazunguka mitaa ambayo probably sio segement inayopanda ndege na pengine wapanda ndege mida hiyo wako makazini.

Isitoshe abiria ndio walioanza na malalamiko ya kukosekana kwa online payments wao ndio wamepiga debe mpaka kuwekwa kwa system ya online.

Utashindana na mashirika yenye wataalamu ambao wakipata info tu zamteja online kwao ni baraka za individual online sales and promotion za kuendelea kupanda ndege zao, kufanya bulk sales, bado ujazungumzia marketing activities zingine.

Embu wacheni kuongea upumbavu ndugu asilimia kubwa ya biashara hufa kwa kuanza bila ya kuwa na plan, huna tofauti na mtu mwenye akili za mhandisi is qualified to run a business organisation. Shirika limekufa kabla alijaanza mwanzo tu unaonyesha linapo elekea.
 
Shirika lenyewe tunaambiwa promotion campaign za ndani wamekodisha gari lenye kipaza sauti eti linaimiza uzalendo wa kupanda ndege na ukute gari lenyewe zinazunguka mitaa ambayo probably. Abiria ndio wanao lalamika kukosekana kwa online payments wao ndio wamepiga debe mpaka kuwekwa kwa system ya online.

Utashindana na mashirika yenye wataalamu ambao wakipata info tu zamteja online kwao ni baraka za individual online sales and promotion za kupanda kuendelea kupanda ndege, kufanya bulk sales, bado ujazungumzia marketing activities zingine. Embu wacheni kuongea upumbavu ndugu asilimia kubwa ya biashara hufa kwa kuanza bila ya kuwa na plan, huna tofauti na mtu mwenye akili za mhandisi is qualified to run a business organization. Shirika limekufa kabla alijaanza mwanzo tu unaonyesha linapo elekea.
hilo gari uliloliona nila crdb ndio wanaotafuta wateja kwa kuzunguka na gari la matangazo, atcl hupati ticket kwa sasa pamoja na mapungufu, leo mwanza dar mwanza 345,000/= hata ukate ticket masaa mawili kabla ya safari. ndege mpya sio hiyo ya kwenu inayodondosha mabegi wakati wa kutua.
 
hilo gari uliloliona nila crdb ndio wanaotafuta wateja kwa kuzunguka na gari la matangazo, atcl hupati ticket kwa sasa pamoja na mapungufu, leo mwanza dar mwanza 345,000/= hata ukate ticket masaa mawili kabla ya safari. ndege mpya sio hiyo ya kwenu inayodondosha mabegi wakati wa kutua.
Mtu mmoja awezi kuwa initiator, user, influencer, decider, buyer and a gatekeeper (serikarini).

Hiyo ni ishara tosha hakuna biashara hapo kama unaelewa majukumu ya hao watu katika organisation purchasing behaviour; ndio maana mzungu wa Boeing alishindwa kujizuia na tabasamu jinsi akili za wa afrika zinavyotutosha wenyewe na maamuzi yetu ya kibiashara yalivyokuwa rahisi. Hayo yanafanyika wakati raisi anajivunia publicly ame negotiate deal ya ndege that is not how business buying decisions are made.

Utaishia kunijia na viroja badala ya hoja stick na kazi ya debe haya sio ya uwezo wako.
 
Kwa taarifa yako JPM hili kalikuta kwenye drowing table na hili tuliliongelea sana humu, ila sijui umejiunga lini na hili jukwaa, hizi ndege order iliwekwa na Andrew Chenge akiwa waziri wa miundo mbinu na waziri Basil mramba akiwa waziri wa fedha wakaambiwa na boing kuwa order zimejaa hadi 2018 tena wakaruhusiwa kununua moja badala ya tatu walivyokuwa wameomba. Tatizo la nyumbu uwezo wa kufikiri ni mdogo

MMNh hata kama hii order iliwekwa zamani...

imekuja kutekelezeka Enzi za serikali hii...

Hivyo tunayemlaumu ni huyu,kuwezesha hili jambo...

afu acha matusi ya reja reja,wewe kukaa kwako JF muda mrefu sio sababu ya kukebehi members wapya
 
Back
Top Bottom