Unazikabili vipi changamoto za choo cha kukaa?

Unazikabili vipi changamoto za choo cha kukaa?

Kama inavyojieleza hapo juu, ni wiki sasa nimepata kazi katika taasisi fulani, ila sasa tatizo ni kwamba hapa kuna vyoo viwili cha kawaida na cha kukaa. Natamani sana kujua namna ya kutumia hiki cha kukaa maana sielewi baada ya kunanihino unatawadha vipi?

Je, unasimama kwanza halafu maji yataenda wapi sasa au unabaki umekaa tu pale?? Yaani nimeumiza kichwa sana ni manuva gani yanatumika kujiswafi baada ya kujisaidia.

Tuelekezane.
 
Vyoo vya kukaa sehemu ya watu wengi sikushauri...yafaa mtumie wachache,favorable zaidi mkiwa wawili
Kujiswafi kunakuwa na Bomba la maji pembeni na tissue, huna haja ya kusimama unakaa unamaliza yote,anza na tissue maji af tissue mwishoni
 
kama inavyojieleza hapo juu,ni wiki sasa nimepata kazi katika taasisi fulani,ila sasa tatizo ni kwamba hapa kuna vyoo viwili cha kawaida na cha kukaa,natamani sana kujua namna ya kutumia hiki cha kukaa maana sielewi baada ya kunanihino unatawadha vipi,unasimama kwanza halafu maji yataenda wapi sasa au unabaki umekaa tu pale??,,,,yaani nimeumiza kichwa sana ni manuva gani yanatumika kujiswafi baada ya kujisaidia.

tuelekezane.
Mind-how-you-go-Toilet-sign-advises-on-how-to-poo-312554.jpg
 
Hizi topic za vyoo vya kukaa zimekuwa nyingi siku hizi. Hivi vyoo mbona vilikuwepo siku nyingi? Tena sehemu za public kama maofisini,hotels etc.
 
Vyoo vya kukalia ni tamaduni. Nimetembelea nchi za kiarabu nyingi unakuta toilet paper na kibomba maalumu chenye maji ya pressure unajisafisha au unaweza tumia toilet paper. Ulaya sehemu kubwa ni toilet paper, hawana kama arabuni maji au kibomba chenye pressure, nadhani ni kutokana na baridi, it might too expensive kuchemsha maji ya kutawazia, wakati arabuni no need to kuchemsha maji. Hivyo kama kuna toilet paper tumia. Niliwahi kuwa na mgeni alikaa almost 2 weeks anaenda kujisaidia buguruni, mpaka akaja kumuuliza kijana wangu ndiyo akaanza kutumia.
 
Umenikumbusha mbali sana nikiwa mdogo tumezoea vyoo vya shimo..sasa siku tumeenda kula ckukuu kwa ndugu zetu walikua na nyumba ya kisasa miaka ya90 nikaomba kwenda chooni nikaoneshwa mlango..kufika nakuta choo cha namna hiyo aisee nilisimama pale lisaa najiuliza nafanyaje..kilichonibabaisha ni yale maji nilivokua nayaona nikawa naogopa kuyachafua.. Nilitoka tu bila kufanya lolote giza lilipoingia nikatafuta kichaka nikapata kwenye maua nikamaliza.. Asubuhi lazma waliisoma namba kuzoa
 
Umenikumbusha mbali sana nikiwa mdogo tumezoea vyoo vya shimo..sasa siku tumeenda kula ckukuu kwa ndugu zetu walikua na nyumba ya kisasa miaka ya90 nikaomba kwenda chooni nikaoneshwa mlango..kufika nakuta choo cha namna hiyo aisee nilisimama pale lisaa najiuliza nafanyaje..kilichonibabaisha ni yale maji nilivokua nayaona nikawa naogopa kuyachafua.. Nilitoka tu bila kufanya lolote giza lilipoingia nikatafuta kichaka nikapata kwenye maua nikamaliza.. Asubuhi lazma waliisoma namba kuzoa
mkuu siku ingine panda pale juu afu chuchumaa ila kuna jamaa yangu alipanda akavunja
 
Mkuu wakijibu kiufasaha na mimi watakuwa wamenisaidia. Nikionaga choo cha hivyo naahirisha issue yote nitatafta namna sehemu nyingine
 
Kwanza kabisa kisafiche kabla ya kutumia na flush hata kama kianaonekana kisafi.
Ukiangalia hicho choo utagundua kuna mifuniko miwili mmoja hufunika kabisa na kingine kina uwazi katikati, kwa mwanaume unapandisha au una vi inua vifuniko vyote ndio unaka,Kwa mwanamke ana kalia hicho kimfuniko kilicho na nafasi kati kati kwani humsaidia pindi anapotoa haja ndogo mkojo usi ruke kwa juu hiko kimfuniko ndiko kina zuia.
Ukitumuia hiko kimfuniko kikiwa hujakifungua una hatari ya kupata magonjwa kwani Uume wako utakuwa unagusa sehemu ya mbele ya huo mfuniko ambapo kama alikitumia mwanamke lazima ukiangalia kwa chini ya mfuniko utakuta mabaki ya mkojo, kwa mwanaume unafungua mifuniko yote ndio unakaa hapo hata umme wako hauwezi kugusa sehmu ya mbele.

Kwenye kuji safisha baada ya haja kubwa pembeni kwa hizi choo huwa kuna Mpira unaitwa Muslim pipe una hamishika uko flexible una upeleka nyuma unajitawadhaa huku unakuwa kama ume inama kwa mbela au unalaia tumbo ( kwa mwanamke una utumia kwa mbela kwani ukiutumia kwa nyuma utapata UTI) kwa mwanaume unaweza tumia either way hats ukiwa na toilet paper.
Ukimaliza una flush kwa kubonyeza handle ya choo hadi chini ili maji yatoke yote. Kwa mwanamke unapaswa unanyue juu mifuniko yote kisha mwagia maji sehmu ya mbele ya mfuniko Wa kati ili kutoa mabaki ya mkojo
 
Mzee vyoo vya kukalia vya public vingi vinakuwa vibovu, ila ukikuta vizima pale kwa juu kuna kijikamba unakivuta, au vingine kuna sehemu unabonyeza basi automaticaly choo kinajiflashi,
 
Kwanza kabisa kisafiche kabla ya kutumia na flush hata kama kianaonekana kisafi.
Ukiangalia hicho choo utagundua kuna mifuniko miwili mmoja hufunika kabisa na kingine kina uwazi katikati, kwa mwanaume unapandisha au una vi inua vifuniko vyote ndio unaka,Kwa mwanamke ana kalia hicho kimfuniko kilicho na nafasi kati kati kwani humsaidia pindi anapotoa haja ndogo mkojo usi ruke kwa juu hiko kimfuniko ndiko kina zuia.
Ukitumuia hiko kimfuniko kikiwa hujakifungua una hatari ya kupata magonjwa kwani Uume wako utakuwa unagusa sehemu ya mbele ya huo mfuniko ambapo kama alikitumia mwanamke lazima ukiangalia kwa chini ya mfuniko utakuta mabaki ya mkojo, kwa mwanaume unafungua mifuniko yote ndio unakaa hapo hata umme wako hauwezi kugusa sehmu ya mbele.

Kwenye kuji safisha baada ya haja kubwa pembeni kwa hizi choo huwa kuna Mpira unaitwa Muslim pipe una hamishika uko flexible una upeleka nyuma unajitawadhaa huku unakuwa kama ume inama kwa mbela au unalaia tumbo ( kwa mwanamke una utumia kwa mbela kwani ukiutumia kwa nyuma utapata UTI) kwa mwanaume unaweza tumia either way hats ukiwa na toilet paper.
Ukimaliza una flush kwa kubonyeza handle ya choo hadi chini ili maji yatoke yote. Kwa mwanamke unapaswa unanyue juu mifuniko yote kisha mwagia maji sehmu ya mbele ya mfuniko Wa kati ili kutoa mabaki ya mkojo.

Mkuu maelezo yako mazuri ila hapo kwenye kutawaza mbona kama mtihani
 
PALE UDSM MAIN CAMPUS CJUI KM KUNA MTU ANAKALIAGA VILE VYOO. MIAKA MITATU MIE NILIKUA NI KUJIPANDIA JUU TU KM NYAN VILE.
 
Ushauri wangu ni kuwa aliejenga hilo jengo usimdharau, alijua wapo wasioweza kutumia vyoo hivyo na ndio maana wakakuwekeeni na chakawaida, hivyo basi kujiepusha na fedheha bora uendelee na hicho hicho ya kawaida maana utakuwa umeepuka mengi (including magonjwa) jidai mshamba tu wala hainaga ujuaji.. Nahisi kuna sehemu niliwahi kusikia mtu akisema "IGNORANCE IS BLISS" sikumbuki ni wapi
 
Umenikumbusha mbali sana nikiwa mdogo tumezoea vyoo vya shimo..sasa siku tumeenda kula ckukuu kwa ndugu zetu walikua na nyumba ya kisasa miaka ya90 nikaomba kwenda chooni nikaoneshwa mlango..kufika nakuta choo cha namna hiyo aisee nilisimama pale lisaa najiuliza nafanyaje..kilichonibabaisha ni yale maji nilivokua nayaona nikawa naogopa kuyachafua.. Nilitoka tu bila kufanya lolote giza lilipoingia nikatafuta kichaka nikapata kwenye maua nikamaliza.. Asubuhi lazma waliisoma namba kuzoa
 
Hizi topic za vyoo vya kukaa zimekuwa nyingi siku hizi. Hivi vyoo mbona vilikuwepo siku nyingi? Tena sehemu za public kama maofisini,hotels etc.
Jamani tuwe tunajibu kikamilifu kama GT's. Mtu kauliza matumizi, hajauliza vilianza kutumika lini.
Jibu ni kwamba? Toilet paper ni kitu cha msingi sana kwenye mavyoo "kabila" hiyo.
Unapomaliza kujisaidia unachana toilet paper unaitumia kama kifungua kinywa ukiwa hapohapo. Halafu unapoteremka ndiyo unatawadha.
Uzuri wa vyoo hivyo, ni muarobaini sana kama unamatatizo ya miguu pamoja na uzee, halafu ni "sound proof", yaani hata mtu awe yupo hatua "0" hawezi kusikia madudu unayoyafanya hata kama unatumbo la kuendesha. Na ukivizoea unalemaa. Ni vizuri mno kuliko maelezo niliyokupatia. Ndiyomaana hata kwenye maduka ya ujenzi vinauzwa bei mbaya.
 
Yani uweke makalio sehemu wengine wameweka makalio yao?hapo ndo siwezi.alafu ukitoa haja kubwa ikishuka Yale maji ndani ya choo yanakurukia sometimes.
 
mkuu siku ingine panda pale juu afu chuchumaa ila kuna jamaa yangu alipanda akavunja
Hiyo "staili" usijaribu tena mkuu kwani ni hatari sana! Choo kinaweza kuvunjika halafu kikakukata kama umekatwa na Kisu na kukutia kilema cha maisha! Hizi ajali za namna hii zimetokea sana tu,Choo cha kukaa unatakiwa ukae,kuchuchumaa ni risk na ni hatari sana!
 
Huwa nikikutana na vyoo vya kukaa natandika toilet paper kwanza ndio nakaa
Yani uweke makalio sehemu wengine wameweka makalio yao?hapo ndo siwezi.alafu ukitoa haja kubwa ikishuka Yale maji ndani ya choo yanakurukia sometimes.
 
Back
Top Bottom