Unataka kuolewa mdada umejipanga?

Unataka kuolewa mdada umejipanga?

Haswaa.Mimi sitaki kumpangiamtu maisha kama nisivyotaka kupangiwa maisha mimi.

Do unto others as you would have them do unto you. That is a golden rule.
Kwa kweli mtu maisha yake tu yanamshinda, ila kwa kupangia wenzake sasa teh. Hiyo mipango si atumie kwake
 
Wakati mwingine huwa naona fikra na mitazamo yangu haiendani kabisa na mitazamo na tamaduni za Kitanzania.

Maana...kama watu ni mashoga huwa sijali kama hawaingii kwenye anga zangu....wasiotaka kuwepo kwenye ndoa huwa nawaelewa na wala huwa siwahukumu....na kwa ujumla huwa sijali sana namna ambavyo watu wengine huamua kuishi watakavyo.

Inaweza kusikika au kuonekana vibaya lakini huwa naona kama vile nilizaliwa kwenye hii jamii kimakosa!!!
Mkuu hiyo ni athari ya mazingira aliyekulia mtu yeyote. Sio chaguo lako kuwa kama ulivyo bali ni mazingira yako.
 
Mwanamke unajiweka tayari sawa!! Sasaaaaa hao the so called waume duuuh!! Bora waanze kujiandaa wao kwakweli.
Wanaume nao wamegawanyika hivyohivyo, waoaji na wachezaji. Wachezaji huwa ni vigumu sana kutua kwenye viwanja vya waolewaji labda kama muolewaji yuko mguu pande kwenye suala la ndoa. Mada imefafanua vizuri upande wa wadada.
 
Mkuu hiyo ni athari ya mazingira aliyekulia mtu yeyote. Sio chaguo lako kuwa kama ulivyo bali ni mazingira yako.

Sasa mimi mbona nimekulia hapa hapa bongo?

Tokea zamani nikiwa mtoto mdogo kabisa nilikuwa tofauti. Nilikuwaga nabishana sana na watoto wengine kuhusu mambo kibao tu.

Nakumbuka wakati flani hivi nilibishana na mtaa mzima kuhusu jina la Bruce Lee.

Mimi nilikuwa nasema hilo jina ni la Kimagharibi wao wanasema ni la Kichina kisa tu aliyekuwa anaitwa hivyo alikuwa na asili ya Kichina.

Unaweza kuniambia nani alikuwa sahihi hapo?
 
Back
Top Bottom