Ungefanya nini ukijua unakufa kesho ?

Ungefanya nini ukijua unakufa kesho ?

Ningetumia huo muda uliobaki kula bata la kifahari na watoto wangu hadi muda ninaoondoka duniani.
 
NINGEFANYA SHEREHE YA kuwaaga wote wanaobaki FAREWELL, ningetumia fursa hii kujipongeza kwa wakati nilioishi, kuwaaga wanaobaki, kuwaomba msamaha. Alieangalia LOVE AT FIRST SIGHT(2023) atanielewa.
 
Kifo ni ukumbusho wa jinsi tulivyo dhaifu, na kwamba kila kitu kinaweza kuondoka kwa sekunde.

Hofu zako zote hizo - wale wanaokuzuia: hofu ya kukataliwa, kuchekwa, kutengwa; - haimaanishi chochote unapoongeza kifo kwenye fomula.

Ungefanya nini, ikiwa ungejua utakufa baada ya saa chache?

Ulimwambia huyo binti unampenda?

Kwa sababu hayo hayapaswi kuogopwa tena.

Kifo huweka mambo yote sawa.

Kila kitu kingine kisichokuwa kifo kinakuwa kitu kidogo tu.

Ungefanya nini ikiwa ungejua utakufa wiki ijayo?

Ungefanya nini ikiwa ungejua utakufa kesho?

Ungefanya nini ikiwa ungejua utakufa mwezi ujao?

Naam. FANYA HIVYO, SASA.

Ishi, wakati bado unaweza.
Kwa mujibu WA Imani yangu Mimi na yako pia ewe msomaji,ikitoke mmoja wenu akafa,akapewa dakika kumi kurudi duniani arudi Tena kaburini,atakachokimbilia kukifanya ni kutoa SADAKA.

SADAKA si pesa TU,ondoa vitu vinavyokera njiani,,,,
 
Pesa zangu chukueni
Mtu mmoja anasemaga siku uliyozaliwa ndipo ulipoanza kufa.So best kujiandaa sababu kila siku unazidi kupunguza siku zako za kuishi unaelekea kufa. Hata kama utaishi miaka mia ila utakufa tuu.Hata wale waliokuja na kikokotoo cha pension akilini mwao ni lini mstaafu atakufa.

Kwa kuwa kinachokufa ni mwili roho kuna mahali inaenda.ni mhimu kuhakikisha unaiandaa ili kusudi iende mahali unapoona patakuwa panafaa kwako
 
Kutubu, kujaribu kuwaelewesha wanangu kwamba hawataniona tena (hapa ndo nachanganyikiwa kabisaaa
 
Fanya hivyo sasa
Ni kweli kabisa tusi subiri kufa ILA. Ukiona BADO unaishi basi jipange kupokea maadui wapya KILA ujuanapo na WATU NDO maisha yalivo ukifanya SASA basi UWE utamaduni WAKO KILA SIKU MANA Leo utakorofishana na WATU utaomba msamaha KESHO TENA uyazinguana NAO mkuu. Kula na watoto yatima tunapenda ILA hatuna hicho kipato mkuu tavanyaje SASA Bora nijue nakufa KESHO tauza mali ZANGU zingine ILI nikamilishe Hilo SWALA man Sito KUEPO TENA.


Kwishaaaaa


Bro Alex on da beats yoow
 
Ningewasiliana na wale ninaowapenda – kusema “nakupenda,” “asanteni,” na kusamehe au kuomba msamaha pale panapostahili. Siache lolote moyoni.

Ningetumia muda wangu kwa utulivu na uzuri – pengine ningeenda mahali penye amani labda ufukweni

Ningeandika ujumbe wa mwisho – maneno machache ya kuacha urithi wa mawazo yangu, upendo wangu, na matumaini yangu kwa waliobaki.
 
I would have talk to my kids niwahusie juu yakufanya ibada,kua watu wema nakuhakikisha wakati ukifika wanaoa wanawake wacha Mungu ambao pia wamelelewa katika familia zenye maadili na kujenga familia nzuri yenye amani upendo etc
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom