Unene sio sifa ni ugonjwa, kwa hii speed NHIF itaelekea kubaya. Tubadilike

RNA

JF-Expert Member
Mar 27, 2013
1,584
2,683
Habari wana JF, Kadri siku zinavyozidi kwenda watu wenye uzito ulipitiliza wamekuwa wakiongezeka kwa kasi sana. Kwa Nchi za wenzetu wanauchukia sana unene kutoka na athari zake lakini cha kushangaza Tanzania ni Tofauti mtu anaponenepa hupewa sifa nyingi sana ikiwemo kuonekana maisha ameyapatia.
Kwa kifupi ukiwa na uzito mkubwa kupitiliza unakuwa kwenye Hatari zaidi kuliko mwenye uzito wa kawaida ya :-

1. Kupata kisukari

2. Kupata Magonjwa ya Moyo

3. Kupata shinikizo la damu -pressure

4. Kupata kansa mbali mbali

5. Kupata maumizi ya Muda mrefu ya Mgongo ,Magoti na visigino vinavyoweza kuambatana na Ganzi au la

6. Tafiti pia zinaonyesha wanawake wenye uzito mkubwa hupati shida kubeba ujauzito sababu ya kutobalance kwa hormone .
...na mengine mengi .

Hayo Magonjwa hapo Juu ni magonjwa ambayo siyo ya kuambukiza na Ndiyo magonjwa yanayoongoza kwa kuwa na gharama kubwa za matibabu hususani gharama kubwa za Dawa ,Je kwa hii kasi NHIF itatoboa ?

Kama una miaka chini ya 60 na hujui uko kundi lipi hebu chukua peni na karatasi fanya hesabu hii

BMI(Body Mass Index )=Uzito(kg)/(Urefu katika mita)^2

Yaani chukua uzito wako katika Kilogram gawa kwa kipeo cha pili cha urefu wako katika mita .Mfano ukiwa na kilo 60 na urefu wa sentimita 165 itakuwa hivi BMI =60/(1.65)^2 utapata 22.03.. .

Jibu utalopata angalia maelezo hapa
¡. 18.5-24.9 uzito wako unaendana na mwili .

¡¡.25-29.9 Uzito wako umezidi jitathmini

¡¡ .30 na kuendelea uzito wako ni mkubwa sana fanya jitihada uupunguze .

Tusisifiane wakati tunakaribisha shida siku kukutana na mtu ana pressure na magonjwa ya moyo katika umri wa miaka 30-40 ni imeongezeka sana Garama za haya magonjwa kila mwezi ni kubwa kasi ikiwa kubwa sana huu mfuko wa bima wa Taifa Utalemewa labda tukibadilika kuna Baadhi ya gharama zitapungua.
 
Acha kutuongopea wewe Marekani ni mojawapo ya nchi zinazoongoza kwa obesity sababu ya maisha mazuri Wana uhakika wa kula vizuri ndo maana.

We Tanzania hii njaa kali halafu unatuongopea kula yao watu shida.
 
Acha kutuongopea wewe Marekani ni mojawapo ya nchi zinazoongoza kwa obesity sababu ya maisha mazuri Wana uhakika wa kula vizuri ndo maana.
We Tanzania hii njaa kali halafu unatuongopea kula yao watu shida.
Marekani watu wanaongoza kwa unene ni Maskini sana vyakula vingi vinavyoongeza unene kule ni bei rahisi
 
Marekani watu wanaongoza kwa unene ni Maskini sana vyakula vingi vinavyoongeza unene kule ni bei rahisi
Kule mzee baba masikini hawazi kula mzee Kama huna uwezo Kuna food banks ambazo ni Kama charity zina provide misosi......kawaongopee wajingawajinga lakini sio wakina ss
 
Acha kutuongopea wewe Marekani ni mojawapo ya nchi zinazoongoza kwa obesity sababu ya maisha mazuri Wana uhakika wa kula vizuri ndo maana.
We Tanzania hii njaa kali halafu unatuongopea kula yao watu shida.
Hao wenye obesity wengi wao wanakula vibaya(wewe unaweza kuona ndio vyakula vizuri), junk food.
 
Mtoa Mada Yuko sahihi kabisa ..Tatizo tunaona watu wanatembea wanene tunaona hamna shida ..pata muda nenda hospital zetu utagundua Hali si njema.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: RNA
Elimu Elimu Elimu juu ya Lishe ni tatizo.
- Chips Yai, Na soda pembeni mlo tayari
 
  • Thanks
Reactions: RNA
Kuna mtu ni mwembamba hajawahi kuwa mnene ila ana kisukari huu mwaka wa 20+.
Magonjwa yoyote anaweza kuyapata

Unajibana kula kuogopa unene unakuja kugongwa na bodaboda unakufa.
 
Hao wenye obesity wengi wao wanakula vibaya(wewe unaweza kuona ndio vyakula vizuri), junk food.
Achageni ushamba wao wanakula vibaya ok sawa. Sasa we mbegu za ugali wako wa mahindi unao kula au alizeti zinatoka wapi bwana.
 
Usipokufa kwa unene utakufa kwa ajari. Isipokua ajari basi utakufa kwa kuuwawa. Wacha watu wafurahie uhai yajayo ni matokeo.
 
Back
Top Bottom