Unawafahamu wanawake wa Amazon?

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,686
106,811
Umewahi kuitazama muvi ya Wonder Woman iliyochezwa na mwadada Gal Gadot? Ni muvi inayohusu wanawake Fulani wanaofahamika kama Amazon Women.

images - 2023-04-26T155210.375.jpeg


Kwa mujibu hadithi za uhiriki (Greek mythology) zinasema kwamba Amazon Women walikua ni jamii ya wanawake ambao walikua hatari sana katika medani za kivita. Walikua wana nguvu hawakua wakiishi na wanaume bali walikutana na wanaume mara moja tu kwa mwaka ambapo walitumia nafasi hiyo kubeba mimba, kama mtoto alipatikana mwanaume basi walimrudisha kwa baba zao na kubaki na watotoo wa kike tu amabao waliwafundisha na kuwaandaa kua wapambanaji.

Wanawake hawa walisifika kwa kupiga mishare na kuendesha farasi, walikua na tabia ya kukata maziwa yao ndio maana walikua hodari katika kupiga mishale, Kwakua walikua wanawake watupu inasemekana hawa walikua hodari wa kusagana pia…lakini pia kwa makabila mengine ya hawa Amazonian walikua na tabaia ya mwanamke mmoja kua na wanaume hadi wanne.

Kuna jamaa mmoja kutoka Hispania anaitwa Francisco de Orellana alikua anafanya uchunguzi wake huko kwenye mssitu wa brazil, alipokua kwenye mto mkubwa unaopatikana katika msitu huo alikutana na jeshi la wanawake watupu wakiwa kando yam to huo. Hivyo akauita mto huo Amazon kutokana na wanawake hao walifanana na wale wanawake wa kwenye simulizi za kigiriki. Lakini pia hata msitu huo ulianza kufahamika kama Amazon kutokana na jina la mto huo…na hicho ndio kikawa chanzo cha msitu mkubwa duniani uliopo Brazil kuitwa Amazon.

images - 2023-04-26T155736.905.jpeg


[Amazon women as depicted in Wonder Woman film]

Katika karne ya 17 huko Africa magharibi kulikua na falme iliyojulikana kama Kingdom Of Dahomey ambayo kwa sasa inafahamika kama Benin, ilikua falme yenye nguvu sana kutokana na biashara ya mafuta ya mawese na biashara ya watumwa. Walipa wazungu watumwa wao wakapewa bunduki, vioo, nk. Falme hii ilikua ina jeshi la wanawake watupu ambao walikua imara kwelikweli na wapiganaji mashuhuli waliojulikana kama Dahomey.

Kikawaida tamaduni za kiafrika tunamchukulia mwanamke kama kiumbe duni na dhaifu, ilikuaje wanawake wakaingizwa jeshini? Kutokana na vita mbalimbali zilizokua zikitokea baina ya falme na falme zilipelekea wanaume kupungua pia wanaume wengi waliuzwa kama watumwa hivyo population ya wanaume ikawa ndogo. Ndio hapo wafalme wa falme ya Dahomey wakaanza kuchukua wanawake na kuwatumia kama wanajeshi wake. Jeshi hilo la wanawake watupu lilijulikana kama Agojie, unaambiwa walikua ni hatari sana kwenye mapigano..Wazungu walipowaona wakawapa jina la Dahomey Amazons

wakiwalinganisha ushupavu wao na wale wanawake kutoka kwenye hadithi za wagiriki. Dahomey ilikuja kuanguka mwaka 1890 kwenye vita iitwayo Franco-Dahomenian war ambapo falme hii ilipoteza ushindi kwa mfaransa na kuchukuliwa kama koloni la ufaransa. Baadae ilikuja kupata uhuru mwaka 1958 ikajiita Republic of Dahomey….mwaka 1975 ilijibadirisha jina na kujiita Benin.

images - 2023-04-26T160240.010.jpeg

[The real Agojie from Benin]

Mwaka 2015 Producer wa muvi za Hollywood Maria Bello alitembelea nchi ya Benin akakuta simulizi zinazowahusu hawa wanawake Agojie kwenye makumbusho akatamani sana stori hizo zitengenezewe muvi. Akarudi kwenye los angels akaanza kutafuta studio ambazo zitasapoti kutengeneza muvi kuhusu wanawake hao…studio ya STX ilitaka kutoa million 6 kama bajet ya muvi ila akakataa kwa kuona bajeti ndogo akapeleka idea yake kwenye studio zingine ila wakakataa kudhamini kutengeneza muvi hiyo.

images - 2023-04-26T150958.327.jpeg


Mwaka 2018 ilipotoka muvi ya Black Panther ikapata mafanikio makubwa kifedha ukizingatia zilikua ni stori za kubuni tu, Maria akapata moyo wa kuendelea kutafuta studio itakayodhamini ndipo kampuni ya Tristar zikapata moyo na kudhamini muvi itengenezwe……Rupita Nyong’o na Viola Davis ndio walitakiwa wawe masterling wa muvi lakini Lupita akatolewa na kuwekwa pisikali Thuso Mbedu.

November 2021 wakaelekea south Africa kwa ajili ya kushoot kwa miezi mitano, asilimia kubwa ya Crew ilikua na wanawake Zaidi maana walitaka muvi iwe kiFeminine Zaidi ukizingatia Producer Maria Bello ni Lesbian wa muda mrefu, Hatimae muvi ikatoka September 2022 ikapwa jina la THE WOMAN KING.

images - 2023-04-26T150851.702.jpeg


Wakati Stan Lee anatengeneza jeshi la wanawake watupu wa Dora Milaje kutoka kwenye comics za Plack Panther aliwatengeneza Dora milaje kutokana na simulizi za jeshi la wanawake watupu la agojie kutoka Benin…Ila akawafanya Dora milaje wawe wanafanana na wamasai maana Wakanda ni nchi iliyopo Afrika Mashariki. Ndio maana kama umetazama muvi ya Black Panther 1&2 utaona kua jeshi la Dora milaje wanavaa kama wamaasai.

6019905d40b2d6787c43e5ef_john-mcarthur-Ue5kuMVmIhU-unsplash.jpg

[Maasai Women from Tanzania]

images - 2023-04-26T190507.401.jpeg

images - 2023-04-26T190439.134.jpeg

[Dora Milaje Warriors from Black Panther]

Da’Vinci
 
Amazon Woman japo ni miaka 3 toka nilipotoa ahadi hii ila nikiahidi kitu hua natimiza no matter muda gani utapita coz I don't forget my promises.
I hope you'll like it ✌️
Cc
Ryan Holiday
images - 2023-04-26T155053.550.jpeg
images - 2023-04-26T151745.460.jpeg

I'm writing something about them..
Amazonian

Amazon woman is a healthy strong woman and powerful. The name I got it from Greeks mythology, these were war warriors fight like men, the spirit and so and so..

I chose this because it portrays some of my characters. Leave aside the lesbianism they had and culture ya kukata maziwa (breasts) Tell me more about it!!
 
Asante mkuu.

Naomba kuuliza,

Hivi haya tunayoita Mavazi ya Kimasai, hawa wamasai walianza kuyavaa kipindi gani?

Maana mengi naona ni Made in China. Sasa huwa najiuliza walikuwa wanatengeneza wenyewe Fabrics zao au ilikuwaje kuwaje?
Sir niliuliza wahusika waliniambia walikuaa wanavaa ngozi.
Ngoja nimwite mkuu The Boss natumaini atakua anajua zaidi.
 
Back
Top Bottom