Black Opal
Senior Member
- Jan 22, 2023
- 199
- 257
Habari Wakuu,
Chapati za kusukuma ni pishi ambalo limekuwa changamoto kwa watu wengi, mtu anajitahidi alkini mwisho wa siku anatoa chapati ngumu na imesimama kama sinia😂🤣.
Mbinu ninayotumia mimi kufanya chapati iwe ni laini, ni kukanda unga na kuhakikisha umekuwa laini kabisa. Tumia hata muda mrefu kama huna nguvu sana mikononi ila hakikisha donge lako linakuwa laini kabisa. Na kipindi unakunja mwanzo fanya iwe nyembamba sana kama karatsi, muda wa kusukuma ili uchome iwe wastani, isiwe nene sana haitaiva na isiwe nyembamba sana itakua kaukau.
Pia wakati wa kuchoma, kama umeweka chapati kwenye kikaango na haifuri jua kuna kitu umekosea, inaweza kuwa hujakanda unga vizuri au umeweka nene.
Lete maujuzi yako mpishi, unatumia njia gani kufanya chapati yako inakuwa laini?
Chapati za kusukuma ni pishi ambalo limekuwa changamoto kwa watu wengi, mtu anajitahidi alkini mwisho wa siku anatoa chapati ngumu na imesimama kama sinia😂🤣.
Mbinu ninayotumia mimi kufanya chapati iwe ni laini, ni kukanda unga na kuhakikisha umekuwa laini kabisa. Tumia hata muda mrefu kama huna nguvu sana mikononi ila hakikisha donge lako linakuwa laini kabisa. Na kipindi unakunja mwanzo fanya iwe nyembamba sana kama karatsi, muda wa kusukuma ili uchome iwe wastani, isiwe nene sana haitaiva na isiwe nyembamba sana itakua kaukau.
Pia wakati wa kuchoma, kama umeweka chapati kwenye kikaango na haifuri jua kuna kitu umekosea, inaweza kuwa hujakanda unga vizuri au umeweka nene.
Lete maujuzi yako mpishi, unatumia njia gani kufanya chapati yako inakuwa laini?