Ripoti: Idadi Ya Wabunge Wanawake 2023 iliongezeka

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,616
Muungano wa Wabunge duniani (UIP) unasema wanawake wameongozeka katika bungu kwa mwaka 2023 ambapo wanawakilisha ongezeko la asilimia 0.4 mwaka baada ya mwaka, kiwango sawa cha ukuaji kwa mwaka 2022. Hata hivyo, ukuaji huo ni wa polepole kuliko miaka iliyopita kwani chaguzi za 2021 na 2020 zilishuhudia ongezeko la asilimia 0.6 ya wabunge. Ripoti ya UIP inasema masuala ya kijinsia yalitawala chaguzi nyingi huku kukiwa na upinzani dhidi ya haki za wanawake katika baadhi ya nchi. Ripoti hiyo pia inaeleza kuwa wanawake kadhaa mashuhuri wameacha siasa hivi karibuni, wakilaumu uchovu na vitisho. Ripoti hiyo ya IPU inatokana na marekebisho yaliyofanywa na bunge katika mabunge 66 kwenye nchi 52 mwaka 2023. Wanawake walikuwa asilimia 27.6 ya wabunge katika mabunge hayo mapya yaliyochaguliwa au kuteuliwa, ikiwa ni ongezeko la jumla la asilimia 1.4 ikilinganishwa na kura za awali katika nchi hizo hizo.

Nyanja zilizopiga hatua

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya UIP kulikuwa na maendeleo makubwa katika baadhi ya maeneo, kwa mfano: Katika bara la Amerika, wanawake walichangia asilimia 42.5 ya wabunge wote waliochaguliwa au kuteuliwa katika mabunge ambayo yalichaguliwa upya mwaka wa 2023, asilimia kubwa zaidi ya kikanda. Kwa hivyo kanda hiyo inashikilia nafasi yake ya muda mrefu kama eneo lenye uwakilishi wa juu zaidi wa wanawake duniani, kwa asilimia 35.1. Ulimwenguni kote, sehemu ya Maspika wanawake wa mabunge iliongezeka hadi asilimia 23.8 ikiwa ni ongezeko la asilimia 1.1. Cambodia na Ivory Cost zilichagua Maspika wanawake kwa mara ya kwanza. Viwango vilivyoundwa vyema na kutekelezwa vinaendelea kuwa jambo muhimu katika kuongeza uwakilishi wa wanawake. Mabunge 43 ambayo yalikuwa na aina fulani ya viti maalum yalichagua wabunge wanawake asilimia 28.8 kwa wastani, dhidi ya asilimia 23.2 katika nchi ambazo hazina.

Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara

Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa mujibu wa Muungano Mabunge duninai(UIP) unasema ulirekodi uboreshaji wa juu zaidi kati ya kanda zote na ongezeko la asilimia 3.9 katika chaguzi za mwaka 2023 ikilinganishwa na kura za awali katika nchi hizo hizo. Mafanikio makubwa zaidi yalikuwa nchini Benin, Eswatini na Sierra Leone, yakiwezeshwa na nafasi za upendeleo. Rwanda inaendelea kuongoza katika orodha ya kimataifa ya IPU huku wanawake wakichukua asilimia 61.3 ya viti katika Baraza la Manaibu, ikifuatiwa na Cuba na Nicaragua zenye asilimia 55.7 na 53.9 mtawalia, huku Andorra, Mexico na Umoja wa Falme za Kiarabu zikiwa na usawa.

Masuala ya jinsia yanatawala katika baadhi ya chaguzi

Ripoti ya IPU inabainisha kuwa masuala ya kijinsia mara kwa mara yaliibuka kama mazungumzo muhimu wakati wa uchaguzi mwaka 2023, hasa haki za uzazi za wanawake katika nchi ambapo utoaji mimba unasalia kuwa suala la kutatanisha. Katika uchaguzi wa Poland, suala hilo lilikuwa kuu baada ya uamuzi wa mahakama wa 2020, ulioungwa mkono na serikali wakati huo, ambao ulizuia vikali fursa za utoaji mimba. Uamuzi huo ulifuatiwa na maandamano makubwa kote nchini, yakiongozwa na wanawake na vijana. Ripoti hiyo inadokeza kuwa hii ni sababu mojawapo iliyopelekea chama tawala kupoteza madaraka. Kwa upande mwingine, Javier Milei, ambaye aliahidi kura ya maoni kufuta sheria zinazoendelea zaidi za utoaji mimba ambazo ziliwekwa mwaka wa 2020, alichaguliwa kuwa Rais wa Argentina. Lakini hata hivyo kwa sasa kuna habari nyingine mpya yenye mashaka ambayo Bunge la Ufaransa limepitisha sheria yautoaji mimba.

Chanzo: Vatcan News
 
Back
Top Bottom