Unataka kuagiza gari??... pitia hapa kwanza

hlw sis!
unajua kwanza watu wengi wanachanganya kuna toyota NOAH na kuna toyota litehiace NOAH. but kwa upeo wa haraka haraka nishajua unayoitaka wewe. ukiitaka gari hiyo andaa milioni 5.5 mpaka 6.5 kutegemea na options kama vile alloy rims, cdplayers, body kits, spoilers nk. kama unahitaji let me know then nitakutumia picha na full quotation best. gud day

Wakuu,

For God's sake, if you can access internet and visit japanese vehicles suppliers in Japan websites, why should you need to use middlemen to order for a car? Just being amazed!!!!

Tiba
 
Ukweli ni kwamba document hii inabidi isainiwe na bandari pamoja na shipper. Sasa sidhani kuwa shipper anaweza kukubali kuwa kakabidhi gari haina radio wakati inayo. Mimi nilipewa hiyo inspection certificate yenye X kwenye radio/TV/DVD player na nilifuatilia kwa shipper hiyo radio (Gari ilikuwa CIF) mpaka akanitumia ingine ingawaje ilikuwa ya low quality.

Mkuu Chief,

Karatasi niliyoizungumzia mimi haina sehemu ya mwenye meli kusaini labda kama tunazungumzia document tofauti. Clearing agent katika mazingira ya kawaida hawana nafasi ya kuona makabidhiano ya wenye meli na bandari. Agents mara nyingi wanaonyeshwa ile karatasi niliyoizungumzia mimi na ukikuta kitu hakimo kwenye gari, kwa kifupi ukitoka nje ya gate ukasimama ukawauliza washikaji wapi unaweza kupata hicho kitu wanakuletea pale pale na kifaa hicho hicho. Last time kuingiza gari nilikuta wameiba power window za gari isuzu tani 2 na wakati wanaichomoa madirisha yalikuwa wazi. Basi mvua,vumbi kila kitu kilikuwa kinaishia mle kwa kuwa madirisha yalikuwa hayawezi kufunga tena. Niliuziwa hiyo power window hapo tu nje baada ya kutoa gari bandarini kwa elfu themanini.

Fumbuka macho!!!!

Tiba
 
Nataka kuagiza gari nimeshaingia mkataba na beforward co ltd ya Japan kuptia [URL="http://www.tradecarview.com"]www.tradecarview.com[/URL] Sasa nasubiri wadau mnipe taarifa Gari ya mwaka 1994 Suzuki Escudo Nomade je mpaka Bongo JAAI Inspection na Insurance USD 3800. Je nitalipia Ushuru kiasi gani maana mimi nimeipenda sana gari hii. Naombe msaaada wadau

According tu ka dubwana haka http://www.gariyangu.com , nikichkulia cc 1600

Jumla ya kodi: 4,240,990 TZS

Tayarisha 4,533,490 kwa ajili ya kodi na charges nyingne pale bandarini.

Halafu na hela ya agent/dalali wako
 
Nataka kuagiza gari nimeshaingia mkataba na beforward co ltd ya Japan kuptia [URL="http://www.tradecarview.com"]www.tradecarview.com[/URL] Sasa nasubiri wadau mnipe taarifa Gari ya mwaka 1994 Suzuki Escudo Nomade je mpaka Bongo JAAI Inspection na Insurance USD 3800. Je nitalipia Ushuru kiasi gani maana mimi nimeipenda sana gari hii. Naombe msaaada wadau

According tu ka dubwana haka http://gariyangu.appspot.com , nikichkulia cc 1600

Jumla ya kodi: 4,240,990 TZS

Tayarisha 4,533,490 kwa ajili ya kodi na charges nyingne pale bandarini.

Halafu na hela ya agent/dalali wako
 
Mkuu Chief,

Karatasi niliyoizungumzia mimi haina sehemu ya mwenye meli kusaini labda kama tunazungumzia document tofauti. Clearing agent katika mazingira ya kawaida hawana nafasi ya kuona makabidhiano ya wenye meli na bandari. Agents mara nyingi wanaonyeshwa ile karatasi niliyoizungumzia mimi na ukikuta kitu hakimo kwenye gari, kwa kifupi ukitoka nje ya gate ukasimama ukawauliza washikaji wapi unaweza kupata hicho kitu wanakuletea pale pale na kifaa hicho hicho. Last time kuingiza gari nilikuta wameiba power window za gari isuzu tani 2 na wakati wanaichomoa madirisha yalikuwa wazi. Basi mvua,vumbi kila kitu kilikuwa kinaishia mle kwa kuwa madirisha yalikuwa hayawezi kufunga tena. Niliuziwa hiyo power window hapo tu nje baada ya kutoa gari bandarini kwa elfu themanini.

Fumbuka macho!!!!

Tiba

Mkuu hivi mbona kuna wengine wanasema wamekuta vitu vyao havipo na wakakomaa wakapata haki yao?

Mimi nimeongea na mshkaji ambaye anafanya kazi kwenye clearing agent flani na stori anayonipa ni tofauti na unachoongea. Yeye akaniambia kwamba ukiona kitu kimetolewa kuna uwezekano mkubwa agent wako ameshiriki kukuchezea chezo. Na akaniambia kuna karatasi ambayo inaonyesha nini kilikuwapo wakati gari inashuka melini (presumably ndio hiyo ambayo shipper ana-sign pia). Na akaniambia ukizembea uka-sign kupokea kabla hujahakiki hiyo karatasi na gari yako, basi imekula kwako kwa sababu huwezi kurudi na kudai. Lakini ukinotice kabla unadai na bandari wanalipa watu kwa kesi hizo.

Na huyu jamaa sio kwamba alikuwa ananitangazia biashara yao, wala. Alikuwa ananieleza ukweli kama mshakaji. Tafuta mshkaji wako anayefanya clearing & forwarding akupigie story. Utakuja kugundua kwamba agent wako ndio chanzo cha wewe kufisadiwa. Utakupigia story unyama wanaowafanyia watu pale, na utasikitika sana. Kwa mfano (na imeshasemwa hapa) agent anakushawishi u-forge documents, halafu anakuzungusha na kuwatonya jamaa wa TRA. Na kwa sababu ndio ushatenda kosa, watakukamua mpaka utakoma. Baadaye utalalamikia TRA na bandari badala ya kumuuliza agent wako.

Wewe unasema clearing agent katika mazingira ya kawaida hawana nafasi ya kuona makabidhiano ya wenye meli na bandari. Unamaana kuna mazingira ambayo anaweza kuyaona hayo makabidhiano? Na je ni yapi hayo? Na je mahakama haiwezi kuwalazimisha bandari kuyatoa? Na je unaona ni sawa kabisa makabidhiano ya wenye meli na bandari kuwa tofauti? Hivi logic hapo itakuwa ni nini?

Unajua tusijazane ujinga. Kama umeshindwa kupigania haki yako wajanja pale wakakuzidi ujuzi, pengine si vizuri kuwashawishi wengine nao wakawa na uoga wa kupigania haki zao. Na wengi wangekuwa wanakuwa wakali pale, hizi kesi zingekuwa zishaisha sikunyingi. Tumezidi kuwa makondoo na kuendekeza tabia chafu halafu baadaye tunalalama tu.

Inanisikitisha sana kuona jinsi watu wanavyofanyiwa ufisadi wazi wazi hivi na wanaona sawa kabisa, wanakubali yaishe. Hivi wale wa EPA tutawaweza kweli namna hii?

Pengine wewe mkuu ndio inabidi uFumbuke macho!!!!
 
Umegusa kunako! Na hiyo inazidi kuonyesha kwamba kuna vitu tunadhani tunavijua kumbe la, halafu tunakaa tunalalama tu.

Maana nilikuwa nashangaa iweje mtu wa TRA tu ndiye asign kwamba hakuna radio? Hiyo ingekuwa bonge ya loophole ambalo sidhani kwamba lingeweza kuwepo kwa miaka yote hiyo ... maana watu wangekuwa wanaibiwa hovyo zaidi bila kuwa na la kufanya.

Tokea nimeanza kufuatilia hili swala ninazidi kupata picha kwamba tatizo pengine ni watu tu kutokujua taratibu hasa, na haki zao mpaka pale wanapokabidhiwa mzigo. Na jinisi ninavyoendelea kukusanya taarifa ndio nazidi kugundua kwamba baadhi ya watu ambao saa nyingine ndio tunaamini wanajua vizuri hizi taratibu na wanaweza kutusaidia, ndio hawana clue kabisa.

Maagenti wengi hawajui kabisa kodi inakalculatiwa vipi na TRA. Kwa hiyo kwao bado ni muujiza tu. Kufanya jaribio lingine, jana tukampigia dalali mmoja na kumuuliza HRV yangu ya mwaka 2002 ambayo iko njiani inakuja itakatwa kodi kiasi gani akasema 3M mpaka 4M. Nikimuuliza unaipataje, anasema ni kwa uzoefu wake. Kama angekuwa ana clue, pengine angeniuliza CIF ni kiasi gani. Kwa hiyo vitu vinaenda kwa makisio tu. Baadaye unakuta kodi tofauti unawalalmikia TRA badala ya kumuuliza dalali wako.

Siku zote nilikuwa nashangaa iweje vitu vinyofolewe kutoka kwenye gari bandarini halafu kusiwe na utaratibu wowote wa kulalamika na kuwa companseted. Kila "agent" ninayemuuliza analiongelea kama ni swala la kawaida tu, na kwamba ikitokea kubali tu imekula kwako. Kumbe zipo taratibu, na wapo watu wanaofuatilia na kupata haki yao.

Bado kuna maswali mengi tu, na bahati mbaya wale unaodhani ndio wanafahamu na wanaweza kukusaidia hawana ufahamu wa kutosha, na ningetamani sana wangefuatilia kwa undani maana wao ndio wanaoagiza magari mara kwa mara. Mimi naagiza mara moja tu kwa matumizi yangu.

Gari yangu inakuja. Ingawa kodi nikubwa, nitalipa kihalali kabisa.

Sasa ngoja ifike hapa halafu mtu achomoe kitu pale bandarini, au TRA wajifanye wana uplift. Nasema hapatakalika pale na patachimbika ... Kudadeki! Hiyo kesi hata kama itaisha miaka 50 ijayo. Nimehakikisha vielelezo vyangu vyote nnavitunza vizuri.

Eti mtu anaambiwa gari yako si ya bei hiyo halafu anakubali tu kwa sababu TRA wameenda kuangalia gari hiyo hiyo wakakuta bei ni tofauti. Haulizi hata wameangalia wapi huko ambako ndio reference ya bei za magari duniani. Yaana nitawapeleka mpaka mahakama kuu wakaonyeshe hiyo reference ya bei za magari duniani iko wapi. Kudadeki!

Sisi ndio tatizo saa nyingine. Watu vihiyo kabisa wanatengeneza mitandao michafu ya kutunyonya, na si tunakaa na kuafiki kama madunya hivi. Hatujui kwamba TRA wakilipishwa zaidi kwa vifaa vinavyopotea pale ndio hivyo wao watalipa hilo swala umuhimu, sio mpaka JK akawaambie.

Kuhusu malipo ya kodi ya gari yako inayokuja, yawezekana ni kweli utafuata ukweli na haki utapoagiza gari yako, lakini bado unachosema hakijajikamilisha maana TRA hawajahakikisha. Hivi TRA ifanyeje kwa wale wanaocollude na suppliers kuiba kodi? Kwa mfano kuna wanunuaji wanamlipa muuzaji Japan bei ya kweli lakini wanakubaliana na muuzaji kuandika bei pungufu kwenye documents. Hata kama TRA wangekua na list ya bei ya magari yote hapo bado haisaidii, maana kuna lingine lilishawahi kupata ajali kubwa na lingine halikuwahi, ama moja limetumika zaidi ya lingine kwa kipindi kile kile. Hapo ndipo uplifting ya wataalam wa TRA inatakiwa lakini bado mlango wa mnunuaji wa kujieleza na kujitetea utakua wazi. Hata hivyo kikomo cha kufuatilia lazima ukibalance mwenyewe maana storage charge itaendelea kuongezeka na ikifikia limit time gari litapigwa mnaada ili kupunguza msongamano bandarini.
 
Kuhusu malipo ya kodi ya gari yako inayokuja, yawezekana ni kweli utafuata ukweli na haki utapoagiza gari yako, lakini bado unachosema hakijajikamilisha maana TRA hawajahakikisha. Hivi TRA ifanyeje kwa wale wanaocollude na suppliers kuiba kodi? Kwa mfano kuna wanunuaji wanamlipa muuzaji Japan bei ya kweli lakini wanakubaliana na muuzaji kuandika bei pungufu kwenye documents. Hata kama TRA wangekua na list ya bei ya magari yote hapo bado haisaidii, maana kuna lingine lilishawahi kupata ajali kubwa na lingine halikuwahi, ama moja limetumika zaidi ya lingine kwa kipindi kile kile. Hapo ndipo uplifting ya wataalam wa TRA inatakiwa lakini bado mlango wa mnunuaji wa kujieleza na kujitetea utakua wazi. Hata hivyo kikomo cha kufuatilia lazima ukibalance mwenyewe maana storage charge itaendelea kuongezeka na ikifikia limit time gari litapigwa mnaada ili kupunguza msongamano bandarini.

TRA ifanyeje?
Kwani TRA huwa wanafanya nini kwa makampuni na watu wanaokwepa kulipa kodi humu ndani ya nchi? Je, huwa wana-uplift randomly tu kodi za makumpuni na watu jinsi wanavyojiskia? Maana watu wanaotutisha humu ni wale wanaotupa picha kwamba TRA wana-uplift wakijiskia tu. Na wengine humu wanasema wana-uplift pale kunapokuwa na clear signs za kutaka kudanganya. Tumwamini yupi?

Yaani mimi mwenyewe nimepata gari ya bei rahisi, na ingawa kulikuwa na mwanya wa ku-burgain CIF nikaogopa nisije nikawapa kisingizio pale wakiamua ku-uplify halafu nikashindwa kuwasha moto vizuri, maana communication kati ya mimi na jamaa nikielelezo nitakachotumia. Hivi kweli unamaanisha watu waache kununua magari yenye bei nafuu? Saa nyingine anayeuza bei nafuu si kwa sababu limepata ajali. Inawezekana tu kwenye mnada siku hiyo mambo hayakwenda vizuri. Sasa je unamaanisha watanzania waepuke kununua magari rahisi? Mimi nilidhani tunasaidia kuokoa pesa zetu za kigeni pale tunapopata magari nafuu.

Sidhani kwamba ni sahihi kuwa-treat waagiza magari kama wezi vile. Na kumpata mtu aliyedanganya si kazi hivyo. Na mifano tumeshatolewa hapa jinsi gani wanaofoji wanadakwaga kirahisi tu. Nina mshakaji wangu mmoja yeye huwa anaagaazi sana akawa ananipa moyo kwamba ku-forge ni rahisi tu, huwa wanatengeneza invoices nyingine tu hapa hapa. Sasa hii inahitaji rocket science kugundua? Wewe unamfahamu hata mmoja anaye-colude na supplier? Na je, ku-colude huko kunafanyika kwenye magari tu?

Hebu fikiria, ukimpata mtu aliye-forge document unatakiwa u-uplift ama umpeleke polisi?

Mimi nadhani kuna watu wanafaidika na huu mfumo wa hovyo hovyo. Na nia yao kubwa kuifanya iwe painful kufuata njia halali ili ukienda huko kwenye mazabe wao watengeneze mingo. Sasa tunapokaa na kutetea huu upuuzi kama vile mwenye haki ni mkusanya kodi tu na mlipa kodi hana haki yoyote kwa sababu rafiki yake ana colude na ma-supplier, nadhani si sawa. Kila mmoja awajibishwe kwa matendo yake. Kama mimi sijadanganya, basi hunitendei haki kuniadhibu kwa kosa ambalo sijalifanya kwa sababu tu unahisi nimelifanya. Kinachonisikitisha ni pale ninavyoona bandugu mnaona hii ni sawa kabisa. Kwamba mtu anahisi umetenda kosa, hana kielelezo chochote, anakuadhibu na wewe unakubali tu.

Sasa mimi nasema, waki-uplift nitatafuta hiyo hela nitawalipa ili kuiondoa hapo bandarini nianze kuitumia. Halafu hiyo kesi yake itafika mpaka kwa mkuu wa TRA. Ikishindikana itaenda mahakamani, hata iishe baada ya miaka 100, nitakula nao sahani moja, kudadeki!!! Na watanilipa gharama zangu zote za usumbufu.

Nikienda pale bandarini ntakuwa na camera yangu, kila niayeongea naye nnampiga picha, maana ataweza kuwa shahidi wangu baadaye atake asitake. Na nimeshaagiza kinasa sauti kidogo cha kujificha, kitafika kabla ya gari.

Hivi sisi tunamatatizo gani? Kuna kampuni imekuuzia gari, invoices unazo, bank transfer unazo, kampuni ipo hapa hapa duniani hata wao TRA wanaweza ku-communicate nao ku-verify. Halafu TRA wanakwambia hujanunua kwa bei hiyo wewe unakubali tu? Na unajipa moyo kabisa kwamba ulilofanyiwa ni sawa kwa sababu kuna rafiki zako huwa wana-forge documents. Namna hii tutaendelea kuwa watumwa nchini kwetu mpaka mwisho wa dunia.

Kwa maelezo ambayo tumeshayapata hapa kutoka kwa waungwana wengine, nawapa TRA benefit of the doubt. Kwamba siku hizi wanaokumbana ku-uplift ni wale wanaojaribu ku-forge documents either kwa kushawishiwa na agents wao au kwa utashi wao wenyewe. Unaambiwa leta bank slip, unaleta yenye value zaidi ya CIF yako. Unaambiwa fungua email yako hapo tuangalie hayo maongezi yenu, unaanza kutetemeka. Halafu baadaye unawalaumu TRA.
 
Tatizo kusema ukweli wala siyo TRA tatizo ni hawa maagent, kiukweli mimi ningeruhusu tu kila mwenye mzigo wake afuatilie mwenyewe kuutowa, kuna gharama kibao ambazo unalipia zinakuwa hazina risiti, sijui lete laki ya kusukumia document, sijui toa elfu sabin hili tulipie dirishana ama sivyo itabidi tukalipe bank,yani sehemu nyingi anaingia agent wewe unasubiri agent wako atakuja kukwambia nini, halafu ni wao maagent ndiyo wanaotishia sijui document zimekwama. mimi kwa ushauri wangu serikali ingeruhusu kila mtu anayeweza kutoa mzigo wake atoe na anayetaka kutumia agent atumie,unajuwa muhusika ukiwa mwenyewe front kila kitu kinakwenda vizuri kama kuna kitu wanataka kujuwa watakuuliza mwenyewe siyo kwanza agent naye ndiyo aje kwako, yani mpaka kibabu kinachoshusha document chini unaambiwa ukipe pesa ndiyo itakuwa faster.maagent kibao muhuri wanaotegemea ni wa mtu mmoja. urasimu urasimu urasimu kila sehemu,
 
Dully jibu maswali yetu, politics nyingine ziache humu, tatizo kila mtu ana experience yake, wengine wanalia wengine wanacheka, wale wanaocheka wanawalazimisha wengine waamini cheka yao.

mambo yakibadilika unakuwa mwenyewe na leso yako machozi!
 
hiyo BOL umemaanisha Bill OF lading? kama ni hiyo huwa hawaandiki options za gari zaidi ya chasisi no na mwaka tu. hata ukisema ubishane bandarini kwa kuibiwa dvd player ya laki 1 lakini ikasababisha ujiongezee storage huoni utakuwa unapoteza muda bure bila ya kupata chochote.
pia inawezekana kabisa kwa watu wawili kuleta gari sawasawa ila mkalipia ushuru tofauti. hayo yalinikuta mie mwenyewe nilinunua toyota raum 2 zote za mwaka 2000 ila moja walinipiga ushuru 1.7ml na nyingine walinipiga 2.2ml.

Ivi ishu kama hii huwezi kwenda mahakamani?
 
Mkuu hivi mbona kuna wengine wanasema wamekuta vitu vyao havipo na wakakomaa wakapata haki yao?

Mimi nimeongea na mshkaji ambaye anafanya kazi kwenye clearing agent flani na stori anayonipa ni tofauti na unachoongea. Yeye akaniambia kwamba ukiona kitu kimetolewa kuna uwezekano mkubwa agent wako ameshiriki kukuchezea chezo. Na akaniambia kuna karatasi ambayo inaonyesha nini kilikuwapo wakati gari inashuka melini (presumably ndio hiyo ambayo shipper ana-sign pia). Na akaniambia ukizembea uka-sign kupokea kabla hujahakiki hiyo karatasi na gari yako, basi imekula kwako kwa sababu huwezi kurudi na kudai. Lakini ukinotice kabla unadai na bandari wanalipa watu kwa kesi hizo.

Na huyu jamaa sio kwamba alikuwa ananitangazia biashara yao, wala. Alikuwa ananieleza ukweli kama mshakaji. Tafuta mshkaji wako anayefanya clearing & forwarding akupigie story. Utakuja kugundua kwamba agent wako ndio chanzo cha wewe kufisadiwa. Utakupigia story unyama wanaowafanyia watu pale, na utasikitika sana. Kwa mfano (na imeshasemwa hapa) agent anakushawishi u-forge documents, halafu anakuzungusha na kuwatonya jamaa wa TRA. Na kwa sababu ndio ushatenda kosa, watakukamua mpaka utakoma. Baadaye utalalamikia TRA na bandari badala ya kumuuliza agent wako.

Wewe unasema clearing agent katika mazingira ya kawaida hawana nafasi ya kuona makabidhiano ya wenye meli na bandari. Unamaana kuna mazingira ambayo anaweza kuyaona hayo makabidhiano? Na je ni yapi hayo? Na je mahakama haiwezi kuwalazimisha bandari kuyatoa? Na je unaona ni sawa kabisa makabidhiano ya wenye meli na bandari kuwa tofauti? Hivi logic hapo itakuwa ni nini?

Unajua tusijazane ujinga. Kama umeshindwa kupigania haki yako wajanja pale wakakuzidi ujuzi, pengine si vizuri kuwashawishi wengine nao wakawa na uoga wa kupigania haki zao. Na wengi wangekuwa wanakuwa wakali pale, hizi kesi zingekuwa zishaisha sikunyingi. Tumezidi kuwa makondoo na kuendekeza tabia chafu halafu baadaye tunalalama tu.

Inanisikitisha sana kuona jinsi watu wanavyofanyiwa ufisadi wazi wazi hivi na wanaona sawa kabisa, wanakubali yaishe. Hivi wale wa EPA tutawaweza kweli namna hii?

Pengine wewe mkuu ndio inabidi uFumbuke macho!!!!

Mkuu,

Naona umewaka kweli kweli, tulia, hapa tunaelimishana tu. Ukweli ni kwamba mimi nikiagiza gari sihitaji msaada wa agent kufanya hiyo kazi. Hata hivyo agent anakuwa hayupo wakati gari linashushwa kutoka kwenye meli na hivyo naogopa kuwahusisha na huu wizi. Ukweli ni kwamba ukikuta vitu vyako havimo na ukataka kulinganisha hiyo report ya Bandari na ile ya report ya makabidhiano ya wenye meli na bandari inawezekana ukapata haki yako. Lakini do you know how much is going to cost you in terms of time and the like?.

Nakumbuka kuna kipindi fulani Bwana mmoja ambaye ni lecturer pale UDSM, Adolf Mkenda alijaribu kuanzisha kitu kama public awareness kuhusu huu wizi na akawa anajaribu kuhamasisha watu wasikubali kuchukua magari yao endapo watakuta vitu vyao vimeibiwa. Sijui kampeni yake ilifanikiwa kiasi gani.

Kama muda unakuruhusu na kwamba huko tayari kupambana na hao jamaa wa Bandari nina uhakika unapata haki yako. Katika mazingira ya kawaida, watu wa meli hawaibi vitu kwenye magari hata kidogo.

Tiba
 
Dully jibu maswali yetu, politics nyingine ziache humu, tatizo kila mtu ana experience yake, wengine wanalia wengine wanacheka, wale wanaocheka wanawalazimisha wengine waamini cheka yao.

mambo yakibadilika unakuwa mwenyewe na leso yako machozi!

Mzee mie naamini humu kuna vichwa vingi ndo maana nimekaa zangu kimya ili na mie nipate kuongeza vi2 vipya kutoka kwao. kuhusu gari kuchomolewa vi2 kwa kweli nashukuru nishaleta gari kama 24 hivi mpaka sasa na hakuna hata 1 iliyowahi kuchomolewa kitu so swala hl nitawaachia wadau walimalize
 
TRA hakuna sijui ya kuwa na vielelezo wala nini, mimi nimewapelekea vyote yani copy ya T/T,bima iliyokatwa japan inaonyesha gharama halisi za gari yani kila kitu nimepeleka na nilikuwa beneti mno na agent mpaka nimetoa, jamaa walichosema wao wana viwango vyao haijalishi CIF yako ni ngapi.

ushauri wangu wa bure, kabla ya kununua gari ni vizuri ukajuwa hiyo gari hiko kwenye kiwango gani TRA, unaweza ukanunua gari CIF 2000 USD, ukaja wekewa 4000 USD. ulizieni kwanza kabla ya kuagiza.

kama kuna mtu wa TRA anapita pita humu, tunawaomba hizo bei zenu za magari mziweke mtandaoni, hili mtu anunuapo ajuwe ni nini kitamkuta.
 
Dullymo asante kwa info yako ila nauliza hizo kampuni ambazo ni fake za tradecarview ni zipi? Tupe hizo. Halafu kuna tabia ya kampuni zingine za Japan kutumia wakala wao ili gari ikija ipitie kwa wakala kabla ya wewe kukabidhiwa? Hii si inaongeza gharama? Watu wengi hawalijui hili. Nadhani ni kuwaambia utalitoa mwenyewe hivyo kusiwe na middleman yeyote. Hebu nipe ufafanuzi.
 
TRA hakuna sijui ya kuwa na vielelezo wala nini, mimi nimewapelekea vyote yani copy ya T/T,bima iliyokatwa japan inaonyesha gharama halisi za gari yani kila kitu nimepeleka na nilikuwa beneti mno na agent mpaka nimetoa, jamaa walichosema wao wana viwango vyao haijalishi CIF yako ni ngapi.

ushauri wangu wa bure, kabla ya kununua gari ni vizuri ukajuwa hiyo gari hiko kwenye kiwango gani TRA, unaweza ukanunua gari CIF 2000 USD, ukaja wekewa 4000 USD. ulizieni kwanza kabla ya kuagiza.

kama kuna mtu wa TRA anapita pita humu, tunawaomba hizo bei zenu za magari mziweke mtandaoni, hili mtu anunuapo ajuwe ni nini kitamkuta.

Pole kwa maswahibu hayo.

Ilikuwa lini hii mkuu?
 
Dullymo asante kwa info yako ila nauliza hizo kampuni ambazo ni fake za tradecarview ni zipi? Tupe hizo. Halafu kuna tabia ya kampuni zingine za Japan kutumia wakala wao ili gari ikija ipitie kwa wakala kabla ya wewe kukabidhiwa? Hii si inaongeza gharama? Watu wengi hawalijui hili. Nadhani ni kuwaambia utalitoa mwenyewe hivyo kusiwe na middleman yeyote. Hebu nipe ufafanuzi.

ukifungua page ya tradcarview nenda kwenye blcklist na utayaona hayo makampuni. kuna nyngne zimefungwa kw kuchelewa ku2mamagari au documents, kuna nyngn zimefungiwa kwa kukata mawacliano na mteja mara bada ya ku2ma pesa nk. ila mby zaidi wanabadili majina kisha wanajiregster upya. je 2tapona??. kuhusu ku2mia maagent wao wanafanya vile ili uwe na imani juu yao kwamb wao co wezi coz hao maagent wana act kama wawakhlishi wao incase wamekuibia unaweza kuwashtaki wao
 
nimecheka sana niliposoma kwenye gazeti kuna watu wameibiwa kwa kununua magari mtandaoni. dully umeongea ukweli ila watu wabishi
 
hello JF bros n sisz!
watu wengi wamekuwa wakitaka kuagiza magari kwa njia ya mtandao. ni njia rahisi na inayosave muda na gharama nyingine kama nauli nk na unapata gari kwa bei poa. mimi ni miongoni mwa wanaoleta magari kwa njia hiyo na nigependa niwape points muhimu ambazo zitawasaidia wale wanaotaka kuleta magari kwa njia hiyo.

Habari za kazi,

Naulizia hivi nikitaka kuagiza gari RAV4-J yaani gharama ya kuagiza mpaka kuitoa jumlisha kulipia na TRA ya hapa kila kitu ni shs./usd Ngapi?
Nitashukuru msaada wako wa maelezo.
 
Back
Top Bottom